Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.

Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

1.Kwanza kabisa tunamsafisha Mgonjwa nywele ili kuondoa wadudu kama vile chawa na mba.

Tunafanya hivyo kwa wakati mwingine kunakuwepo na chawa au mba ambao uweza kumsumbua mgonjwa na kufanya hali yake iweze kuwa mbaya kwa sababu chawa wanafyonza damu kama mgonjwa amelala kwa mda wa mwezi mmoja na hakuna usafi tunaona kuwa ni hatari kwa mgonjwa na pengine anahisi maumivu na hawezi kujikuna na hali hii usababisha hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

 

2. Tunafanyia mgonjwa usafi wa nywele ili kuweza kuruhusu vizuri mzunguko wa damu.

Kwa kufanya hivyo mzunguko wa damu inaweza kwenda vizuri kwa sababu kama kuna mba  kwa mda mrefu na sehemu hiyo mzunguko wa damu utakuwa shida kwa hiyo tunapaswa kusafisha sehemu hiyo ili kuweza kuruhusu mzunguko wa damu uenda vizuri.

 

3. Tunamsafisha Mgonjwa nywele ili kuweza kumfanya awe safi na kuweza kumpatia ahueni ya ugonjwa na anakuwa na matumizi mazuri na kujisikia vizuri kwamba anapendwa na kuna Watu wanamjali na pia mwonekano wa mgonjwa unakuwa vizuri.

 

4.Kwa hiyo tunapaswa kuwafanyia wagonjwa wetu usafi wa nywele kwa sababu kwenye nywele kunakuwepo na uchafu mwingi ambao Mgonjwa kama hajiwezi anashindwa kuomba masada ila mkijiongeza mkamsafisha anajisikia vizuri na anaweza kupata nafuu kwa sababu ya usafi mnaomuonyesha kwa hiyo tuwajali wagonjwa wetu hasa wanapokuwa hawajiwezi kwa kuwafanyia usafi kwa sababu na yenyewe ni sehemu ya tiba

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1316

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰5 web hosting    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.

Soma Zaidi...
Visababishi vya magonjwa.

Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma ya kwanza

Huduma ya kwanza ni huduma anayopewa mgonjwa au mtu yeyote aliyepata ajali kabla ya kumpeleka hospitalini

Soma Zaidi...
Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure

Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโ€™ATWA NA NYUKI

Kungโ€™atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

Soma Zaidi...
Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu

Soma Zaidi...
fahamu kuhusu vitamini B na faida zake

makala hii inakwenda kukupa faida, kazi na athari za vitamini B mwilini. Nini hutokea endapo utakuwa na upungufu wa vitamini B mwilini?

Soma Zaidi...
Athari za mkojo mwilini.

Posti hii inahusu zaidi athari za mkojo mwilini, kwa kawaida tunafahamu kwamba mkojo ni matokeo ya mkusanyiko wa uchafu wa maji maji yanayokusanyika kutoka mwilini ikiwa mkojo umebaki mwilini usababisha madhara mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Hatari ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...