Sheria za kutunza usafi wakati wa upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi sheria za kutunza usafi wakati wa upasuaji, iwapo sheria mojawapo ikienda kinyume ijulikane kuwa usafi haujaenda sawa na pengine kwa kitaalamu huitwa contamination.

Sheria za usafi wakati wa upasuaji.

1.kifaa chochote ambacho kimegusa kidonda cha mgonjwa uhesabiwa kubwa ni kichafu na kinapaswa kufanyiwa usafi kwa kuanzia kwenye ndoo yenye maji ya sabuni, baadae kwenye maji ya chlorine na baadae kwenye maji masafi na baada ya hapo upelekea na kuunguzwa ili kuua wadudu wote na baadae kutumiwa tena. Kwa hiyo hata kama chombo kimegusa kwa sehemu ndogo kinaesabiwa kuwa ni kichafu.

 

2.Sehemu yoyote safi inapaswa kukutana na sehemu nyingine ambayo ni safi na sehemu chafu inapaswa kukutana na sehemu chafu, ikiwa sehemu ya kifaa kilicho safi limekutana na sehemu nyingine ya kifaa iliyochafu hata sehemu ndogo kifaa hicho kinaesabiwa kubwa ni kichafu kwa hiyo kinapaswa kusafishwa kwa utaratibu unaofaa.

 

3.Kwa upanda wa wafanyakazi au wahudumu wa kwenye chumba cha upasuaji wanapaswa kutembea kutoka kwenye sehemu safi kwenda sehemu safi na kutoka sehemu chafu kwenda chafu, ikitokea mmoja anatembelea kwenye sehemu safi kwenda chafu anaesabika kubwa hazingatii usafi na anapaswa kubadilisha nguo na kunawa vizuri ndipo anaruhusiwa kuendelea na shughuli za upasuaji.

 

4.Kutembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine ila sehemu iliyo safi wakati wote wa upasuaji haina maana kwamba umekosea sheria za usafi wakati wa upasuaji, kwa sababu kuna vitu vinapaswa kutolewa sehemu moja kwenda nyingine, ila kama ni kutembea sehemu chafu na kurudi kwenye sehemu safi hapo kuna makosa.

 

5.Sehemu yoyote kwenye chumba cha upasuaji inapaswa kukingwa kutokana na unyevunyevu kwa maana unyevunyevu utunza uchafu mwingi sana na kusababisha magonjwa mengi na Maambukizi kwa mgonjwa kwa hiyo chumba cha upasuaji kinapaswa kusafishwa mda wote na kuhakikisha kubwa kinabaki safi hata mtu akigusa kwenye sehemu yoyote hasitoke na vumbi.

 

6.Wakati wa kufanya upasuaji vifaa vyote ambavyo ni safi na vinapaswa kutumiwa kwa mda huo vinapaswa  juwa wazi na vinaonekana kwa hiyo wahudumu wanaohusika na vifaa wanapaswa kuwa karibu ili kuweza kuweka vifaa karibu na kuepuka kutoka sehemu moja na kwenda nyingine, kwa hiyo maandalizi ni ya maana kwa mtunza vifaa.

 

7.Kifaa chochote ambacho kinatiliwa  mashaka kuhusu usafi kinaesabiwa kubwa ni kichafu kama kinapaswa kusafishwa na kutumia kama kinahitajika, kwa hiyo waandaaji wa vifaa wanapaswa kuwa makini katika kuandaa vifaa vyao ili kuepuka makosa wakati wa upasuaji na kutilia mashaka kwa baadhi ya vifaa.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 984

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi nguo za kuvaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake, hizi ni nguo ambazo wahudumu wa afya wanapaswa kuzivaa wakati wa upasuaji kwa ajili ya kuwakinga na Maambukizi kati ya wahudumu wa afya na wagonjwa pia

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Kitabu Cha matunda

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
hathari zitokanazo na uvutaji wa sigara ,pombe na madawa ya kulevya na mbinu za kujikinga nayo

Posti hii inahusu zaidi utumiaji wa pombe na sigara pamoja na madawa katika jamii.

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
DONDOO 100 ZA AFYA

Pata dondoo 100 za Afya

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya ngozi kuwa laini

Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufanya ili ngozi iweze kuwa laini bila kuwa na make up yoyote.

Soma Zaidi...