22.
22. Kuwa Mpole na Mnyenyekevu
Mtu mpole ni yule aliyetulia, asiyelipuka kwa hamaki. Huzungumza na watu kwa sauti ya chini. Akiudhiwa halipuki kwa hasira na kupaza sauti bali husubiri kwa utulivu. Huwa ni mwepesi wa kuwasamehe waliomkosea. Muumini hana budi kujipamba na sifa hii ya upole kwani ni miongoni mwa sifa za waja wema wa Allah (s.w)
“Na waja wa Rahman ni wale wanokwenda (na kurejea) katika ardhi kwa unyenyekevu; na wajinga wakisema nao (maneno mabaya) huwajibu (maneno ya) salama”. (25:63)
Pamoja na kujipamba na tabia ya upole, Waislamu hawaruhusiwi kuyaachia maovu yakafanyika katika jamii bila ya kuyakemea. Ni juu ya Waumini kuamrisha mema na kukataza maovu na kuwa wagumu kwa maadui wa Uislamu na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Hii ndiyo tabia ya Mtume na Maswahaba wake kama tunavyojifunza katika Qur’an:
“Muhammad ni Mtume wa Allah na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti (ngumu) dhidi ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao...” (48:29).
Pindi maadui wakiacha uadui wao dhidi ya Uislamu, waislamu watawaelekea kwa upole:
“Na kama (hao maadui) wakielekea katika amani, wewe pia ielekee (amani) na mtegemee Allah. Hakika yeye ndiye asikiaye na ajuaye.Na kama wakitaka kukuhadaa basi Allah atakutosheleza. Yeye ndiye aliyekusaidia kwa nusura yake na kwa walioamini”. (8:61-62).
Umeionaje Makala hii.. ?
Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu.
Soma Zaidi...Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.
Soma Zaidi...Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali.
Soma Zaidi...Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.
Soma Zaidi...