image

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?



Tumejifunza kuwa jamii yenye kudumisha nguzo ya Zakat na kutilia mkazo suala la kutoa mali na huduma kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ni jamii yenye kuendelea kiuchumi na yenye kuishi kwa furaha na amanai ya kweli ya kibinafsi na kijamii. Jamii ya Mtume (s.a.w) na ile ya Makhalifa waongofu ni mfano wa wazi ulio mbele yetu. Jamii yetu hivi leo, pamoja na mahimizo ya utoaji wa Zakat na Sadaqat katika majukwaa mbali mbali bado hatuyapati matunda ya Zakat katika jamii. Miongoni mwa sababu zinazowafanya Waislamu wasipate matunda yanayotarajiwa kutokana na utoaji wa Zakat na Sadaqat ni:



(i)Wengi miongoni mwa Waislamu Hawatekelezi Nguzo ya Zakat



Wengi miongoni mwa Waislamu wenye uwezo wa kutoa zakat hawaitekelezi nguzo ya zakat na hawajihimizi kutoa misaada midogo na mikubwa kwa wale wanaohitajia.
Kwa sababu ya kutotoa Zakat na Sadaqat kwa wale wenye uwezo miongoni mwa Waislamu, kumeipelekea jamii ya Waislamu kuwa duni na dhalili mbele aya Makafiri na Washirikina.



(ii)Wengi Watoa Zakat na Sadaqat Hawatekelezi Masharti ya Utoaji



Miongoni mwa matajiri wachache wanaojitahidi kutekeleza nguzo ya Zakat na utoaji mali kwa ajili ya kuwasaidia wanaohitajia, hawazingatii masharti ya utoaji.Baadhi ya matajiri hutoa mali zao kwa ria na hufuatilia kwa masimbulizi. Utoaji wa namna hii umefutiwa baraka na hauwezi kumnufaisha mwenye kutoa wala jamii. Ubaya wa kutoa mali au msaada wowote kwa ria na kwa masimbulizi umedhihirishwa wazi katika aya ifu atayo:



Enyi mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia; kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonesha watu, wala hamwamini Mwenyezi Mungu wala siku ya mwisho. Basi hali yake ni kama hali ya jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha ikalifikia (jabali hili) mvua kubwa (likasukuma udongo wote huo) na ikaliacha tupu. Basi haw atakuw a na uw ezo (wa kupata) chochote katika walivyovichuma; na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri”. (2:264)



Kuna baadhi ya miongoni mwa Waislamu matajiri wanaotoa Zakat bila ya kuzingatia wale wanaostahiki (Rejea Qur-an, 9:60). Badala yake huenda na kapu la fedha msikitini na kumgawia kila mtu atakayekuwa tayari kupokea. Ugawanyaji huu wa Zakat hupelekea kupewa wasiostahiki na kuwakosesha wanaostahiki na kuwabakisha katika dhiki yao. Utoaji wa namna hii huibakisha jamii ya Waislamu katika dhiki na katika uadui na uhasama. Kuna baadhi ya Waislamu pamoja na kutoa Zakat na Sadaqat, hawazingatii mipaka ya halali na haramu katika uchumi wao. Wengine huchuma kwa njia za haramu ambazo hazinufaishi jamii bali huiingiza jamii katika matatizo ya rushwa, riba, kamari, wizi, ujambazi na udhalimu wa kila namna.



(iii) Zakat haikusanywi na Kugawanywa Kijamii
Tumejifunza kuwa utoaji na ugawaji wa Zakat, ili unufaishe jamii hauna budi kusimamiwa na jamii. Lazima jamii ya Kiislamu iwe na watu maalum wanaopita kwa kila Muislamu mwenye uwezo wa kutoa zakat, na kuipokea Zakat yake kisha kuikabidhi kwa Mtunzaji wa Baitil-Mali (Mhazini), kisha kuigawa kwa wanaostahiki.
Sehemu kubwa ya jamii ya Waislamu hivi leo, haifuati utaratibu huu wa ukusanyaji na ugawaji wa Zakat na sadaqat bali kila mwenye kutoa Zakat huigawanya mwenyewe kwa wale wanaostahiki walio machoni mwake. Kuacha Zakat mikononi mwa watoaji binafsi, kuna hasara kubwa zifuatazo:



Kwanza; hapitiwi na mhimizo wa makusudi juu ya utoaji wa Zaka, kiasi kwamba wenye kustahiki kutoa Zakat hujisahau na hatimaye kuacha kutoa Zakat kabisa.



Pili; kwa kutokuwa na utaratibu wa ugawaji, sehemu kubwa ya Zakat hupewa wasiostahiki na wale wanaostahiki hubaki na dhiki yao.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 907


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo? Soma Zaidi...

Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...

Njia haramu za uchumi
Soma Zaidi...

Mirathi Katika Uislamu, nani anarithi na ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kirisisha
Soma Zaidi...

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

Usawa katika uchumi wa kiislamu
5. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani
(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu. Soma Zaidi...

Hukumu ya Mtu asiyefunga kwa makusudi mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha mkojo wa Mtoto mdogo Najisi Hafifu
Soma Zaidi...

Ni nini maana ya swala
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala. Soma Zaidi...

Hukumu na taratibu za ndoa katika uislamu
Soma Zaidi...

Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu
Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu. Soma Zaidi...