image

Misingi na Maadili Katika Uislamu

5.

Misingi na Maadili Katika Uislamu

MFUMO WA JAMII YA KIISLAMU

5.1. Misingi na Maadili Katika Uislamu

Maana ya Maadili

Ni mwenendo na tabia inayomfikisha mwanaadamu katika hadhi yake yak ukhalifa na kufikia lengo la kuumbwa kwake.


Mtazamo wa Makafiri juu ya Maadili

Wanafalsafa wa kikafiri wamejaribu kutoa majibu ya maswali ya msingi yafuatayo;

1) Ni lipi lengo kuu la maisha?

2) Ni zipi chem.-chem tunazozitegemea kutambua yapi mema na yapi maovu?

3) Nani msimamizi wa maadili katika jamii?

4) Ni kipi kichocheo kinachowafanya watu katika jamii wawe na maadili?



Udhaifu wa majibu ya maswali haya

1) Lengo kuu la maisha hapa duniani ni;

1. Kuishi maisha yenye furaha – Je, ni furaha ya nini, ya aina gani, ya nani?

2. Kufikia utimilifu – Je, ni upi utimilifu?, wa nini? wa nani?, na kivipi?

3. Kutimiza wajibu kwa lengo la kutimiza wajibu – Je, ni lipi hilo lengo?, nani kaliweka?, lina maana gani?




2) Utambuzi wa mema na maovu ni;

1. Kwa kutumia uzoefu (human experience) – Je, ni uzoefu wa nani? wa nini?

Na kwa muda gani?

2. Kwa kutumia silka zetu (intuition) – Je, tutegemee akili ya nani? kizazi kipi?

3. Kwa kufikiri na kuhoji (rationalism) – Je, ni fikira zipi na za nani?



3) Msimamizi wa maadili ni;

1. Kuwa yatasimamiwa na lengo husika – Je, lengo lipi ndio sahihi? n.k.

2. Kanuni zinazooana na hoja, akili (law of practical reason) – Je, ni akili ya nani itumike? Na kivipi?
3. Serikali kwa kutumia vyombo vyake.

4. Maoni ya watu katika jamii – social pressure



4) Motisha wa Kufuata maadili ni;

1. Kutaka malipo na kuepuka adhabu (reward and punishment) – Je, ni nani anayetoa malipo au adhabu?
2. Maumbile ya binaadamu kutii na kuheshimu sheria.



Hivyo, ni wazi kuwa majibu na hoja zote zinaudhaifu mkubwa sana na kamwe haziwezi kumwongozo mwanadamu kimaadili.


Mtazamo wa Uislamu juu ya Maadili

Udhaifu wa majibu ya makafiri juu ya maadili ni kutojua chanzo, hadhi na lengo halisi la mwanaadamu hapa ulimwenguni.
Hivyo, Uislamu unajenga maadili kwa kujibu maswali yafuatayo kwa usahihi;

1) Nini chanzo cha binaadamu? – Ni Allah (s.w)

Rejea Qur’an (15:28-29)



2) Ni ipi hadhi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni? – Ni Khalifa, kiongozi wa

Allah (s.w). Qur’an (2:30-34).



3) Ni lipi lengo kuu la maisha ya mwanaadamu na vyote vinavyomzunguka?

- Mwanaadamu ameumbwa ili kumuabudu Allah (s.w). Qur’an (51:56).

- Viumbe vinavyomzunguka ni kumwezesha binaadamu kufikia lengo lake.

Rejea Qur’an (2:29), (17:70)

4) Ni ipi chem chem ya ujuzi wa mema na maovu?

- Ni Allah (s.w) kupitia Vitabu vyake na Mitume wake. Qur’an (57:25)

- Qur’an na Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))



5) Ni nani msimamizi wa maadili katika?

- Ni imani thabiti juu ya Allah (s.w), siku ya mwisho na nguzo za imani.

Rejea Qur’an (33:36)

- Mamlaka na Dola ya Kiislamu.

Rejea Qur’an (22:41)

6) Ni kipi kichocheo cha watu Kufuata maadili katika jamii?

- Ni kuhofu adhabu ya Allah (s.w) duniani na akhera

Rejea Qur’an (89:25-26)

- Kutarajia msamaha na malipo ya pepo maisha ya akhera.

Qur’an (9:111), (61:10-13)

- Kuhofu mamlaka ya Dola ya Kiislamu.





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 873


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Uislamu na Jamii kwa ujumla
Soma Zaidi...

KUSOMA TAHIYATU NA KUMSWALIA MTUME KWENYE SWALA
11. Soma Zaidi...

Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu? Soma Zaidi...

Ujuwe utaratibu mzima wa funga na kutekeleza ibada ya Swaumu
Soma Zaidi...

Umuhimu wa uchumi katika uislamu
Post hii itakufundisha faida na umuhimu wa kijenga uchumi katika jamii ya kiislamu. Soma Zaidi...

Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu
Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli. Soma Zaidi...

Kugungisha ndoa ya kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Hapa utajifunza jinsi ya kuozesha hatuwa kwa hatuwa. Pia utajifunza masharti ya kuoa na masharti ya kuolewa. Soma Zaidi...

Maana ya Swaumu na Lengo la kufunga
Soma Zaidi...

NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI
Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r. Soma Zaidi...

Maana ya shahada
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza
Soma Zaidi...