Taratibu za mahari katika uislamu

Taratibu za mahari katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.

Mahari

Kabla ya mkataba wa ndoa kupitishwa jambo muhimu ni mwanamke kutaja kiasi cha mahari atakacho penda kupokea kama hidaya au zawadi anayopewa kwa amri ya Mwenyezi Mungu (s.w) kutoka kwa anayemuoa. Uhuru wa kutamka kiasi cha mahari uko kwa muolewaji na bila ya mahari hayo kutolewa taslimu au kwa ahadi ya kulipa baadaye, ndoa haiswihi. Msititizo wa mahari unapatikana katika aya zifuatazo:

 

Na wapeni wanawake mahari yao, hali ya kuwa ni hidaya (aliyowapa Mwenyezi Mungu). (Lakini hao wake zenu) wakikupeni kwa radhi ya nafsi zao kitu katika hayo (mahari) basi kuleni kwafuraha na kunufaika. (4:4).

 

"...Na (mmehalalishiwa kuwaoa) wanawake wema wa Kiislamu na wanawake wema katika wale waliopewa Kitabu kabla yen u,mtakapowapa mahari yao, kafunga nao ndoa..." (5:5)

 


Katika aya hizi tunajifunza kuwa kutoa mahari kuwapa wanawake tunaowaoa ni jambo Ia lazima aliloliamrisha Mwenyezi Mungu (s.w), lakini wenye kuolewa kwa hiari yao wenyewe, wakiamua kuyasamehe mahari hayo au kuyapunguza hata baada ya kutaja, hapana ubaya wowote bali ni jambo zuri pia Ienye kuzidisha mapenzi baina ya mume na mke. Pia mume anaweza kukopeshwa mahari na mkewe akaja kumlipa baadaye.

 


Lakini kulingana na hadithi ya Mtume (s.a.w) mtu akimlaghai mwanamke kuwa atamlipa mahari hapo baadaye iii akubali wafunge naye ndoa na huku ana nia ya kutomlipa, basi hiyo ndoa haitosihi na huyo mwanamume atahesabiwa kuwa anakaa kimada na huyo mwanamke mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w). Mahari ndiyo inayomuhalalishia mume tendo Ia ndoa kwa mkewe kama tunavyojifunza katika hadithi:

 


Uqbah bin Amir (r. a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) amesema: Jambo ?a msingi katika ndoa ni kwamba utimize kwanza kutoa idle kilichofanya sehemu za sin (za mwanamke) kuwa halali (kwako). (Bukhari Muslim).

 

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2940

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...
Maana ya shahada
Maana ya shahada

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno
Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno

Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.

Soma Zaidi...
Misingi ya fiqh
Misingi ya fiqh

Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.

Soma Zaidi...