image

Misingi na Maadili Katika Uislamu

5.

Misingi na Maadili Katika Uislamu

MFUMO WA JAMII YA KIISLAMU

5.1. Misingi na Maadili Katika Uislamu

Maana ya Maadili

Ni mwenendo na tabia inayomfikisha mwanaadamu katika hadhi yake yak ukhalifa na kufikia lengo la kuumbwa kwake.


Mtazamo wa Makafiri juu ya Maadili

Wanafalsafa wa kikafiri wamejaribu kutoa majibu ya maswali ya msingi yafuatayo;

1) Ni lipi lengo kuu la maisha?

2) Ni zipi chem.-chem tunazozitegemea kutambua yapi mema na yapi maovu?

3) Nani msimamizi wa maadili katika jamii?

4) Ni kipi kichocheo kinachowafanya watu katika jamii wawe na maadili?



Udhaifu wa majibu ya maswali haya

1) Lengo kuu la maisha hapa duniani ni;

1. Kuishi maisha yenye furaha – Je, ni furaha ya nini, ya aina gani, ya nani?

2. Kufikia utimilifu – Je, ni upi utimilifu?, wa nini? wa nani?, na kivipi?

3. Kutimiza wajibu kwa lengo la kutimiza wajibu – Je, ni lipi hilo lengo?, nani kaliweka?, lina maana gani?




2) Utambuzi wa mema na maovu ni;

1. Kwa kutumia uzoefu (human experience) – Je, ni uzoefu wa nani? wa nini?

Na kwa muda gani?

2. Kwa kutumia silka zetu (intuition) – Je, tutegemee akili ya nani? kizazi kipi?

3. Kwa kufikiri na kuhoji (rationalism) – Je, ni fikira zipi na za nani?



3) Msimamizi wa maadili ni;

1. Kuwa yatasimamiwa na lengo husika – Je, lengo lipi ndio sahihi? n.k.

2. Kanuni zinazooana na hoja, akili (law of practical reason) – Je, ni akili ya nani itumike? Na kivipi?
3. Serikali kwa kutumia vyombo vyake.

4. Maoni ya watu katika jamii – social pressure



4) Motisha wa Kufuata maadili ni;

1. Kutaka malipo na kuepuka adhabu (reward and punishment) – Je, ni nani anayetoa malipo au adhabu?
2. Maumbile ya binaadamu kutii na kuheshimu sheria.



Hivyo, ni wazi kuwa majibu na hoja zote zinaudhaifu mkubwa sana na kamwe haziwezi kumwongozo mwanadamu kimaadili.


Mtazamo wa Uislamu juu ya Maadili

Udhaifu wa majibu ya makafiri juu ya maadili ni kutojua chanzo, hadhi na lengo halisi la mwanaadamu hapa ulimwenguni.
Hivyo, Uislamu unajenga maadili kwa kujibu maswali yafuatayo kwa usahihi;

1) Nini chanzo cha binaadamu? – Ni Allah (s.w)

Rejea Qur’an (15:28-29)



2) Ni ipi hadhi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni? – Ni Khalifa, kiongozi wa

Allah (s.w). Qur’an (2:30-34).



3) Ni lipi lengo kuu la maisha ya mwanaadamu na vyote vinavyomzunguka?

- Mwanaadamu ameumbwa ili kumuabudu Allah (s.w). Qur’an (51:56).

- Viumbe vinavyomzunguka ni kumwezesha binaadamu kufikia lengo lake.

Rejea Qur’an (2:29), (17:70)

4) Ni ipi chem chem ya ujuzi wa mema na maovu?

- Ni Allah (s.w) kupitia Vitabu vyake na Mitume wake. Qur’an (57:25)

- Qur’an na Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))



5) Ni nani msimamizi wa maadili katika?

- Ni imani thabiti juu ya Allah (s.w), siku ya mwisho na nguzo za imani.

Rejea Qur’an (33:36)

- Mamlaka na Dola ya Kiislamu.

Rejea Qur’an (22:41)

6) Ni kipi kichocheo cha watu Kufuata maadili katika jamii?

- Ni kuhofu adhabu ya Allah (s.w) duniani na akhera

Rejea Qur’an (89:25-26)

- Kutarajia msamaha na malipo ya pepo maisha ya akhera.

Qur’an (9:111), (61:10-13)

- Kuhofu mamlaka ya Dola ya Kiislamu.





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1093


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir Soma Zaidi...

Aina za swala..
Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha Najisi ndogo
Soma Zaidi...

maana ya Eda na aina zake
Ni kipindi au muda wa kungojea mwanamke aliyepewa talaka (aliyeachwa) au kufiwa na mumewe kabla ya kuolewa na mume mwingine. Soma Zaidi...

Mafunzo ya swala
Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike? Soma Zaidi...

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu
Soma Zaidi...

malezi ya mtoto mchanga baada ya talaka
Soma Zaidi...

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Soma Zaidi...

Zijuwe nguzo 17 za swala.
Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala. Soma Zaidi...

lengo la kuswali za faradhi na suna
Soma Zaidi...

Maana ya swala
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...

Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...