22.
22. Kuwa Mpole na Mnyenyekevu
        Mtu mpole ni yule aliyetulia, asiyelipuka kwa hamaki. Huzungumza na watu kwa sauti ya chini. Akiudhiwa halipuki kwa hasira na kupaza sauti bali husubiri kwa utulivu. Huwa ni mwepesi wa kuwasamehe waliomkosea. Muumini hana budi kujipamba na sifa hii ya upole kwani ni miongoni mwa sifa za waja wema wa Allah (s.w)
“Na waja wa Rahman ni wale wanokwenda (na kurejea) katika ardhi kwa unyenyekevu; na wajinga wakisema nao (maneno mabaya) huwajibu (maneno ya) salama”. (25:63)
Pamoja na kujipamba na tabia ya upole, Waislamu hawaruhusiwi kuyaachia maovu yakafanyika katika jamii bila ya kuyakemea. Ni juu ya Waumini kuamrisha mema na kukataza maovu na kuwa wagumu kwa maadui wa Uislamu na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Hii ndiyo tabia ya Mtume na Maswahaba wake kama tunavyojifunza katika Qur’an:
“Muhammad ni Mtume wa Allah na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti (ngumu) dhidi ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao...” (48:29).
        Pindi maadui wakiacha uadui wao dhidi ya Uislamu, waislamu watawaelekea kwa upole:
“Na kama (hao maadui) wakielekea katika amani, wewe pia ielekee (amani) na mtegemee Allah. Hakika yeye ndiye asikiaye na ajuaye.Na kama wakitaka kukuhadaa basi Allah atakutosheleza. Yeye ndiye aliyekusaidia kwa nusura yake na kwa walioamini”. (8:61-62).
Umeionaje Makala hii.. ?
Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?
Soma Zaidi...Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.
Soma Zaidi...Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.
Soma Zaidi...Tumesha mzika maiti sasa imebakia mali yae nyumbani, watoto, wake na menginyeo.
Soma Zaidi...Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.
Soma Zaidi...Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani.
Soma Zaidi...