NAMNA YA KUTAYAMAMU HATUWA KWA HATUWA


image


Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.


Kutayammamu

Kutayammamu ni kujitwaharisha kwa kutumia udongo safi. Waislamu huruhusiwa kujitwaharisha kwa kutayammamu katika hali ya dharura ya:
(i)Ugonjwa usioruhusu kutumia maji.
(ii)Kuwa safarini na kukosa maji ya kutumia au kuwa katika mazingira ya safari yasiyoruhusu kutumia maji.
(iii)Kukosa maji.
Tunajifunza haya katika aya ifuatayo:

 

“Na mkiwa wagonjwa au mumo safarini au mmoja wenu ametoka chooni au mmeingiliana na wanawake, na hamkupata maji, basi, kusudieni udongo ulio safi (tayammamuni) kwa kuzipaka nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi Mw enyezi Mungu kukutieni katika taabu; bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru”. (5:6)

 


Katika aya hii tunajifunza kuwa kutayammamu kumeruhusiwa kwa wakati wa dharura tu. Funzo hili tunalipata katika maneno ya Allah kuwa, “Hapendi Allah kukutieni katika taabu”

 


Masharti ya Kutayammamu

Tayammamu haitaswihi mpaka yatakapozingatiwa masharti yafuatayo:
1. Ipatikane dharura inayompelekea mtu kuruhusiwa kutayammarnu.
2. Pawe na hitajio la tayammamu kama vile kuswali, kutufu n.k.
3. Kama kusudio la kutayammarnu ni kutekeleza swala ya faradh, tayammamu hiyo ifanyilce baada ya kuingia wakati wa swala hiyo.
4. Pawe na udongo safe (ulio twahara na ulio katika asili yake) ulio mkavu na wenye vumbi vumbi.

 

Nguzo za Tayammam
Nguzo za tayammam zinabainishwa na aya ifuatayo:
`... Basi kusudieni udongo ulio safi na kupaka nyuso zenu nn mikono yenu..." (4:43)
Aya hii inabainisha kuwa nguzo za tayammam ni:

 


(i)Nia (kukusudia udongo).
(ii)Kupaka uso.
(iii)Kupaka mikono.
(iv)Kufuata utaratibu huu.
Nampa ya Kutayammamu
(i)Kutia nia. Nia huwekwa pale Muislamu anapokusudia udongo na kuutayarisha kwa ajili ya tayammamu.
(ii)Kupaka uso. Piga udongo uliokusudia kwa viganja vyote viwili vya mikono, kisha puliza viganja iii takataka na vijiwe jiwe vilivyo juu yake vitoke. Kisha paka uso wako kwa kutumia viganja viwili kwa pamoja.

 


(iii) Kupaka mikono. Anza kupaka mkono wa kulia kwa kiganja cha kushoto. Weka kiganja cha kushoto nyuma ya kiganja cha kulia. Paka mkono wa kulia kuanzia hapo kwa kurudisha kiganja cha kushoto kinyume nyume mpaka kwenye fundo kisha kupaka sehemu ya juu ya mkono wa kulia na kuishia kwenye kidole gumba bila ya kuugusa kiganja mkono wa kulia. Utarudia zoezi hilo kupaka mkono wa kushoto.

 


Kutumia Ukuta kwa Ajili ya Tayammamu

 


Mtume (s.a.w) aliwahi kutayammamu kwa kutumia ukuta wa nyumba kama inavyobainika katika hadith ifuatayo:
“Abu Juhaim Al-A nsary (r.a) amehadithia kuw a Mtume w a Allah (Rehema na amani ziwe juu yake) alikuja kutoka upande wa Bir-al-Jamal. Mtu mmoja alimuona akamsalimia. Lakini Mtume hakumjibu, bali alienda kwenye ukuta wa nyumba akapakaza viganja vyake vumbi la ukuta kisha akapaka uso wake wote, kisha mkono wa kulia na wa kushoto, ndipo akamrudishia salamu ”. (Bukhari na Muslim).

 


Kutokana na hadithi hii tunajifunza kuwa vumbi kwa ajili ya tayammamu si lazima liwe la ardhini tu bali ukuta au jiwe au sehemu yoyote yenye vumbi vumbi iliyotwahara inafaa kutumika kwa ajili ya tayammamu. Kwa mfano wakati wa mvua ambapo udongo umelowana ukuta wa nyumba au ukuta wa chombo cha usafiri au sehemu yoyote yenye vumbi vumbi au iliyokavu na twahara, itakuwa aula kuitumia kwa tayammamu.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    5 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    6 Hadiythi za alif lela u lela    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu
Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili. Soma Zaidi...

image Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

image Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

image Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

image Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...

image Ufafanuzi kuhudu mgogoro wa mwezi ni muda gani mtu aanze kufunga.
Je inapoonekana sehemu moja tufunge duania nzima ama tufunge kwa kuangalia mwandamo katika maenro tunayoishi. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya haja
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

image Shart kuu nne za swala
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu masharti ya swala. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake
Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada. Soma Zaidi...