.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu

3.

.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu

3.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu Kanuni kuu za uchumi katika Uislamu ni:



(i)Kumwamini Allah kuwa ndiye Muumba na mfalme wa ulimwengu huu yaani kumtii Allah katika mambo yote.



(ii)Binaadamu ni Khalifa wa Allah hapa duniani, hivyo wajibu wake ni kusimamisha amri ya Allah.



(iii)Ili kumsaidia mwanaadamu kutimiza wajibu wake kama Khalifa, Allah amemdhalilishia kila kitu katika ulimwengu huu:


“Mw enyezi Mungu ndiye aliyekutiishieni bahari ili humo zipite merikebu kwa amri yake ili mtafute fadhila yake na mpate kushukuru ”. (45:12).


“Je, Hukuona kwamba Mwenyezi Mungu amevitiisha kwa ajili yenu vilivyomo ardhini…” (22:65)


“Je, Hukuona kwamba Mwenyezi Mungu amekutiishieni vilivyomo mbinguni na ardhini na anakukamilishieni neema zake zilizo dhahiri na za siri? …” (31:20).



“Yeye ndiye aliyefanya ardhi iweze kutumika kwa ajili yenu. Basi nendeni katika pande zake zote na kuleni katika rizki zake na kwake ndiyo marejeo.” (67:15).
Hivyo kuzitumia neema hizo za Allah si dhambi bali ni katika kushukuru.



(iv)Kutokana na wajibu wa Ukhalifa wa Allah, mwanaadamu ataulizwa kwa neema alizompatia na atahesabiwa kwazo, ikiwa ni pamoja na namna alivyochuma na kutumia mali.



(v) Kuwa na mali au kutokuwa na mali nyingi au kidogo si dalili ya ubora au udhalili wa mtu. Hali zote mbili ni mtihani. Anachotazama Allah ni nyoyo za watu. Misingi au kanuni hizo zikithibiti katika moyo wa mtu zinakuwa na athari kubwa sana katika shughuli za kiuchumi za Muislamu.



Kanuni ya kwanza kwa mfano humfanya mtu afuate maamrisho ya Allah na hivyo atafanya kila njia ajiepushe na makatazo yake.



Pili, kwa kujua kuwa yeye ni Khalifa tu atajua yeye si mmilikaji wa hakika, hivyo atafuata maagizo ya huyo aliyempa ukhalifa yaani Allah.



Tatu, atajua kuwa utajiri si kitu cha kukipigania, bali mtu apiganie maisha bora na afya katika kutafuta radhi za Allah (s.w).



Nne, kwa kujua kuwa atahesabiwa na Allah anayeshuhudia kila kitu ataendesha shughuli zake za kiuchumi kwa kumcha Allah.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1131

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq

Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Kutoa vilivyo vizuri

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...