5.
5.1. Misingi na Maadili Katika Uislamu
Maana ya Maadili
Ni mwenendo na tabia inayomfikisha mwanaadamu katika hadhi yake yak ukhalifa na kufikia lengo la kuumbwa kwake.
Mtazamo wa Makafiri juu ya Maadili
Wanafalsafa wa kikafiri wamejaribu kutoa majibu ya maswali ya msingi yafuatayo;
1) Ni lipi lengo kuu la maisha?
2) Ni zipi chem.-chem tunazozitegemea kutambua yapi mema na yapi maovu?
3) Nani msimamizi wa maadili katika jamii?
4) Ni kipi kichocheo kinachowafanya watu katika jamii wawe na maadili?
Udhaifu wa majibu ya maswali haya
1) Lengo kuu la maisha hapa duniani ni;
1. Kuishi maisha yenye furaha – Je, ni furaha ya nini, ya aina gani, ya nani?
2. Kufikia utimilifu – Je, ni upi utimilifu?, wa nini? wa nani?, na kivipi?
3. Kutimiza wajibu kwa lengo la kutimiza wajibu – Je, ni lipi hilo lengo?, nani kaliweka?, lina maana gani?
2) Utambuzi wa mema na maovu ni;
1. Kwa kutumia uzoefu (human experience) – Je, ni uzoefu wa nani? wa nini?
Na kwa muda gani?
2. Kwa kutumia silka zetu (intuition) – Je, tutegemee akili ya nani? kizazi kipi?
3. Kwa kufikiri na kuhoji (rationalism) – Je, ni fikira zipi na za nani?
3) Msimamizi wa maadili ni;
1. Kuwa yatasimamiwa na lengo husika – Je, lengo lipi ndio sahihi? n.k.
2. Kanuni zinazooana na hoja, akili (law of practical reason) – Je, ni akili ya nani itumike? Na kivipi?
3. Serikali kwa kutumia vyombo vyake.
4. Maoni ya watu katika jamii – social pressure
4) Motisha wa Kufuata maadili ni;
1. Kutaka malipo na kuepuka adhabu (reward and punishment) – Je, ni nani anayetoa malipo au adhabu?
2. Maumbile ya binaadamu kutii na kuheshimu sheria.
Hivyo, ni wazi kuwa majibu na hoja zote zinaudhaifu mkubwa sana na kamwe haziwezi kumwongozo mwanadamu kimaadili.
Mtazamo wa Uislamu juu ya Maadili
Udhaifu wa majibu ya makafiri juu ya maadili ni kutojua chanzo, hadhi na lengo halisi la mwanaadamu hapa ulimwenguni.
Hivyo, Uislamu unajenga maadili kwa kujibu maswali yafuatayo kwa usahihi;
1) Nini chanzo cha binaadamu? – Ni Allah (s.w)
Rejea Qur’an (15:28-29)
2) Ni ipi hadhi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni? – Ni Khalifa, kiongozi wa
Allah (s.w). Qur’an (2:30-34).
3) Ni lipi lengo kuu la maisha ya mwanaadamu na vyote vinavyomzunguka?
- Mwanaadamu ameumbwa ili kumuabudu Allah (s.w). Qur’an (51:56).
- Viumbe vinavyomzunguka ni kumwezesha binaadamu kufikia lengo lake.
Rejea Qur’an (2:29), (17:70)
4) Ni ipi chem chem ya ujuzi wa mema na maovu?
- Ni Allah (s.w) kupitia Vitabu vyake na Mitume wake. Qur’an (57:25)
- Qur’an na Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))
5) Ni nani msimamizi wa maadili katika?
- Ni imani thabiti juu ya Allah (s.w), siku ya mwisho na nguzo za imani.
Rejea Qur’an (33:36)
- Mamlaka na Dola ya Kiislamu.
Rejea Qur’an (22:41)
6) Ni kipi kichocheo cha watu Kufuata maadili katika jamii?
- Ni kuhofu adhabu ya Allah (s.w) duniani na akhera
Rejea Qur’an (89:25-26)
- Kutarajia msamaha na malipo ya pepo maisha ya akhera.
Qur’an (9:111), (61:10-13)
- Kuhofu mamlaka ya Dola ya Kiislamu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani.
Soma Zaidi...Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.
Soma Zaidi...Taratibu za Kutaliki KiislamuKama palivyo na taratibu za kuoa Kiislamu ndivyo hivyo pia ilivyo katika kuvunja ndoa.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.
Soma Zaidi...Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga.
Soma Zaidi...