Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa


image


Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.


Kutayammamu

Kutayammamu ni kujitwaharisha kwa kutumia udongo safi. Waislamu huruhusiwa kujitwaharisha kwa kutayammamu katika hali ya dharura ya:
(i)Ugonjwa usioruhusu kutumia maji.
(ii)Kuwa safarini na kukosa maji ya kutumia au kuwa katika mazingira ya safari yasiyoruhusu kutumia maji.
(iii)Kukosa maji.
Tunajifunza haya katika aya ifuatayo:

 

“Na mkiwa wagonjwa au mumo safarini au mmoja wenu ametoka chooni au mmeingiliana na wanawake, na hamkupata maji, basi, kusudieni udongo ulio safi (tayammamuni) kwa kuzipaka nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi Mw enyezi Mungu kukutieni katika taabu; bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru”. (5:6)

 


Katika aya hii tunajifunza kuwa kutayammamu kumeruhusiwa kwa wakati wa dharura tu. Funzo hili tunalipata katika maneno ya Allah kuwa, “Hapendi Allah kukutieni katika taabu”

 


Masharti ya Kutayammamu

Tayammamu haitaswihi mpaka yatakapozingatiwa masharti yafuatayo:
1. Ipatikane dharura inayompelekea mtu kuruhusiwa kutayammarnu.
2. Pawe na hitajio la tayammamu kama vile kuswali, kutufu n.k.
3. Kama kusudio la kutayammarnu ni kutekeleza swala ya faradh, tayammamu hiyo ifanyilce baada ya kuingia wakati wa swala hiyo.
4. Pawe na udongo safe (ulio twahara na ulio katika asili yake) ulio mkavu na wenye vumbi vumbi.

 

Nguzo za Tayammam
Nguzo za tayammam zinabainishwa na aya ifuatayo:
`... Basi kusudieni udongo ulio safi na kupaka nyuso zenu nn mikono yenu..." (4:43)
Aya hii inabainisha kuwa nguzo za tayammam ni:

 


(i)Nia (kukusudia udongo).
(ii)Kupaka uso.
(iii)Kupaka mikono.
(iv)Kufuata utaratibu huu.
Nampa ya Kutayammamu
(i)Kutia nia. Nia huwekwa pale Muislamu anapokusudia udongo na kuutayarisha kwa ajili ya tayammamu.
(ii)Kupaka uso. Piga udongo uliokusudia kwa viganja vyote viwili vya mikono, kisha puliza viganja iii takataka na vijiwe jiwe vilivyo juu yake vitoke. Kisha paka uso wako kwa kutumia viganja viwili kwa pamoja.

 


(iii) Kupaka mikono. Anza kupaka mkono wa kulia kwa kiganja cha kushoto. Weka kiganja cha kushoto nyuma ya kiganja cha kulia. Paka mkono wa kulia kuanzia hapo kwa kurudisha kiganja cha kushoto kinyume nyume mpaka kwenye fundo kisha kupaka sehemu ya juu ya mkono wa kulia na kuishia kwenye kidole gumba bila ya kuugusa kiganja mkono wa kulia. Utarudia zoezi hilo kupaka mkono wa kushoto.

 


Kutumia Ukuta kwa Ajili ya Tayammamu

 


Mtume (s.a.w) aliwahi kutayammamu kwa kutumia ukuta wa nyumba kama inavyobainika katika hadith ifuatayo:
“Abu Juhaim Al-A nsary (r.a) amehadithia kuw a Mtume w a Allah (Rehema na amani ziwe juu yake) alikuja kutoka upande wa Bir-al-Jamal. Mtu mmoja alimuona akamsalimia. Lakini Mtume hakumjibu, bali alienda kwenye ukuta wa nyumba akapakaza viganja vyake vumbi la ukuta kisha akapaka uso wake wote, kisha mkono wa kulia na wa kushoto, ndipo akamrudishia salamu ”. (Bukhari na Muslim).

 


Kutokana na hadithi hii tunajifunza kuwa vumbi kwa ajili ya tayammamu si lazima liwe la ardhini tu bali ukuta au jiwe au sehemu yoyote yenye vumbi vumbi iliyotwahara inafaa kutumika kwa ajili ya tayammamu. Kwa mfano wakati wa mvua ambapo udongo umelowana ukuta wa nyumba au ukuta wa chombo cha usafiri au sehemu yoyote yenye vumbi vumbi au iliyokavu na twahara, itakuwa aula kuitumia kwa tayammamu.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...

image Mifumo ya benki ya kiislamu.
Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu
Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

image Mifumo ya benki na kazi zake
Hapa utajifunza kazi za benki. Soma Zaidi...

image Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii. Soma Zaidi...

image Tarstibu za kulipa swaumu ya Ramadhani
Hapa utajifunza namna ambayo utatakiwa kulipa funga ya Ramadhani kwa siku ambazo hukufunga Soma Zaidi...

image Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...