Tanzu (makundi) za hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Tanzu (makundi) za Hadith.
- Tanzu za Hadith kutokana na Usahihi.
- Kutokana na usahihi, hadith zimegawanyika makundi manne;
- Hadith Sahihi.
- Ni Hadith zenye wasimulizi wote wenye sifa zilizokamilika na kuwa na
matini sahihi.
- Hadith Hasan.
- Ni Hadith zenye matini sahihi lakini baadhi ya wasimulizi wake
wamekuwa dhaifu.
- Hadith Dhaifu.
- Ni Hadith yenye matini sahihi lakini miongoni mwa wasimulizi wake
wanakasoro kubwa zilizojitokeza.
- Hadith za namna hii haziaminiki na si za kutegemea.
- Hadith Maudhu’u.
- Ni Hadith ya uwongo ambayo Mtume (s.a.w) amezuliwa nayo.
- Hizi ni Hadith zinazopingana na Qur’an na Hadith zilizo sahihi pia.
- Tanzu kutokana na Umashuhuri (Umaarufu).
- Kutokana na Umashuhuri, Hadith zimegawanyika makundi mawili;
- Hadith Mutawatir.
- Ni Hadith yenye kusimuliwa na watu wengi kwa nyakati tofauti, wanne
au zaidi wote wakiwa na sifa kamili.
- Hadith hizi ni ndio zenye kukubalika na watu wote.
- Hadith Ahad.
- Ni Hadith ambayo ina wasimulizi wenye sifa zilizokamilika, lakini
hawana mfungamano au msururu wa wasimulizi una mapengo kati kati.
- Ni Hadith zisizokubalika kwa watu wengi, ni za mashaka mashaka na si za kutegemea.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 ai web app 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina