Umuhimu wa kuvaa nguo za upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa nguo za upasuaji, tunajua wazi kuwa, wakati wa upasuaji tunapaswa kusafisha chumba na mazingira yake lengo ni kuhakikisha kuwa tunazuia wadudu wasisambae au kuingia kwenye mwili wa binadamu.

Umuhimu wa nguo za upasuaji.

1.Nguo za upasuaji zinaweka umbali kati ya mgonjwa na mhudumu ili kuepuka kusambaa kwa Magonjwa kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa na kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu kwa kufanya hivyo utaratibu na nidhamu ya upasuaji uende vizuri likiwa na lengo kuu ambalo ni kuzuia kusambaa kwa Magonjwa wakati wa upasuaji, kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kushika sheria za kuvaa nguo hizi. Ambao hawafanyi hivyo wanapaswa kuchukuliwa hatua.

 

2. Vile vile nguo za upasuaji usaidia kuzuia damu na majimaji ambayo yanaweza kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, ikitokea kwa bahati mbaya maji yakaruka kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu spidi ya kwanza yatafikia kwenye apron na hayataweza kumfikia mhudumu, kwa hiyo wahudumu wa upasuaji wanapaswa kujikinga na magonjwa kwa kuvaa nguo za upasuaji kwa kufuata mtiririko wote kwa sababu wakati wa upasuaji chochote kinaweza kutokea.

 

3.Pia nguo za upasuaji usaidia kuzuia magonjwa na chemikali nyingine kusambaa kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu kwa mfano kama mgonjwa ana Maambukizi ya ukimwi, na homa ya ini katika kufanya upasuaji ukiwa na nguo za upasuaji unaweza kuepuka na magonjwa haya, kwa hiyo wahudumu wawe makini sana katika kutumia nguo za upasuaji ili kuepukana na magonjwa na kemikali nyingine zinazotumika wakati wa upasuaji.

 

4. Kwa hiyo baada ya kujua faida za nguo za upasuaji kila kituo cha afya wanapaswa kuwa na nguo zote za kufaa na zinapaswa kusafishwa kwa wakati na kwa utaratibu maalum na pia wanaoziandaa wanapaswa kuwa waangalifu na kuwa na ujuzi katika kazi hiyo, pia na wahudumu wanaozivaa wanapaswa kuwa na moyo wa kujali wa kutumia nguo hizo kwa wakati wake na kwa usahihi kwa sababu wasipozitumia wanaweza kuhatarisha maisha yao na wagonjwa pia.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 1577

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 41-60

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
Nini maana ya Afya

Maana ya afya ni pana sana tofauti na vile ambavyo sisi tunajuwa. Afya inahusisha mambo mengi sana.

Soma Zaidi...
kitabu cha kanuni 100 za afya

Zijue kanuni 100 za afya ambazo watu wengi hawazijui. Laiti wangelizijua kwa hakika wangefaidika sana.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupiga push up kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Masomo ya Afya kwa kiswahili

Makala za afya zilizopata kusomwa zaidi kutoka bongoclass kitengo cha afya

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza chumba cha upasuaji

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji ni tofauti na vyumba vingine kwenye hospitali kwa hiyo vinahitaji uangalizi wa hali ya juu sana ili kuepuka aina yoyote ya uchafu kuwepo kwenye chumba hicho, zifuatazo ni na

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...