Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu

Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu

Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha

Download Post hii hapa

Khutuba ya Ndoa

Kabla ya kuozesha (kufungisha ndoa), ni Sunnah kwanza kuleta khutuba ya ndoa (mawaidha ya ndoa) kwa ufupi iii kuwakumbusha wanaooana na Waislamu wengine wachunge ahadi waliyoichukua mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa watakaa kwa wema katika maisha ya ndoa na ikibidi kuachana, wataachana kwa wema vile vile.

 

Ni vyema katika mawaidha haya kuwafahamisha hawa wenye kuoana na kuwakumbusha Waislamu wote waliohudhuria kuwa maisha ya ndoa yatakuwa ya furaha na upendo endapo kila mmoja, mume na mke, atajua wajibu wake kwa mwenziwe na akawajibika kwake ipasavyo. Ndoa iliyofanikishwa kulingana na ahadi ya ndoa ni msingi wa furaha, ushirikiano, utulivu na amani katika familia na jamii kwa ujumla. Ndoa pia imekusudiwa iwaokoe wenye kuoana na adui Shetani na iwasalimishe kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa ujumla, katika khutuba hii, ni vyema umuhimu wa ndoa uelezwe kwa muhtasari.

 


Msisitizo wa Khutuba unaonekana katika hadithi zifuatazo:

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema; Ndoa yoyote ambayo ndani yake hamna Tashahhud (Maamkizi ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni kama kata isiyo na mkono. (Tirmidh).

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Jambo lolote muhimu lililofanyika bila ya kumtukuza (Kumhimidi) Mwenyezi Mungu (s.w) kwa utukufu wake, limekosa baraka. (Ibn Majah).

 


Kutckana na hadithi ilisimuliwa naAbdullah bin Mas'ud (r.a), Mtume (s.a.w) amelündisha tashahud mbili, ya kwanza ni ile ya swala (Tahiyyatu) na ya li ni ile inayopalikana katika khutuba ya kukidhiwa haja, kama vile khutuba ya ndoa, ambayo inaanza na kuendelea kama iluatavyo:

 

Sfa zote anastahiki Mwenyezi Mungu (s.w). tunamtukuza kwa Utukufu wake, Tunataka msaada wake, na msamaha Wake, na tunajikinga kwake na shari ya nafsi zenu na shari ya vitendo vyetu viovu. Ambaye Mwenyezi Mungu amemuongoa, hakuna awezaye kumpoteza, na ambaye amempoteza hatakuwa na wa kumwongoa. Na ninashuhudia kuwa hapana mola ila Mwenyezi Mungu (s.w), na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtumwa wake na Mjumbe Wake.

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha wala msfe ispokuwa mmekwisha kuwa Waislamu kamili. (3:102).

 

Enyi Watu! Mcheni Mola wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi (asili) moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile. Na akaeneza wanaume wengi na wanawake kutoka wawili hao. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana.Na (muwatazame) jamaa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mlinzi juu yenu. (4:1).

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya Haki Atakutengenezeeni vizuri vitendo vyenu na Atakusameheni madhambi yenu; Na anayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake bila shaka amefuzu kufuzu kukubwa. (33:70-71).

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2581

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
Kuwapa wanaostahiki
Kuwapa wanaostahiki

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai
Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai

Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa.

Soma Zaidi...
Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu
Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu

Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.

Soma Zaidi...