picha

Zijue sababu za kupungukiwa damu mwilini

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kupungukiwa damu mwilini, ni ugonjwa unaotokana sana hasa kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano ingawa na kwa watu wazima.

Sababu za upungufu wa damu mwilini.

Hili ni tatizo ambalo ushambulia sana watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano na watu wazima, zifuatazo ni sababu za upungufu wa damu

1. Kiwango kidogo Cha damu ambacho uzalishwa na mifupa inayoitwa kwa kitaalamu bone marrow,hii ni mifupa ambapo chembechembe ndogo za damu uzalishwa ambazo kwa kitaalamu huitwa (red blood cell) ushindwa kuzalisha vizuri hizi seli kwa sababu ya maambukizi kwenye mifupa hiyo.

 

2. Kuharibika kwa kiwango kikubwa Cha seli kabla ya mda wake. Upungufu wa damu utokea kwa sababu ya kuharibika kwa seli kabla ya mda wake, hizi seli zinazobeba damu kwenye mwili huaribika kabla ya mda wake kutimia inawezekana kuwa ni maambukizi kama vile malaria, pneumonia ,Homa kali haya magonjwa yote usababisha seli kufa kabla ya mda wake.

 

3. Damu kushindwa kuganda pale mtu anapopata ajali utokea pale ambapo mtu akipata ajali yoyote Damu uendelea kutoka na kusababisha seli nyingi kutoka kwenye mzunguko wake na damu upungua, huu ni ugonjwa ambao hawapaswi kuendelea kuwepo kwa sababu unatibika sana hospitalini na watu wanapona

 

4. Wakati mwingine tatizo la kuishiwa damu ni kutokana na ugonjwa wa kuridhi ambapo seli huwa tofauti na za wengine yaan kwa kitaalamu huitwa sickle cell huu ni ugonjwa wa kuridhi ambapo seli nyekundu za damu huwa tofauti na nyingine hali hii usababisha hewa kushindwa kupita kwenye seli na damu upungua, ugonjwa huu ni hatari usipotibiwa unaweza kuleta madhara makubwa zaidi na hata kifo kwa hiyo tuwe na tahadhari kwa watu wenye ugonjwa huu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3559

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 web hosting     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Jinsi ya kujikinga na U.T.I inayijirudia rudia.

Endapo U.T.I inajirudiarudia baada yavkutibiwa inawezabkuwa ikakupa mawazo mengi. Katika post hii nitakufafanulia nini ufanye.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya mwili.

Posti hii inahusu zaidi sababu ya kuwepo kwa maumivu ya mwili kwa sababu tunaweza kuhisi maumivu kwenye sehemu za mwili kwa sababu mbalimbali kama tutakavyoona hapo chini

Soma Zaidi...
fahamu kuhusu vitamini B na faida zake

makala hii inakwenda kukupa faida, kazi na athari za vitamini B mwilini. Nini hutokea endapo utakuwa na upungufu wa vitamini B mwilini?

Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...
Njia za kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya njia za kuongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini

Soma Zaidi...