picha

Funga za kafara

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

    -    Ni funga anazolazimika muislamu kufunga ili ziwe kitubio au fidia baada ya kutenda  kosa fulani.

 

  1.   Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemuua mtu kwa bahati mbaya na akakosa mali ya kulipa fidia.

Rejea Qur’an (4:92).

  1.   Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemsusa mkewe kwa kumfananisha na mama mzazi wake.

Rejea Qur’an (58:1-4).

 

  1.   Kufunga siku tatu mfululizo kama kafara kwa muislamu aliyevunja kiapo.

Rejea Qur’an (5:89).

 

  1.    Kufunga miezi miwili mfululizo kwa mume na mke waliofanya jimai (tendo la ndoa) mchana wa mwezi wa Ramadhani.

 

  1.    Kufunga kama kitubio cha muislamu aliyewinda na hali yuko katika Ihram.

-    Idadi ya siku inategemea na thamani ya kile alichokiua (alichokiwinda).

-    Kama hana uwezo wa kufunga, atatoa fidia ya mbuzi au kondoo.

      Rejea Qur’an (5:95).

 

  1.    Kufunga siku 10, tatu akiwa Makkah na 7 baada ya kurejea nyumbani kwa muislamu aliyevunja miiko ya Ihram.

-    Kama hana uwezo wa kufunga, atafidia kwa kuchinja mbuzi au kondoo.

Rejea Qur’an (2:196).

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 3772

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 ai web app     👉5 web hosting     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato

Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya haja

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza

عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُ?...

Soma Zaidi...