Taratibu za mahari katika uislamu


image


Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.


Mahari

Kabla ya mkataba wa ndoa kupitishwa jambo muhimu ni mwanamke kutaja kiasi cha mahari atakacho penda kupokea kama hidaya au zawadi anayopewa kwa amri ya Mwenyezi Mungu (s.w) kutoka kwa anayemuoa. Uhuru wa kutamka kiasi cha mahari uko kwa muolewaji na bila ya mahari hayo kutolewa taslimu au kwa ahadi ya kulipa baadaye, ndoa haiswihi. Msititizo wa mahari unapatikana katika aya zifuatazo:

 

Na wapeni wanawake mahari yao, hali ya kuwa ni hidaya (aliyowapa Mwenyezi Mungu). (Lakini hao wake zenu) wakikupeni kwa radhi ya nafsi zao kitu katika hayo (mahari) basi kuleni kwafuraha na kunufaika. (4:4).

 

"...Na (mmehalalishiwa kuwaoa) wanawake wema wa Kiislamu na wanawake wema katika wale waliopewa Kitabu kabla yen u,mtakapowapa mahari yao, kafunga nao ndoa..." (5:5)

 


Katika aya hizi tunajifunza kuwa kutoa mahari kuwapa wanawake tunaowaoa ni jambo Ia lazima aliloliamrisha Mwenyezi Mungu (s.w), lakini wenye kuolewa kwa hiari yao wenyewe, wakiamua kuyasamehe mahari hayo au kuyapunguza hata baada ya kutaja, hapana ubaya wowote bali ni jambo zuri pia Ienye kuzidisha mapenzi baina ya mume na mke. Pia mume anaweza kukopeshwa mahari na mkewe akaja kumlipa baadaye.

 


Lakini kulingana na hadithi ya Mtume (s.a.w) mtu akimlaghai mwanamke kuwa atamlipa mahari hapo baadaye iii akubali wafunge naye ndoa na huku ana nia ya kutomlipa, basi hiyo ndoa haitosihi na huyo mwanamume atahesabiwa kuwa anakaa kimada na huyo mwanamke mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w). Mahari ndiyo inayomuhalalishia mume tendo Ia ndoa kwa mkewe kama tunavyojifunza katika hadithi:

 


Uqbah bin Amir (r. a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) amesema: Jambo ?a msingi katika ndoa ni kwamba utimize kwanza kutoa idle kilichofanya sehemu za sin (za mwanamke) kuwa halali (kwako). (Bukhari Muslim).

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

image Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika. Soma Zaidi...

image Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Maana ya hadathi na aina zake
Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi Soma Zaidi...

image Ni kwa nini riba imeharamishwa kwenye Uislamu
Hapa utajifinza uharamu wa riba na sababu za kuharamishwa kwake. Soma Zaidi...

image Ni nini maana ya swala
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala. Soma Zaidi...

image Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

image Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake. Soma Zaidi...

image Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu. Soma Zaidi...

image Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.
Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...