kuwa mwenye kusamehe, na faida zake

27.

kuwa mwenye kusamehe, na faida zake

27. Kuwa Mwenye Kusamehe



Muislamu anatakiwa ajenge tabia ya kuwavumilia wengine. Awe na tabia ya kujihesabu. Ajione kuwa naye kama binaadamu wenzake ni mkosaji na angependa asamehewe na wale aliowakosea kwa makusudi au kwa bahati mbaya. Kitendo cha kuwasamehe wale waliokukosea ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w) kama inavyobainishwa katika aya zifuatazo:


'Na yaendeeni upesi upesi maghufira ya Mola wenu na Pepo (yake) ambayo upana wake (tu) ni (sawa na) mbingu na ardhi. (Pepo) iliyowekewa wamchao Mungu. Ambao hutoa katika (hali ya) wasaa na katika (hali ya) dhiki, na wazuiyao ghadhabu na wanasamehe watu na Mw enyezi Mungu anawapenda wafanyao ihsani. ' (3:133-134)


'Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilichoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele). Watakistahiki wale walioamini na wakawa wanamtegemea Mola wao.(42:36)
'Na wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na mambo


mabaya, na wale ambao wanapokasirika husamehe. (42:37)
Mwenye kuwasamehe wengine husamehewa makosa yake na Allah


'Na wasiape wale wenye mwendo mzuri (waumini) na wenye wasaa (katika maisha yao) miongoni mwenu (wasiape kujizuia) kuwapa walio jamaa na maskini na waliohama kwa njia ya Mwenyezi Mungu; na w aachilie mbali, (wapuuze yaliyopita). Je, nyinyi hampendi Mwenyezi Mungu akusameheni? Na Mwenyezi Mungu ni Mw ingi w a msamaha (na) Mwingi wa Rehema. (24:22).



Naye Mtume (s.a.w) anatufahamisha ubora wa kusamehe katika Hadithi zifuatazo:
'Uqbah bin Amir (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 'Ee 'Uqbah! Je, nikufahamishe juu ya watu wema kuliko w ote katika dunia hii na akhera?' Alijibu Ndio, akasema (Mtume): 'Utaendeleza uhusiano mwema na mtu aliyevunja uhusiano kati yako na yeye; utampa yule aliyekunyima; na utamsamehe yule aliyekudhulumu'. (Baihaqi).



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema kuwa Mussa (a.s), mwana wa Imran, aliuliza: Ee Mola wangu! Nani, katika waja wako anayeheshimika (mwenye hadhi) zaidi mbele yako? (Allah) alimjibu: Yule anayesamehe ambapo ana nguvu au uwezo (wa kutosamehe). (Ba ih aqi).
Hivyo Allah (s.w) anatuusia:


'Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili...' (7:199)


Kukataa kusamehe baada ya kuombwa msamaha na yule aliyekukosea ni jambo ovu. Allah (s.w) hamsamehi yule asiyesamehe wanaadamu wenzake. Ukweli ni kwamba wanayotukosea wanaadamu wenzetu hata tuyaone ni makubwa vipi, ni madogo sana ukilinganisha na makosa yetu kwa Allah (s.w). Inakuwaje sasa tushindwe kusamehe haya makosa madogo madogo na wakati huo tunatamani kusamehewa milima na milima ya makosa yetu?



Hivyo, yule anayetaka kusamehewa na Allah(s.w), basi awe mwepesi wa kuwasamehe wanaadamu wenzake. Kuhusu uovu wa kukataa kuwasamehe wale waliokiri makosa yao na kuomba msamaha, anasema Mtume (s.a.w):



Kama mtu, anakiri makosa yake kwa mwingine na kutaka msamaha, na yule akakataa kutoa msamaha, basi hatanyweshwa maji ya kawthar (huyo aliyekataa, kusamehe). (Tabrani).




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 404


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

utaratibu wa lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...

Namna ya kuswali
2. Soma Zaidi...

Hijabu na kujikinga na zinaa
Soma Zaidi...

KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' '?... Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)
SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Ghasia na chokochoko za Makhawariji na kuuliwa kwa Ally
Soma Zaidi...

DARSA ZA NDOA, FAMILIA, SIASA, BIASHARA, UCHUMI, HAKI NA SHERIA KATIKA UISLAMU
1. Soma Zaidi...

Namna ya Kutayamam hatua kwa hatua, suna zake nguzo za kutayamam na masharti ya kutayamam
Soma Zaidi...

Dua Sehemu ya 01
Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua? Soma Zaidi...

Quran haikutoka kwa Mtu zezeta wala mwenye upungufu wa akili
Soma Zaidi...