dharura

14.

14. Kujiepusha na Dharau


Kudharau wengine ni tabia mbaya na ni kitendo kiovu mbele ya Allah (s.w). Katazo la kuwadharau watu liko bayana katika Qur-an:

“Enyi mlioamini! Wanaume wasiw adharau wanaume wenzao, huwenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao; huwenda wakawa bora kuliko wao...” (49:11)
Mwenye kuwadharau wengine hujihisi kuwa yeye ni bora kuliko hao anaowadharau. Hili ni kosa kubwa kwani anaye mjua aliye mbora ni Allah (s.w) Pekee kama tunavyojifunza katika Qur-an:

“Enyi Watu! Kwa hakika tumekuumbeni(nyote) kutoka kwa (yule) mwanaume(mmoja; Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja; Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbalimbali) ili mjuane. Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika ninyi. Kw a yakini Mw enyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye habari (49:13).
Aya hii kwa ujumla inatuwekea msingi wa usawa. Inatukumbusha kuwa watu wote asili yao ni moja; ni watoto wa Adam ambaye ameumbwa kutokana na udongo.

“Na tulimuumba mtu kwa udongo mkavu unaotoa sauti, wenye kutokana na matope meusi yaliyovunda. ” (15:26).
Tofauti za rangi, kabila, taifa n.k. ziko pale kwa ajili ya anuani tu na kamwe zisiwe msingi wa kubaguana na kudharauliana. Pia tofauti za vipawa zilizopo kati ya watu kama vile elimu, utajiri, ufalme, n.k. isiwe sababu ya kubaguana. Vipawa hivyo ametunukiwa mwanaadamu kama mtihani kwake.Ama atamshukuru Mola wake kwa kutumia vipawa hivyo kwa ajili yake kama inavyostahiki awe mwenye kufaulu au atatakabari kwa kutumia vipawa hivyo apendavyo kinyume na maagizo ya Mola wake awe ni mwenye kufeli.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 451

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 web hosting    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Uhakiki wa hadithi za mtume

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
(xi)Hutoa Zakat na Sadakat

Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakat wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza.

Soma Zaidi...
Fadhila za kujenga msikiti

Kuna malipo makubwa kwa ambaye amejenga msikiti kwa ajili ya kuoatavradhi za Allah.

Soma Zaidi...
(viii)Wenye khushui katika swala

Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala.

Soma Zaidi...
Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nani Muadilifu na zipi sifa za mtu muadilifu kwenye uislamu

Uadilifu ni usimamizi wa ukweli na kutoa haki kwa kila anayestahiki kulingana na ukweli.

Soma Zaidi...