Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Umuhimu na Hekima ya Sheria ya Mirathi ya Kiislamu

1. Mrithi na Mrithishaji mkuu ni Allah (s.w).

Rejea Qurโ€™an (7:128), (57:10)



2. Sheria ya Kiislamu kuhusu mirathi imezingatia nguzo kubwa ya jamii ambayo ni familia.


3. Mirathi katika Uislamu inahusika tu kwa ndugu na jamaa wa karibu wa marehemu kinasaba wenye sifa za kurithi.


4. Kila mwenye sifa za kurithi, ana fungu lake lililokadiriwa kwa madhumuni ya ustawi wa jamii na kujenga mapenzi ya familia.


5. Uislamu umezingatia uhusiano wa karibu na wa mbali wa kinasaba na marehemu ili kila mmoja apate haki na fungu lake analostahili.


6. Mgawo wa mirathi katika Uislamu unazingatia uwiano wa nafasi na majukumu ya kila mwenye fungu ndani ya jamii.


7. Sheria ya Uislamu juu ya kurithi, inazuia kila aina ya upendeleo, dhuluma, unyanyasaji, n.k miongoni mwa warithi.




Hekima ya Mtoto wa Kiume Kupata Mara Mbili ya Mtoto wa Kike

1. Mtoto wa kiume ndiye mwenye majukumu makubwa ya kulea na kuhudumia familia na jamii kwa ujumla.


2. Mtoto wa kiume pia anajukumu la kuwa walii kwa dada zake pindi inapoidhinishwa kwa nafasi hiyo katika kuwaozesha.


3. Mtoto wa kike ikitokea ameachwa (ametalikiwa), kaka yake ndiye muwajibikaji wa kumtunza mpaka atakapoondoka katika himaya yake.

4. Mtoto wa kike pamoja na kuwa na majukumu machache kulinganisha na wa kiume, bado anafursa ya kupata fungu la mahari yake pia.


5. Mtoto wa kike pamoja na kuwa na fursa ya kumiliki mali na rasilimali, bado hana wajibu wowote wa kutuzimia kuhudumia familia ila kwa dharura.




Udhaifu wa Sheria za Kitwaghuti za Kurithi

- Katika jamii za kijahili, wanawake hawana haki na nafasi ya kurithi chochote.

- Katika zama za Jahiliyah, kabla ya kuja Mtume (s.a.w), sio tu wanawake walikuwa hawarithi, bali wao wenyewe walikuwa wanarithiwa kama mali pia.


- Sheria za kitwaghuti juu ya mirathi zimejengeka katika misingi ya upendeleo, dhuluma, unyanyasaji, n.k.


- Sheria za kitwaghuti hazizingatii sifa na vigezo vya warithi kwa marehemu kinasaba ambapo wasiostahiki wanaweza kupewa na wanaostahiki wakakosa.


- Hakuna mafungu maalum ya kurithi katika sheria ya kitwaghuti, bali kwa vigezo vya kijinsia.


- Sheria za kitwaghuti hazizingatii majukumu ya warithi.

Mfano mwanamke hupewa fungu kubwa kuliko mwanaume kwa kigezo kuwa eti hana uwezo wa kuchuma.


- Sheria za kitwaghuti huzingatia, hali ya maisha, uwezo kati ya warithi badala ya ukaribu wa nasaba na vigezo.



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1510

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria

Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?

Soma Zaidi...
 Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza
Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุงู„ู†ูู‘ุนู’ู…ูŽุงู†ู ุจู’ู†ู ุจูŽุดููŠุฑู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ูู…ูŽุงุŒ ู‚ูŽุงู„ูŽ: ุณูŽู…ูุนู’ุช ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ูŠูŽู‚ู?...

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa

Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut

Soma Zaidi...
Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.

Soma Zaidi...
Sunnah za funga ya ramadhan
Sunnah za funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua
Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Njia haramu za uchumi.
Njia haramu za uchumi.

Njia hizi ni haramu katika kukuza uchumi wako.

Soma Zaidi...