NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)

Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)

 NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W).

Njia za Kumtambua Mwenyezi Mungu (s.w).

Nafasi ya Fitrah (maumbile).

- Kila Mwanaadamu amepandikizwa hisia za kimaumbile zinazomtambua Mungu kupitia ujuzi wa kutambua mema na maovu.

 

- Mwanaadamu akipatwa na raha au misukosuko na huzuni hukiri uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Quran (17:67), (30:30) na (91:7-8).

 

Vipaji vya Binaadamu.

- Vipaji vya akili na milango ya fahamu na fani zingine za elimu ni nyenzo pekee zikitumiwa vilivyo humuwezesha mtu kumjua Mola wake.

Rejea Quran (3:190-191), (35:28).

 

Nafsi ya mwanaadamu.

- Mfumo mzima wa mwili wa mwanaadamu na utendaji wake wa kazi wa ajabu wa viunge mbali mbali vya mwili kama kuyeyusha chakula tumboni, msukumo wa damu mwilini, n.k. ni ishara tosha juu ya uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Quran (51:20-21) 

 

Mazingira.

- Utegemezi na uhusiano wa kimahitaji ya kutumia rasilimali ya kuishi kati ya mimea, wanyama na binaadamu (ecological balance).

 

- Maumbile mengine kama mbingu, ardhi na yote yanayoonekana na yasiyooneka katika mazingira yanayotunguka.

Rejea Quran (3:190).

 

Wahyi (Ufunuo).

- Wahyi ndio nyenzo kuu ya kumwezesha mwanaadamu kumtambua Mwenyezi Mungu (s.w) kwa usahihi unaotakikana.

 

- Elimu, vipaji na ujuzi au sayansi pekee haviwezi kumwezesha mwanaadamu kumtambua Mungu kwa baadhi ya maeneo, mfano nguzo za imani, n.k.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 3151

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...

Soma Zaidi...
Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza

Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.

Soma Zaidi...