Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.

Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

1.Kwanza kabisa tunamsafisha Mgonjwa nywele ili kuondoa wadudu kama vile chawa na mba.

Tunafanya hivyo kwa wakati mwingine kunakuwepo na chawa au mba ambao uweza kumsumbua mgonjwa na kufanya hali yake iweze kuwa mbaya kwa sababu chawa wanafyonza damu kama mgonjwa amelala kwa mda wa mwezi mmoja na hakuna usafi tunaona kuwa ni hatari kwa mgonjwa na pengine anahisi maumivu na hawezi kujikuna na hali hii usababisha hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

 

2. Tunafanyia mgonjwa usafi wa nywele ili kuweza kuruhusu vizuri mzunguko wa damu.

Kwa kufanya hivyo mzunguko wa damu inaweza kwenda vizuri kwa sababu kama kuna mba  kwa mda mrefu na sehemu hiyo mzunguko wa damu utakuwa shida kwa hiyo tunapaswa kusafisha sehemu hiyo ili kuweza kuruhusu mzunguko wa damu uenda vizuri.

 

3. Tunamsafisha Mgonjwa nywele ili kuweza kumfanya awe safi na kuweza kumpatia ahueni ya ugonjwa na anakuwa na matumizi mazuri na kujisikia vizuri kwamba anapendwa na kuna Watu wanamjali na pia mwonekano wa mgonjwa unakuwa vizuri.

 

4.Kwa hiyo tunapaswa kuwafanyia wagonjwa wetu usafi wa nywele kwa sababu kwenye nywele kunakuwepo na uchafu mwingi ambao Mgonjwa kama hajiwezi anashindwa kuomba masada ila mkijiongeza mkamsafisha anajisikia vizuri na anaweza kupata nafuu kwa sababu ya usafi mnaomuonyesha kwa hiyo tuwajali wagonjwa wetu hasa wanapokuwa hawajiwezi kwa kuwafanyia usafi kwa sababu na yenyewe ni sehemu ya tiba

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2022/02/18/Friday - 12:33:15 pm     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 602

Post zifazofanana:-

Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini. Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa upele
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele. Soma Zaidi...

Ratiba ya chanjo ya polio
Posti hii inahusu zaidi namna chanjo ya polio inavyotolewa na ratiba zake yaani kuanzia siku ya kwanza mpaka pale mtoto anapomaliza chanjo hii kwa hiyo tuone ratiba ya chanjo ya polio. Soma Zaidi...

Ujue ugonjwa wa kuishiwa na damu
post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuishiwa damu kwa kitaalamu huitwa(Anemia) ni ugonjwa wa kuishiwa na damu mwilini na kusababisha maisha ya mtu kuwa hatarini Soma Zaidi...

Je na kwa upande wa mwanaume kuumwa upande wa kushoto wa tumbo kuna shida gani?
Maumivu ya tumbo upande wa kushoti, kwa mwanamke huwenda ikawa ni ujauzito ama shida nyingine za kiafya kama tumbo kujaa gesi, kukosa choo na kadhalika. Sasa vipi kwa wanaume ni ipi hasa sababu' Soma Zaidi...

Dalili za mimba ya siku 4
Unaweza kutaka kujuwa je naweza kupata dalili za mimba baada ya siku nne toka ujauzito kutungwa? ama baada ya siku nne toka kushiriki tendo la ndoa. Makala hii itakwenda kujibu maswali haya na mengineyo. Soma Zaidi...

Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuzuia Malaria kwa wajawazito. Soma Zaidi...

Dawa za mitishamba za kutibu meno
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno Soma Zaidi...

Dalili za Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa. Soma Zaidi...

Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Dalili za Pua iliyovunjika
posti hii inahusu dalili za Pua iliyovunjika, pia inaitwa fracture ya pua, ni kuvunjika au kupasuka kwa mfupa katika pua yako Soma Zaidi...

Namna ya kusaidia vijana wakati wa kubarehe
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia vijana wakati wa kubarehe, ni njia za kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa na mwelekeo , Soma Zaidi...