Madhara ya matusi katika jamii, na Kujiepusha na Matusi

15.

Madhara ya matusi katika jamii, na Kujiepusha na Matusi

15. Kujiepusha na Matusi


Mtu anayetukana ana lengo la kumdhalilisha mwingine. Waislamu tumekatazwa kutukanana na hata kuitana majina tusiyoyapenda kwa k ej eli.
“.... Wala msitukanane kwa kabila wala msiitane majina mabaya (ya kejeli). Jina baya kabisa kuitwa mtu ni “Fasiqi” baada ya kuwa yeye ni Muislamu. Na wasiotubu basi hao ndio madhalimu ”. (49:11)


Fasiq ni yule aliyebobea katika uasi. Yaani mtu anayejizatiti kumuasi Allah (s.w) kwa namna mbali mbali kama vile mwizi, mlevi,

mzinzi na kadhalika. Ni vibaya mno mbele ya Allah (s.w) kumsingizia au kumwita Muislamu ”mwizi” na huku si mwizi au kumwita “mnafiki” au “kafir” na huku ni Muislamu kamili. Tabia hii imekemewa vikali katika Qur-an:

“Kwa yakini wale wanaopenda uenee uovu kwa wale walioamini watapata adhabu iumizayo katika dunia na katika akhera, na Allah ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui”. (24:19).
Kutokana na makemeo haya, Muumini wa kweli hana budi kujiepusha na tabia ya kuwaita watu kwa majina mabaya kwani kufanya hivyo mtu hujilaani mwenyewe kiasi kwamba hayo majina mabaya yatamgeukia, kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Abu Dh-dhari(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Hapana mtu atakayemsingizia mwingine uasi kwa Allah au akamwita “kafiri”, ila hayo yatamgeukia yeye mwenyewe iwapo huyo aliyemsingizia hayuko hivyo”. (Bukhari)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 1443

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Zoezi la 3

Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Dua 120

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI WAKE.

Soma Zaidi...
Assalam Baada yakufariki wazazi wake mtume alilelewa nanani???

Mtume Muhammad s.a.w amezaliwa yatima asiyena baba. Lakini hii haikumfanya asipate maelezo bora yaliyo mazuri. Je unajuwa aliyemlea baada ya kufariki kwa mama yake?.

Soma Zaidi...