picha

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA VYAKULA

YANAYOATHIRI AFYA
Afya yamtu inaweza kuathiriwa kuwa njema au kuwa mbovu kwa kuzingatia mambo kadhaa wakadhaa. Hapa nimechagua mambo makuu matano ambayo nitakwenda kuyaangalia ambayo ni;-


A).vyakula
B)Mazingira
C)Shughuli za kila siku
D)Tabia na mazoea
E)Vizazi, familia ama kurithi.


1.VYAKULA
Vyakula ni katika sababu kubwa ambazo husaidia kwa kiwango kikubwa kuathiri afya za watu. Wataalamu wa afya leo wanaeleza na kutaja magonjwa mengi sana ambayoyo yanapatikana kwa kupitia vyakula. Pia yapo magonjwa ambayo huambukizwa kwa kupitia ulaji wa chakula. Hivyo magonjwa mengi na hatari zaidi yamekuwa na mahusiano na vyakula vyetu. Chakula kinaweza kuwa msaada kwako au kuwa ni chanzo cha matatizo ya afya yako. Mfano mzuri ni kuwa leo wataalamu wa afya anaeleza kuwa mamilioni ya watu wanakufa kwa ugonjwa wa saratani kila mwaka. Tafiti zinaonesha kuwa miongoni mwa sababu za ugonjwa huu ni vyakula. Vyakula ambavyo tunavila leo sio rafiki kwa afya zetu. Tumekuwa tukila vyakula ambavyo vimejaa kemikali nyingi na matatizo kadha wakadha.

Mfano wa pili ni ugonjwa wa kisukari, huu ugonjwa umekuwa ukienea kwa kasi sana duniani leo. Kuanzia watoto, vijana wazee na wajawazito wote wapo hatarini kuapata maradhi haya. Wataalamu wa afya wanataja kuwa vyakula ni katika sababu mjawapo ya kupata maradhi haya. Kuongezeka kwa uzito nje ya uzito wa kawaidi ni katika sababu za kutokea kwa kisukari. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa vyakula ni sababu ya kuongezeka kwa uzito mwilini na kutofanya mazoezi ijapokuwa zipo sababu zingine.

Magonjwa ya moyo kama shinikizo la damu (presha) pamoja na shambulio la moyo (heart attack) ni katika magonjwa yanayowapata watu weng duniani na kusababisha vifo vingi sana. Wataalamu wa afya wanaeleza katika sababu kubwa za kutokea kwa maradhi haya ni vyakula. Hususan vyakula vyenye mchanganyiko mkubwa wa mafuta ya viwandani.

Maradhi ya utapiamlo kama matege, baadhi ya matatizo ya macho, unyafuzi na kwashiakoo pamoja na kudumaa ni katika maradhi ambayo husababishwa na vyakula. Majeraha kutokupona haraka, kuchelewa kupona kwa vidonda na makovu, ngozi kupasuka na kutokwa na vidonda kwenye mdomo ni katika baadhi ya matatizo yanayosababishwa na vyakula Kwa ufupi ni kuwa vyakula ni katika sababu kubwa sana ya maradhia mabayo tuanayapata. Tutazungumzia kwa undani zaidi somo hili kwenye kurasa zijazo na tutaona kwa undani vipi vyakula vinaweza kusababisha yote hayo.


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 879

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Vipi mkojo unaeleza kuhusu afya ya mtu

Hapa tutajifunza namna ambavyo mkojo unaweza kueleza kuhusu hali ya kiafya ya mtu

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuhesabu siku za hatari za kupata mimba.

Kujua siku zako za hatari (siku ambazo una uwezekano mkubwa wa kupata mimba) ni njia muhimu sana kwa wanandoa wanaopanga kupata mtoto. Siku hizi hutegemea mchakato wa kupevuka kwa yai (ovulation), ambapo yai huachiliwa kutoka kwenye ovari ili kurutubishwa. Makala hii inaelezea mbinu rahisi ya kalenda unayoweza kutumia.

Soma Zaidi...
Njia za Kujikinga na Maambukizi ya UTI

Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ni tatizo la kiafya linalowapata watu wengi, hasa wanawake. UTI husababishwa na bakteria wanaoingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha maumivu, kuwashwa, na usumbufu mkubwa wakati wa kukojoa. Kwa bahati nzuri, kuna njia mbalimbali za kujikinga na maambukizi haya kupitia usafi wa mwili, ulaji wa maji ya kutosha, na mtindo bora wa maisha. Makala hii inaelezea njia muhimu za kuzuia UTI na ukweli muhimu kuhusu ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Vipi kinyesi cha haja kubwa kinaelezea afya ya mtu

Katika somo hili tutajifunza ni Kwa namna gani afya Yako inaweza kuelezewa kupitia kinyesi

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
YANAYOATHIRI AFYA TABIA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...