Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi nguo za kuvaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake, hizi ni nguo ambazo wahudumu wa afya wanapaswa kuzivaa wakati wa upasuaji kwa ajili ya kuwakinga na Maambukizi kati ya wahudumu wa afya na wagonjwa pia

Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji.

1.Kofia

Hii ni mojawapo ya nguo inayokaliwa kwenye chumba cha upasuaji, kofia yenyewe huwa mara nyingi imeshinwa kwa nguo, kazi yake ni kuzuia nywele kutoka kwenye kichwa cha mhudumu kuingia kwa mgonjwa wakati wa upasuaji, kwa hiyo kila mhudumu anapaswa kuivaa hii kofia kwa kufanya hivyo Maambukizi yataweza kupungua na kuepuka kuwepo kwa magonjwa yadiyotegemewa.

 

2.Nguo nyingine ni Maski au kwa lugha nyingine tunaweza kuita Barakoa.

Mask au barakoa uvaliwa na kufunika sehemu za mdomo, pua kwa hiyo kazi yake ni kuzuia mate kudondoka wakati wa upasuaji au hewa kutoka mdomoni inaweza kuwa na wadudu kwa hiyo ikasababisha wadudu kuingia kwenye sehemu ambayo imefunguliwa na kuleta Maambukizi au pengine mhudumu anaweza kupiga chafya na kusababisha wadudu kusambaa, lakini kama kuna Maski hakuna kitu chochote kinachoweza kutokea mdomoni au puani.

 

3.Nguo nyingine ni apron.

Hivi ni nguo ambayo uvaliwa juu ya gauni, nguo hii kazi yake ni kuzuia damu au majimaji kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, kwa sababu wakati mwingine mgonjwa anaweza kuwa na Maambukizi na yakifika kwa mhudumu moja kwa moja yanaweza kusababisha Maambukizi kwa mgonjwa kwa hiyo ni lazima mhudumu kuvaa hii apron ili kuepukana na Maambukizi.

 

4.Nguo nyingine ni gauni.

Hii nayo ni nguo inapaswa kuvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu au kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa, kwa hiyo kila mhudumu ni lazima kuvaa hii nguo hili kuepukana na Maambukizi ya magonjwa mbalimbali yanayoweza kusambaa kwa damu au kwa maji maji kama vile Ukimwi, homa ya ini na magonjwa mengine mengi.

 

5.Nguo nyingine ni boot au viatu vilivyofunikwa.

Pia nazo zinapaswa kuvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu uzuia Maambukizi kwa mfano kama kuna sindano imedondoka chini kwa bahati mbaya isiweze kuingia moja kwa moja kwenye mwili bali Uchoma juu ya viatu kwa sababu pengine mgonjwa anaweza kuwa na magonjwa ya kuambukiza kama sindano ikichoma juu ya boot ni vizuri kuliko kuchoma moja kwa moja kwenye ngozi.

 

6.Nguo nyingine ni gloves.

Pia nazo uvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu uzuia maambukizi kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa na kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, hizi gloves kama zikichafua inabidi zibadilishwe ili zivaliwe nyingine kwa kuepuka Maambukizi kwa hiyo nazo zinapaswa kuvaliwa kwa mda wake na kwa sheria zake.

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 1766

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

kitabu cha kanuni 100 za afya

Zijue kanuni 100 za afya ambazo watu wengi hawazijui. Laiti wangelizijua kwa hakika wangefaidika sana.

Soma Zaidi...
DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI

Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.

Soma Zaidi...
CHUKUWA TAHADHARI HIZI KWENYE MAZINGIRA ILI KULINDA AFYA YAKO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
TABIA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji

Post hii inahusu zaidi juu ya vyumba vidogo vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji, ingawa chumba cha upasuaji ni kimoja ila kuna vyumba vingine vidogo ambavyo vinatumika kwa kazi mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
hathari zitokanazo na uvutaji wa sigara ,pombe na madawa ya kulevya na mbinu za kujikinga nayo

Posti hii inahusu zaidi utumiaji wa pombe na sigara pamoja na madawa katika jamii.

Soma Zaidi...
DONDOO 100 ZA AFYA

Pata dondoo 100 za Afya

Soma Zaidi...
MARADHI YASABABISHWAYO NA HALI ZA MAISHA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 81-100

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dondoo za afya

Soma Zaidi...