Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu

Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha

Khutuba ya Ndoa

Kabla ya kuozesha (kufungisha ndoa), ni Sunnah kwanza kuleta khutuba ya ndoa (mawaidha ya ndoa) kwa ufupi iii kuwakumbusha wanaooana na Waislamu wengine wachunge ahadi waliyoichukua mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa watakaa kwa wema katika maisha ya ndoa na ikibidi kuachana, wataachana kwa wema vile vile.

 

Ni vyema katika mawaidha haya kuwafahamisha hawa wenye kuoana na kuwakumbusha Waislamu wote waliohudhuria kuwa maisha ya ndoa yatakuwa ya furaha na upendo endapo kila mmoja, mume na mke, atajua wajibu wake kwa mwenziwe na akawajibika kwake ipasavyo. Ndoa iliyofanikishwa kulingana na ahadi ya ndoa ni msingi wa furaha, ushirikiano, utulivu na amani katika familia na jamii kwa ujumla. Ndoa pia imekusudiwa iwaokoe wenye kuoana na adui Shetani na iwasalimishe kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa ujumla, katika khutuba hii, ni vyema umuhimu wa ndoa uelezwe kwa muhtasari.

 


Msisitizo wa Khutuba unaonekana katika hadithi zifuatazo:

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema; Ndoa yoyote ambayo ndani yake hamna Tashahhud (Maamkizi ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni kama kata isiyo na mkono. (Tirmidh).

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Jambo lolote muhimu lililofanyika bila ya kumtukuza (Kumhimidi) Mwenyezi Mungu (s.w) kwa utukufu wake, limekosa baraka. (Ibn Majah).

 


Kutckana na hadithi ilisimuliwa naAbdullah bin Mas'ud (r.a), Mtume (s.a.w) amelündisha tashahud mbili, ya kwanza ni ile ya swala (Tahiyyatu) na ya li ni ile inayopalikana katika khutuba ya kukidhiwa haja, kama vile khutuba ya ndoa, ambayo inaanza na kuendelea kama iluatavyo:

 

Sfa zote anastahiki Mwenyezi Mungu (s.w). tunamtukuza kwa Utukufu wake, Tunataka msaada wake, na msamaha Wake, na tunajikinga kwake na shari ya nafsi zenu na shari ya vitendo vyetu viovu. Ambaye Mwenyezi Mungu amemuongoa, hakuna awezaye kumpoteza, na ambaye amempoteza hatakuwa na wa kumwongoa. Na ninashuhudia kuwa hapana mola ila Mwenyezi Mungu (s.w), na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtumwa wake na Mjumbe Wake.

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha wala msfe ispokuwa mmekwisha kuwa Waislamu kamili. (3:102).

 

Enyi Watu! Mcheni Mola wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi (asili) moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile. Na akaeneza wanaume wengi na wanawake kutoka wawili hao. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana.Na (muwatazame) jamaa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mlinzi juu yenu. (4:1).

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya Haki Atakutengenezeeni vizuri vitendo vyenu na Atakusameheni madhambi yenu; Na anayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake bila shaka amefuzu kufuzu kukubwa. (33:70-71).

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3233

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Nini maana ya twahara katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Mifumo ya benki ya kiislamu.

Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
TOFAUTI KATI YA MAKATOZO NA MAAMRISHO KATIKA SUNNAH

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ صَخْرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُولُ: "م...

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...