Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua


image


Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


  • Namna ya Kuosha Maiti hatua kwa hatua.
  1. Maiti awekwe juu ya kitanda chenye tobo katikati ili kupitisha uchafu unaotoka tumboni.
  2. Pawepo na shimo (ufuo) usawa wa tobo la kitanda, kama hakuna uwekano chombo kiwepo cha kukingia uchafu unaotoka kwa maiti.

        -  Pia maiti inaweza kuoshewa bafuni au kwenye karo liliotengenezwa

                     kwa kazi hiyo.

 

  1. Maiti afunikwe na nguo moja kubwa yenye kupenyeza maji wakati wa kuosha.

 

  1. Maiti akalishwe juu ya kitanda usawa wa tobo na shimo (ufuo) na ainamishwe nyuma kidogo, kama ni mzito ni vizuri msaidizi wa muoshaji amuegemeze kwenye magoti yake.

 

  1. Muoshaji apitishe mkono wa kushoto kwenye tumbo la maiti na kuliminyaminya taratibu ili kutoa uchafu ndani.

 

  1. Amlaze chali na kuminyaminya tumbo lake kama ilivyo mara ya kwanza.

 

  1. Aikalishe tena na apitishe mkono wa kushoto chini akiwa amevaa kitambaa au gloves na kusafisha tupu mbili kwa maji safi. 

-   Kama hapaja takata, basi na avae gloves safi na ile chafu aitupe kwenye  

                       ufuo na asafishe tena kama mara ya kwanza mpaka patakate.

 

  1. Baada ya hapo, muoshaji afunge kitambaa safi kwenye kidole chake shahada na akichovye kwenye maji na kumswakisha maiti meno yote na kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Muoshaji azungushe kitambaa kingine safi kidole chake kidogo mkono wa kushoto na kumsafisha nacho maiti tundu za pua kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Asafishe kucha za maiti kwa kijiti safi na laini iwapo ni ndefu na chafu.

 

  1. Kisha amkalishe maiti na amtawadhishe kwa kufuata taratibu za kawaida za kutia udhu (kutawadha).

 

  1. Maiti akiwa amekalishwa, ataanza kumuoshwa kichwa akiwa ameinamishwa mbele kidogo.

- Kama nywele au ndevu ni nyingi zichanwe na kuoshwa kwa sabuni na

   maji mpaka zitakate.

            - Mwanamke mwenye nywele nyingi zisukwe mikia, na zilizong’oka 

              ziambatanishwe na sanda.

 

  1. Baada ya kuoshwa kichwa, maiti italazwa kwa ubavu wa kushoto na kuanza kuoshwa ubavu wa kulia, mbele na nyuma kwa pamoja kwa sabuni na maji safi mpaka itakate.

 

  1. Kisha itaoshwa ubavu wa kushoto kama ilivyooshwa wa kulia.

 

  1. Baada ya makosho (maosho) haya mawili, la maji na sabuni na la kuondoa sabuni, kosho la tatu la maji liwekewe karafuu na marashi ili kulegeza viungo (maungo) vya maiti.

 

  1. Baada ya makosho matatu haya, muoshaji anyooshe viungo vya maiti na kumlaza kama alikuwa mara tu baada ya kufa.

 

  1. Kisha achukue nguo kavu na kumfuta maiti, na baada ya hapo maiti awekwe juu ya mkeka mkavu na kufunikwa kwa nguo kavu tayari kuvalishwa sanda (kukafiniwa). 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Wanaowajibika kuhijji
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mgawanyo wa Elimu Usiokubalika katika uislamu.
Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu. Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya zakat na sadaqat
Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya shahada
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Namna lengo la zakat linavyofikiwa
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Haki za nafsi
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...