kuwa mwenye kusamehe, na faida zake

27.

kuwa mwenye kusamehe, na faida zake

27. Kuwa Mwenye Kusamehe



Muislamu anatakiwa ajenge tabia ya kuwavumilia wengine. Awe na tabia ya kujihesabu. Ajione kuwa naye kama binaadamu wenzake ni mkosaji na angependa asamehewe na wale aliowakosea kwa makusudi au kwa bahati mbaya. Kitendo cha kuwasamehe wale waliokukosea ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w) kama inavyobainishwa katika aya zifuatazo:


“Na yaendeeni upesi upesi maghufira ya Mola wenu na Pepo (yake) ambayo upana wake (tu) ni (sawa na) mbingu na ardhi. (Pepo) iliyowekewa wamchao Mungu. Ambao hutoa katika (hali ya) wasaa na katika (hali ya) dhiki, na wazuiyao ghadhabu na wanasamehe watu na Mw enyezi Mungu anawapenda wafanyao ihsani. ” (3:133-134)


“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilichoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele). Watakistahiki wale walioamini na wakawa wanamtegemea Mola wao.(42:36)
“Na wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na mambo


mabaya, na wale ambao wanapokasirika husamehe. (42:37)
Mwenye kuwasamehe wengine husamehewa makosa yake na Allah


“Na wasiape wale wenye mwendo mzuri (waumini) na wenye wasaa (katika maisha yao) miongoni mwenu (wasiape kujizuia) kuwapa walio jamaa na maskini na waliohama kwa njia ya Mwenyezi Mungu; na w aachilie mbali, (wapuuze yaliyopita). Je, nyinyi hampendi Mwenyezi Mungu akusameheni? Na Mwenyezi Mungu ni Mw ingi w a msamaha (na) Mwingi wa Rehema. (24:22).



Naye Mtume (s.a.w) anatufahamisha ubora wa kusamehe katika Hadithi zifuatazo:
‘Uqbah bin Amir (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Ee ‘Uqbah! Je, nikufahamishe juu ya watu wema kuliko w ote katika dunia hii na akhera?” Alijibu Ndio, akasema (Mtume): “Utaendeleza uhusiano mwema na mtu aliyevunja uhusiano kati yako na yeye; utampa yule aliyekunyima; na utamsamehe yule aliyekudhulumu”. (Baihaqi).



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema kuwa Mussa (a.s), mwana wa Imran, aliuliza: Ee Mola wangu! Nani, katika waja wako anayeheshimika (mwenye hadhi) zaidi mbele yako? (Allah) alimjibu: Yule anayesamehe ambapo ana nguvu au uwezo (wa kutosamehe). (Ba ih aqi).
Hivyo Allah (s.w) anatuusia:


“Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili...” (7:199)


Kukataa kusamehe baada ya kuombwa msamaha na yule aliyekukosea ni jambo ovu. Allah (s.w) hamsamehi yule asiyesamehe wanaadamu wenzake. Ukweli ni kwamba wanayotukosea wanaadamu wenzetu hata tuyaone ni makubwa vipi, ni madogo sana ukilinganisha na makosa yetu kwa Allah (s.w). Inakuwaje sasa tushindwe kusamehe haya makosa madogo madogo na wakati huo tunatamani kusamehewa milima na milima ya makosa yetu?



Hivyo, yule anayetaka kusamehewa na Allah(s.w), basi awe mwepesi wa kuwasamehe wanaadamu wenzake. Kuhusu uovu wa kukataa kuwasamehe wale waliokiri makosa yao na kuomba msamaha, anasema Mtume (s.a.w):



Kama mtu, anakiri makosa yake kwa mwingine na kutaka msamaha, na yule akakataa kutoa msamaha, basi hatanyweshwa maji ya kawthar (huyo aliyekataa, kusamehe). (Tabrani).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2641

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kitabu Cha Dua 120

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe

Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi.

Soma Zaidi...
Neno la awali

Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.

Soma Zaidi...
nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

Soma Zaidi...
Mawaidha Kutokwa kwa Shekhe

Karibu kwenye Darsa za mawaidha na Mafundisho ya dini.

Soma Zaidi...