Madhara ya riba kwenye jamii

Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?

8. Tatizo la Riba
Riba ni kupata chochote kile cha ziada kutoka katika mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara. Mwenyezi Mungu anatufahamisha katika Qur’an:

 


Wale wanaokula riba hawasimami ila kama anavyosimama yule ambaye shetani kamzuga kwa kumsawaa; haya ni kwa sababu wamesema, Biashara ni kama riba, hali Mwenyezi Mungu amehalalisha biashara na kuiharamisha riba.(2:275)

 

Mwenyezi Mungu huyafutia (baraka mali ya) riba; na kuyatia baraka (mali iliyotolewa) sadaka (2:2 76).
Madhara ya riba katika jamii

 


(i)Riba inachafua nafsi ya Tajiri na uchumi wake. Tajiri ambaye hayuko tayari kukukopesha mali yake pasi na riba, kamwe hawezi kutoa mali yake bure kuwasaidia wanyonge na wenye dhiki. Tajiri asiye tayari kutoa mali yake kuwasaidia wenziwe wenye dhiki na shida katika jamii huwa mchoyo, bahili, mpupiaji mali, asiyetosheka na utajiri alionao, mfujaji, muonevu na dhalimu. Tajiri mwenye moyo wa namna hii hata kama atajiita Muislamu hawezi kamwe kuchunga mipaka ya halali na haramu katika kuchuma!

 


(ii)Riba inamkandamiza Mnyonge mwenye dhiki. Wanyonge na wenye dhiki katika jamii inayoendesha uchumi wake katika misingi ya riba, hawapati msaada wowote wa bure kutoka kwa matajiri kwa kiasi ambacho wengi wa wale wasiojiweza kabisa kujitosheleza kwa mahitaji muhimu ya maisha yao kwa namna duni sana - wengi hujipatia chakula chao kutoka katika mapipa ya taka (watoto wa mtaani), wengi hujisitiri kwa masalio yaliyookotezwa hapa na pale na wengi makazi yao ni stesheni na sokoni. Hawa, kisaikolojia, hujiona ni watu duni wasio na maana yoyote katika jamii na huwaona matajiri na watu wenye uwezo kuwa ndio wenye maana. Na hapa ndipo inapojengeka chuki baina ya wasionacho kuwachukia walio nacho.

 


(iii) Riba inaharibu uchumi wa jamii na maendeleo yake. Riba na msingi wake wa unyonyaji imma ikitozwa na tajiri mmoja au kikundi cha matajiri, imefanywa msingi wa uchumi wa taifa au wa kimataifa. Kwa bahati mbaya kutokana na mazoea tuliyonayo juu ya vyombo vya uchumi vya kitaifa na kimataifa vinavyoendeshwa katika misingi ya Riba kama vile mabenki ya taifa na shirika la Bima la Kimataifa, baadhi ya watu wamediriki kuhalalisha Riba ya mabenki na Bima. Kuhalalisha huku kwa riba ya mabenki na Bima aidha kumetokana na uzoefu wa uchumi haramu katika jamii zetu au umetokana na kushindwa kuona ubaya wa riba kitaifa au kimataifa.
Waislamu hatuna budi kukumbuka kuwa alichokiharamisha Allah (s.w) kinakuwa ni haramu katika wingi wake na katika uchache wake. Tukichukua mfano wa pombe Mtume (s.a.w.) amesema:

 


Kinacholewesha kikiwa kingi ni haramu pia hata kikiwa kichache. (Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah). Kwa hiyo kilicho haramishwa kwa mtu binafsi, pia ni haramu kwa taifa na ni haramu kwa mataifa yote ulimwenguni. Kwa upande mwingine jambo la haramu litakapotendwa kitaifa litakuwa na athari mbaya zaidi kwa jamii kuliko likitendwa katika kiwango cha mtu binafsi, hali kadhalika jambo baya likitendwa kimataifa huwa na athari kubwa na mbaya zaidi kwa jamii ya mwanadamu kuliko likitendwa katika kiwango cha kitaifa.

 


(iv) Riba ni mali ya dhulma inayonyakuliwa na matajiri kutoka kwa wanyonge kwa njia moja au nyingine kiuchumi, pia riba inaukandamiza na kuudidimiza uchumi wa kitaifa au kimataifa. Mali ya riba kwa kuwa ni mali inayopatikana bila jasho na bila hata ya kushiriki katika mashaka ya uchumi, huwafanya matajiri na wenye uwezo wa kuendesha miradi mbali mbali ya kiuchumi wakae tu bila kazi wakingojea fedha zao zizae katika mabenki ambazo wana kila uhakika wa kuzipata hata itokee gharka ya namna gani. Kwa hiyo kutokana na riba, jamii huwakosa watu wenye uwezo mkubwa wa kuzalisha mali ambao wangaliweza kuendesha miradi mbali mbali ya kiuchumi ambayo ingaliinua uchumi wa taifa na wa kimataifa kwa ujumla.

 


Wataalam wa uchumi wanakiri kuwa riba inaporomosha uchumi. Wamegundua kuwa kadiri kiwango cha riba kinavyokuwa kikubwa ndivyo uchumi unavyozidi kushuka kwa sababu matajiri huona kuwa wanapata faida kubwa zaidi na kwa njia nyepesi isiyotoa jasho lolote wakiweka fedha zao benki kuliko kuziingiza katika miradi ya kiuchumi. Hivyo utaona kuwa riba hupunguza uzalishaji na huongeza gharama za uzalishaji.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/26/Friday - 10:21:01 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1169

Post zifazofanana:-

Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika
Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa. Soma Zaidi...

Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo Soma Zaidi...

Njia haramu za uchumi.
Njia hizi ni haramu katika kukuza uchumi wako. Soma Zaidi...

Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu
Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu. Soma Zaidi...

Mifumo ya benki na kazi zake
Hapa utajifunza kazi za benki. Soma Zaidi...

Tofauti ya uchumi wa kiislamu na uchumi wa kikafiri
Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo. Soma Zaidi...

Nadharia ya uchumi wa kiislamu
Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa. Soma Zaidi...

Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu
Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo Soma Zaidi...

Taratibu za kufanya kazi na kuajiri katika uislamu
Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo. Soma Zaidi...

Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu. Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...