Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo ya kiafya yanayozungumzwa na umoja wa mataifa
UMOJA WA MATAIFA (UN) UNAZUNGUMZIAJE AFA?
Umoja wa mataifa una kitengo ambacho kinajihusisha na masuala yote ya afya kitengo hiko nikajulikana kama HYPERLINK "https://en.wikipedia.org/wiki/World_Health_Organization" o "WHO" World_Health_Organization. Kulingana na tafiti za shirika hili la umoja wa mataifa, nimeamua kukuletea HYPERLINK "https://bongoclass.com/dondoo-100/dondoo-100-za-afya.html" o "dondoo 100 za afya" dondoo kadhaa za afya. Dondoo hizi zinahusu takwimu mbalimbali za afya duniani kote. Nitaanza kunukuu moja kati ya taarifa hizo hapo chini..
'
Takribani nusu ya wakazi wa dunia bado hawapati huduma za msingi za afya.
'
'
Takribani watu milioni 100 bado wanasukumwa kwenye ufukara kwa kuwa hawana uwezo wa kulipia huduma zao za afya.
'
Zaidi ya watu milioni 800 , sawa na asilimia 12 ya wakazi wote wa dunia, wanatumia asilimia 10 ya kipato cha kaya kugharimia huduma za afya.
'
'
Mataifa yote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa wamekubaliana kufikia lengo la huduma ya afya kwa wote ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni sehemu ya malengo ya maendeleo endelevu, HYPERLINK "https://www.undp.org/content/undp/en/home/sustainable-development-goals.html" o "sustainable-development-goals" SDGs.
'
Huu ni ukweli usio pingika kwamba bado vijijini kuna watu wengi sana ambao wanaishi huko hali ya kuwa huduma za afya haipo vizuri ukilinganisha maeneo ya mijini. Mfano mzuri ni ukosekanaji wa baadhi ya vifaa vya kutolea huduma za afya na wakati mwingine hali ya usafiri kuwa mbovu huchangia matatizo ya afya kuendelea kutokea. Elimu ya afya pia maeneo ya vijijini haipatikani ipasavyo, na ndio maana hata hali ya unyanyasaji kwa wenye HIV imekuwa kubwa vijijini kuliko mijini.
Sambamba na kuwa utoaji wa huduma bora za afya maeneo mengi duniani haupo vizuri, na hii ni kutokana na kipato cha wananchi wenyewe. Atahitajika kununua dawa ama kulipia vipimo. Serikali mbalimbali zimeweka utaratibu wa kulipia bima ili kuboresha huduma za afya, hii ni nzuri lakini bado wananchi wengi hawajaweza kuchangia huduma hio. Huenda ni kulingana na kipato chao ni kidogo ama kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kulipia HYPERLINK "http://www.nhif.or.tz/pages/health-insurance-for-private-individual" o "bima ya afya" bima ya afya .
HYPERLINK "http://afya.bongoclass.com/elimu.htm" o "elimu ya afya" Elimu ya afya inahitajika zaidi ili kuweza kuhakikisha maeneo mengi yanapata huduma hizi za afya. Kwa nini elimu ya afya? hii ni kwa sababu endapo wananchi wataelimishwa wataweza kuboresha huduma za afya kwa nguvu zao na raslimali zao. Serikali nazo pia kwa upande mwingine zihakikishe kuwa uboreshwaji wa afya unafikia mpaka maeneo ya vijijini, na wananchi wanashiriki kwa umakini maswala yote ya afya.
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Author Tarehe 2021/11/10/Wednesday - 08:46:14 pm Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 567
Ujuwevmv ugonjwa Nimonia na dalili zake
Nimonia ni Hali ya kuvimba pafu inayoathiri hasa vifuko vya hewa viitwavyo Alveoli, husababishwa na Maambukizi ya virusi Soma Zaidi...
Sababu za Uvimbe wa tishu za Matiti kwa wavulana au wanaume
posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wa tishu za matiti kwa wavulana au wanaume, unaosababishwa na kutofautiana kwa homoni za estrojeni na testosterone. Pia unaweza kuathiri matiti moja au zote mbili, wakati mwingine bila usawa. Watoto wachanga, wavulana wanaobalehe na wanaume wazee wanaweza kupata Uvimbe wa tishu za matiti kama matokeo ya mabadiliko ya kawaida katika viwango vya homoni, ingawa sababu zingine pia zipo. Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Saratani.
Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo wa kuenea katika mwili wako wote. Soma Zaidi...
Ujue ugonjwa wa tauni
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya. Soma Zaidi...
Matibabu ya macho
Somo Hili linakwenda kukuletea matibabu ya macho Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi Soma Zaidi...
Msaada kwa wenye Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwahudumia wenye Maambukizi kwenye mifupa, ni njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuwasaidia wenye Maambukizi kwenye mifupa. Soma Zaidi...
DAWA YA FANGASI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi Soma Zaidi...
Mabadiliko ya Matiti kwa Mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo. Soma Zaidi...
Zijue kazi za ini
Post hii inahusu zaidi kazi za ini, ni kiungo muhimu kwenye mwili ambacho Kina umuhimu sana, bila ini maisha ya mwanadamu yanaweza kuishia pabaya Soma Zaidi...
Vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo Soma Zaidi...
Sifa za siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba Soma Zaidi...