image

dharura

14.

14. Kujiepusha na Dharau


Kudharau wengine ni tabia mbaya na ni kitendo kiovu mbele ya Allah (s.w). Katazo la kuwadharau watu liko bayana katika Qur-an:

“Enyi mlioamini! Wanaume wasiw adharau wanaume wenzao, huwenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao; huwenda wakawa bora kuliko wao...” (49:11)
Mwenye kuwadharau wengine hujihisi kuwa yeye ni bora kuliko hao anaowadharau. Hili ni kosa kubwa kwani anaye mjua aliye mbora ni Allah (s.w) Pekee kama tunavyojifunza katika Qur-an:

“Enyi Watu! Kwa hakika tumekuumbeni(nyote) kutoka kwa (yule) mwanaume(mmoja; Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja; Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbalimbali) ili mjuane. Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika ninyi. Kw a yakini Mw enyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye habari (49:13).
Aya hii kwa ujumla inatuwekea msingi wa usawa. Inatukumbusha kuwa watu wote asili yao ni moja; ni watoto wa Adam ambaye ameumbwa kutokana na udongo.

“Na tulimuumba mtu kwa udongo mkavu unaotoa sauti, wenye kutokana na matope meusi yaliyovunda. ” (15:26).
Tofauti za rangi, kabila, taifa n.k. ziko pale kwa ajili ya anuani tu na kamwe zisiwe msingi wa kubaguana na kudharauliana. Pia tofauti za vipawa zilizopo kati ya watu kama vile elimu, utajiri, ufalme, n.k. isiwe sababu ya kubaguana. Vipawa hivyo ametunukiwa mwanaadamu kama mtihani kwake.Ama atamshukuru Mola wake kwa kutumia vipawa hivyo kwa ajili yake kama inavyostahiki awe mwenye kufaulu au atatakabari kwa kutumia vipawa hivyo apendavyo kinyume na maagizo ya Mola wake awe ni mwenye kufeli.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 147


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

kuwa mwenye kusamehe, na faida zake
27. Soma Zaidi...

(xi)Hutoa Zakat na Sadakat
Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakat wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza. Soma Zaidi...

viapo
20. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Quran na sayansi
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah
Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Soma Zaidi...

Uhakiki wa hadithi za mtume
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Elimu
Uwanja wa elimu na maarifa Soma Zaidi...

(xiii)Huwa muaminifu
Waumini wa kweli waliofuzu huchunga amana. Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NENO LA AWALI
Darasa la elimu inayohusu ujauzito na namna ya kulea mimba Soma Zaidi...

jamii somo la 26
(vii)Hufanya bias hara na Allah (s. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Dua 120
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...