picha

Tanzu (makundi) za hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

-  Kutokana na usahihi, hadith zimegawanyika makundi manne;

  1. Hadith Sahihi.

                -  Ni Hadith zenye wasimulizi wote wenye sifa zilizokamilika na kuwa na  

                    matini sahihi.

 

  1. Hadith Hasan.

   - Ni Hadith zenye matini sahihi lakini baadhi ya wasimulizi wake 

      wamekuwa dhaifu.   

 

  1. Hadith Dhaifu.

      -  Ni Hadith yenye matini sahihi lakini miongoni mwa wasimulizi wake 

          wanakasoro kubwa zilizojitokeza.

      -  Hadith za namna hii haziaminiki na si za kutegemea.   

 

  1. Hadith Maudhu’u.

      -  Ni Hadith ya uwongo ambayo Mtume (s.a.w) amezuliwa nayo.

      -  Hizi ni Hadith zinazopingana na Qur’an na Hadith zilizo sahihi pia.

 

-  Kutokana na Umashuhuri, Hadith zimegawanyika makundi mawili;

  1. Hadith Mutawatir.

-  Ni Hadith yenye kusimuliwa na watu wengi kwa nyakati tofauti, wanne 

    au zaidi wote wakiwa na sifa kamili. 

-  Hadith hizi ni ndio zenye kukubalika na watu wote.

 

  1. Hadith Ahad.

-  Ni Hadith ambayo ina wasimulizi wenye sifa zilizokamilika, lakini 

    hawana mfungamano au msururu wa wasimulizi una mapengo kati kati.


                    -  Ni Hadith zisizokubalika kwa watu wengi, ni za mashaka mashaka na si                             za kutegemea.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 3629

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 ai web app     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Elimu

Uwanja wa elimu na maarifa

Soma Zaidi...