image

Misingi na Maadili Katika Uislamu

5.

Misingi na Maadili Katika Uislamu

MFUMO WA JAMII YA KIISLAMU

5.1. Misingi na Maadili Katika Uislamu

Maana ya Maadili

Ni mwenendo na tabia inayomfikisha mwanaadamu katika hadhi yake yak ukhalifa na kufikia lengo la kuumbwa kwake.


Mtazamo wa Makafiri juu ya Maadili

Wanafalsafa wa kikafiri wamejaribu kutoa majibu ya maswali ya msingi yafuatayo;

1) Ni lipi lengo kuu la maisha?

2) Ni zipi chem.-chem tunazozitegemea kutambua yapi mema na yapi maovu?

3) Nani msimamizi wa maadili katika jamii?

4) Ni kipi kichocheo kinachowafanya watu katika jamii wawe na maadili?



Udhaifu wa majibu ya maswali haya

1) Lengo kuu la maisha hapa duniani ni;

1. Kuishi maisha yenye furaha – Je, ni furaha ya nini, ya aina gani, ya nani?

2. Kufikia utimilifu – Je, ni upi utimilifu?, wa nini? wa nani?, na kivipi?

3. Kutimiza wajibu kwa lengo la kutimiza wajibu – Je, ni lipi hilo lengo?, nani kaliweka?, lina maana gani?




2) Utambuzi wa mema na maovu ni;

1. Kwa kutumia uzoefu (human experience) – Je, ni uzoefu wa nani? wa nini?

Na kwa muda gani?

2. Kwa kutumia silka zetu (intuition) – Je, tutegemee akili ya nani? kizazi kipi?

3. Kwa kufikiri na kuhoji (rationalism) – Je, ni fikira zipi na za nani?



3) Msimamizi wa maadili ni;

1. Kuwa yatasimamiwa na lengo husika – Je, lengo lipi ndio sahihi? n.k.

2. Kanuni zinazooana na hoja, akili (law of practical reason) – Je, ni akili ya nani itumike? Na kivipi?
3. Serikali kwa kutumia vyombo vyake.

4. Maoni ya watu katika jamii – social pressure



4) Motisha wa Kufuata maadili ni;

1. Kutaka malipo na kuepuka adhabu (reward and punishment) – Je, ni nani anayetoa malipo au adhabu?
2. Maumbile ya binaadamu kutii na kuheshimu sheria.



Hivyo, ni wazi kuwa majibu na hoja zote zinaudhaifu mkubwa sana na kamwe haziwezi kumwongozo mwanadamu kimaadili.


Mtazamo wa Uislamu juu ya Maadili

Udhaifu wa majibu ya makafiri juu ya maadili ni kutojua chanzo, hadhi na lengo halisi la mwanaadamu hapa ulimwenguni.
Hivyo, Uislamu unajenga maadili kwa kujibu maswali yafuatayo kwa usahihi;

1) Nini chanzo cha binaadamu? – Ni Allah (s.w)

Rejea Qur’an (15:28-29)



2) Ni ipi hadhi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni? – Ni Khalifa, kiongozi wa

Allah (s.w). Qur’an (2:30-34).



3) Ni lipi lengo kuu la maisha ya mwanaadamu na vyote vinavyomzunguka?

- Mwanaadamu ameumbwa ili kumuabudu Allah (s.w). Qur’an (51:56).

- Viumbe vinavyomzunguka ni kumwezesha binaadamu kufikia lengo lake.

Rejea Qur’an (2:29), (17:70)

4) Ni ipi chem chem ya ujuzi wa mema na maovu?

- Ni Allah (s.w) kupitia Vitabu vyake na Mitume wake. Qur’an (57:25)

- Qur’an na Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))



5) Ni nani msimamizi wa maadili katika?

- Ni imani thabiti juu ya Allah (s.w), siku ya mwisho na nguzo za imani.

Rejea Qur’an (33:36)

- Mamlaka na Dola ya Kiislamu.

Rejea Qur’an (22:41)

6) Ni kipi kichocheo cha watu Kufuata maadili katika jamii?

- Ni kuhofu adhabu ya Allah (s.w) duniani na akhera

Rejea Qur’an (89:25-26)

- Kutarajia msamaha na malipo ya pepo maisha ya akhera.

Qur’an (9:111), (61:10-13)

- Kuhofu mamlaka ya Dola ya Kiislamu.





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 871


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali
Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO. Soma Zaidi...

KUSOMA TAHIYATU NA KUMSWALIA MTUME KWENYE SWALA
11. Soma Zaidi...

Haki ya Serikali kuzuia Dhulma
Soma Zaidi...

Wafundisheni kuswali watoto wenu
Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10 Soma Zaidi...

Mambo gani ni Haramu kwa mwenye janaba?
Hadathi ya kati na kati (Janaba). Soma Zaidi...

Umuhimu na nafasi za hijjah katika uislamu
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kupanga uzazi na uzazi wa mpango katika uislamu
Soma Zaidi...

Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga. Soma Zaidi...

Je ni zipi nguzo za uislamu, na ni ngapi nguzo za uislamu?
Post hii itakujuza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...