Kujiepusha na ubadhirifu (israfu) na ubakhili
Kujiepusha na ubadhirifu (israfu) na ubakhili
(b)Kujiepusha na Ubadhirifu (israfu)
Ubadhirifu ni utumiaji wa mali au kitu chochote kile chenye thamani kama vile muda, zaidi kuliko mahitajio. Pia kutoa mali au huduma na kuwapa watu wasiostahiki ni katika kufanya ubadhirifu. Vile vile kutumia mali au muda katika yale yaliyoharamishwa, ni katika israfu. Ubadhirifu wa aina zote umekatazwa katika Uislamu na afanyae ubadhirifu ni rafiki yake shetani.
(c)Kujiepusha na ubakhili
Ubakhili ni kinyume cha ubadhirifu.Ubakhili ni kitendo cha kuwanyima msaada wale wanaostahiki wakati uwezo wa kuwasaidia upo. Pia ni katika kufanya ubakhili kwa mtu kujinyima mahitaji muhimu ya maisha kama vile lishe bora, mavazi na makazi bora na huku anauwezo. Katika kutumia na kutoa misaada, Waumini wanatakiwa wawe kati na kati:
"Wala usifanye mkono wako kama uliofungwa shingoni mwako, wala usiukunjue ovyo ovyo, utakuwa ni mwenye kulaumiwa na kufilisika ”(17:29)
"Na (katika waja wa Rahman ni) wale ambao wanapotumia hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubakhili, bali wanakuwa kati kati baina ya hayo." (25:67)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an
(v)Kuwaombea dua wazazi.
Soma Zaidi...Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu
Soma Zaidi...Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao
Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.
Soma Zaidi...Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.
Soma Zaidi...