Umuhimu wa kuvaa nguo za upasuaji.


image


Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa nguo za upasuaji, tunajua wazi kuwa, wakati wa upasuaji tunapaswa kusafisha chumba na mazingira yake lengo ni kuhakikisha kuwa tunazuia wadudu wasisambae au kuingia kwenye mwili wa binadamu.


Umuhimu wa nguo za upasuaji.

1.Nguo za upasuaji zinaweka umbali kati ya mgonjwa na mhudumu ili kuepuka kusambaa kwa Magonjwa kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa na kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu kwa kufanya hivyo utaratibu na nidhamu ya upasuaji uende vizuri likiwa na lengo kuu ambalo ni kuzuia kusambaa kwa Magonjwa wakati wa upasuaji, kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kushika sheria za kuvaa nguo hizi. Ambao hawafanyi hivyo wanapaswa kuchukuliwa hatua.

 

2. Vile vile nguo za upasuaji usaidia kuzuia damu na majimaji ambayo yanaweza kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, ikitokea kwa bahati mbaya maji yakaruka kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu spidi ya kwanza yatafikia kwenye apron na hayataweza kumfikia mhudumu, kwa hiyo wahudumu wa upasuaji wanapaswa kujikinga na magonjwa kwa kuvaa nguo za upasuaji kwa kufuata mtiririko wote kwa sababu wakati wa upasuaji chochote kinaweza kutokea.

 

3.Pia nguo za upasuaji usaidia kuzuia magonjwa na chemikali nyingine kusambaa kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu kwa mfano kama mgonjwa ana Maambukizi ya ukimwi, na homa ya ini katika kufanya upasuaji ukiwa na nguo za upasuaji unaweza kuepuka na magonjwa haya, kwa hiyo wahudumu wawe makini sana katika kutumia nguo za upasuaji ili kuepukana na magonjwa na kemikali nyingine zinazotumika wakati wa upasuaji.

 

4. Kwa hiyo baada ya kujua faida za nguo za upasuaji kila kituo cha afya wanapaswa kuwa na nguo zote za kufaa na zinapaswa kusafishwa kwa wakati na kwa utaratibu maalum na pia wanaoziandaa wanapaswa kuwa waangalifu na kuwa na ujuzi katika kazi hiyo, pia na wahudumu wanaozivaa wanapaswa kuwa na moyo wa kujali wa kutumia nguo hizo kwa wakati wake na kwa usahihi kwa sababu wasipozitumia wanaweza kuhatarisha maisha yao na wagonjwa pia.



Sponsored Posts


  đꑉ    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       đꑉ    2 Madrasa kiganjani offline       đꑉ    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       đꑉ    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Sababu na dalili za ugonjwa wa Njia ya mkojo.
Ujue ugonjwa wa Njia ya mkojo unaoitwa urethra stricture. Ambapo kwenye hii posti inaonyesha dalili na Sababu zinazopelekea Njia ya mkojo kuwa ngumu,nyembamba,na kovu. Soma Zaidi...

image Upungufu was fati
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu was fati Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe au puto katika mshipa wa damu kwenye ubongo. Uvimbe kwenye Ubongo unaweza kuvuja au kupasuka, na kusababisha kuvuja damu kwenye ubongo. Mara nyingi, kupasuka kwa Uvimbe wa Ubongo hutokea katika nafasi kati ya ubongo na tishu nyembamba zinazofunika ubongo. Aina hii ya Kiharusi cha kuvuja damu huitwa Subarachnoid hemorrhage. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI Soma Zaidi...

image Mambo ambayo yanaweza kuongeza hatari ya Ugonjwa wa Homa ya ini yenye sumu.
Posti hii inazungumzia zaidi kuhusiana na Homa ya ini yenye sumu ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuguswa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumu inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, madawa ya kulevya au virutubisho vya lishe. Katika baadhi ya matukio, homa ya ini yenye sumu hukua ndani ya saa au siku baada ya kuathiriwa na sumu.Katika hali nyingine, inaweza kuchukua miezi ya matumizi ya kawaida kabla ya dalili na dalili za homa ya ini yenye sumu kuonekana. Lakini homa ya ini yenye sumu inaweza kuharibu ini kabisa, na kusababisha kovu lisiloweza kutenduliwa la tishu za ini (cirrhosis) na katika visa vingine ini kushindwa kufanya kazi Soma Zaidi...

image Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango
Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali. Soma Zaidi...

image Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa. Soma Zaidi...

image Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula. Soma Zaidi...

image Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya uke
Saratani ya uke ni Saratani adimu inayotokea kwenye uke wako mrija wa misuli unaounganisha uterasi na sehemu zako za siri. Saratani ya uke mara nyingi hutokea katika seli zilizo kwenye uso wa uke wako, ambao wakati mwingine huitwa njia ya uzazi. Wanawake walio na saratani ya uke katika hatua za awali wanayo nafasi nzuri ya kupata tiba. Saratani ya uke inayoenea nje ya uke ni vigumu zaidi kutibu. Soma Zaidi...

image Dalili za mtu aliyegongwa na nyoka
Post hii inahusu zaidi dalili za mtu aliyegongwa na nyoka, nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na sumu ikiingia mwilini mtu huwa na dalili mbalimbali Soma Zaidi...