Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Maiti awekwe juu ya kitanda chenye tobo katikati ili kupitisha uchafu unaotoka tumboni.
  2. Pawepo na shimo (ufuo) usawa wa tobo la kitanda, kama hakuna uwekano chombo kiwepo cha kukingia uchafu unaotoka kwa maiti.

        -  Pia maiti inaweza kuoshewa bafuni au kwenye karo liliotengenezwa

                     kwa kazi hiyo.

 

  1. Maiti afunikwe na nguo moja kubwa yenye kupenyeza maji wakati wa kuosha.

 

  1. Maiti akalishwe juu ya kitanda usawa wa tobo na shimo (ufuo) na ainamishwe nyuma kidogo, kama ni mzito ni vizuri msaidizi wa muoshaji amuegemeze kwenye magoti yake.

 

  1. Muoshaji apitishe mkono wa kushoto kwenye tumbo la maiti na kuliminyaminya taratibu ili kutoa uchafu ndani.

 

  1. Amlaze chali na kuminyaminya tumbo lake kama ilivyo mara ya kwanza.

 

  1. Aikalishe tena na apitishe mkono wa kushoto chini akiwa amevaa kitambaa au gloves na kusafisha tupu mbili kwa maji safi. 

-   Kama hapaja takata, basi na avae gloves safi na ile chafu aitupe kwenye  

                       ufuo na asafishe tena kama mara ya kwanza mpaka patakate.

 

  1. Baada ya hapo, muoshaji afunge kitambaa safi kwenye kidole chake shahada na akichovye kwenye maji na kumswakisha maiti meno yote na kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Muoshaji azungushe kitambaa kingine safi kidole chake kidogo mkono wa kushoto na kumsafisha nacho maiti tundu za pua kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Asafishe kucha za maiti kwa kijiti safi na laini iwapo ni ndefu na chafu.

 

  1. Kisha amkalishe maiti na amtawadhishe kwa kufuata taratibu za kawaida za kutia udhu (kutawadha).

 

  1. Maiti akiwa amekalishwa, ataanza kumuoshwa kichwa akiwa ameinamishwa mbele kidogo.

- Kama nywele au ndevu ni nyingi zichanwe na kuoshwa kwa sabuni na

   maji mpaka zitakate.

            - Mwanamke mwenye nywele nyingi zisukwe mikia, na zilizong’oka 

              ziambatanishwe na sanda.

 

  1. Baada ya kuoshwa kichwa, maiti italazwa kwa ubavu wa kushoto na kuanza kuoshwa ubavu wa kulia, mbele na nyuma kwa pamoja kwa sabuni na maji safi mpaka itakate.

 

  1. Kisha itaoshwa ubavu wa kushoto kama ilivyooshwa wa kulia.

 

  1. Baada ya makosho (maosho) haya mawili, la maji na sabuni na la kuondoa sabuni, kosho la tatu la maji liwekewe karafuu na marashi ili kulegeza viungo (maungo) vya maiti.

 

  1. Baada ya makosho matatu haya, muoshaji anyooshe viungo vya maiti na kumlaza kama alikuwa mara tu baada ya kufa.

 

  1. Kisha achukue nguo kavu na kumfuta maiti, na baada ya hapo maiti awekwe juu ya mkeka mkavu na kufunikwa kwa nguo kavu tayari kuvalishwa sanda (kukafiniwa). 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1573

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Matendo ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Njia za kudhibiti riba

Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana.

Soma Zaidi...
Haki za viumbe na mazingira

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Je manii ni twahara au najisi?

Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis

Soma Zaidi...
Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.

Soma Zaidi...