Menu



Kuwa na mwenye haya, na faida zake

24.

Kuwa na mwenye haya, na faida zake

24. Kuwa na Haya



Kuwa na haya ni miongoni mwa tabia njema. Mtu mwenye haya ni yule anayejichunga na maovu na mambo ya aibu. Kuhusu umuhimu wa kuwa na haya, tunajifunza katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Haya ni sehemu ya imani na imani mahali pake ni Peponi; na uchafu (uovu) ni sehemu ya ugumu wa moyo na ugumu wa moyo mahali pake ni Motoni. (Ahmad, Tirmidh).



Ibn Mas โ€™ud amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Miongoni mwa ujumbe watu waliopokea kutokana na mafundisho ya mwanzo ya Utume ni: Wakati unapokuwa huna haya, fanya ulitakalo. (Bukhari).



Hapa ina maana kuwa mtu asiye na haya hachagui la kufanya au la kusema. Pia Mtume (s.a.w) amesema katika Hadithi iliyosimuliwa na Imran bin Husain kuwa:
Haya haileti kitu kingine ila uzuri na katika maelelezo mengine; Haya ni nzuri katika kila hali. (Bukhari na Muslim).
Mtume (s.a.w) ambaye ndiye kiigizo chetu alikuwa ni mwenye haya sana kama Hadithi ifuatayo inavyobainisha:


Abu Said al-Khudri (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa na haya zaidi kuliko wasichana vigori ndani ya mitandio yao. Alipoona kitu kisichopendeza kwake tulikuwa tunakigundua kutokana na uso wake. (Bukhari na Muslim).



Muislamu anatakiwa awe na haya katika maongezi, katika kuangalia na katika kujisitiri uchi na katika kufanya kila jambo. Haya ni ngao ya kumuepusha mja na mambo maovu na machafu. Wa kwanza anayestahiki kuonewa haya ni Allah (s.w) kwani mwanaadamu hana kificho chochote cha kumsitiri asionekane kwake. Hivyo mja anayemuamini Allah (s.w) atamuonea haya na kujiepusha na maovu na machafu katika maisha yake yote popote atakapokuwa.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 846

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Uchambuzi wa hadithi za mtume

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Elimu

Uwanja wa elimu na maarifa

Soma Zaidi...
nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubaliย Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

Soma Zaidi...
HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุญูŽู…ู’ุฒูŽุฉูŽ ุฃูŽู†ูŽุณู ุจู’ู†ู ู…ูŽุงู„ููƒู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฎูŽุงุฏูู…ู ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุนูŽู†ู’ ุงู„ู†ูŽู‘ุจููŠูู‘ ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ?...

Soma Zaidi...
Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe

Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...