Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.
3. Swala ya Witri
Witri maana yake ni namba isiyogawanyika kwa mbili kama vile 1, 3, 5, 7, 9, 11 n.k. Sunnah ya witri huswaliwa katika kipindi cha usiku baada ya swala ya Al-Isha na kabla ya kuingia swala ya Al-Fajiri. Lakini ni bora kuichelewesha Witri na kuiswali katika theluthi ya mwisho ya usiku, baada ya swala ya kisimamo (tahajjud).
Mtume (s.a.w) alikuwa akiswali Witri pamoja na swala ya Tahajjud (Swala ya Usiku) na wakati mwingine alikuwa akiswali Witri mara tu baada ya Al-Ishaai. Ni vema kuswali witri baada ya al-Isha kama hakuna uhakika wa kuamka Usiku. Mtume (s.a.w) ameikokoteza sana swala ya Witri kama tunavyojifunza katika hadithi ifuatayo:
Buraydah (r.a) amesimulia, Nimemsikia Mtume (s.a.w) akisema; Witri ni haq (wajibu). Asiyeswali si miongoni mwetu. Witri ni wajibu”. (Abu Da udi)
Witri ina swaliwa kwa rakaa tatu. Huswaliwa kwa rakaa mbili na kutoa Salaam, kisha hukamilishwa na rakaa moja.
Namna ya Kuswali Swala ya Witri
1. Katika rakaa ya kwanza utasoma Sura ya Al-A’alaa (Sabbihisma) baada ya Suratul-Faatiha.
Katika rakaa ya pill utasoma Suratul-Kaafiruuna baada ya suratul-faatiha..
Katika rakaa moja ya mwisho. baada ya kusoma Suratul-Faatiha, utasoma Suratul- lkhlas, AI-Falaq na An-naas. Kuleta Qunut (dua) katika rakaa ya mwisho katika ltidali.
Dua tunayoileta katika Qunut ni hii ifuatayo:
Allahumma ihdidaa fii man hadaita "Ewe Mola n[ongoze kama wale uliouxiongoza"
Wa `aafinaa fiiman `aafaita "Na unininusuru kama hao uliowarursuru"
Watawallanii fiiman tawaffaita "Na unitawalishe pamoja na wale ulio watawalisha
wabaarik lii fii maa a'atwaitanii "Na unitilie pataka katika vile ulivyonipa
Waqinii sharra maa gadhwaita "Unikinge na shari ulizonikadiria"
Tabaarakta rabbanaa wata’aalaita "Ni nyingi kabisa juu yetu baraka zako na umetukuka kweli kweli"
Ni muafaka kuleta dua nyinginezo vile vile kulingana na haja ya mwenye kuswali.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.
Soma Zaidi...Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.
Soma Zaidi...Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...