Post hii itakufundisha kuhusu nguzo kuu sita za udhu.
Nguzo za Udhu
Allah (s.w) anatufunza kutia udhu katika aya ifuatayo:
Enyi mlioamini! Mnaposimama ili mkaswali, basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na (osheni) miguu yenu mpaka vifundoni...” (5:6)
Kutokana na aya hii na kutokana na mafundisho ya Mtume (s.a.w) nguzo au faradhi za udhu ni hizi zifuatazo
1. Kutia nia moyoni kuwa unatawadha.
2. Kuosha uso kwa ukamilifu kwa kufikisha maji mpaka kwenye mipaka yote ya uso.
3. Kuosha mikono miwili mpaka vifundoni.
4. Kupaka maji kichwani.
5. Kuosha miguu, mpaka vifundoni.
6. Kufuata utaratibu huu kwa kuanza (1) hadi (5) katika mfuatano huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume
Soma Zaidi...Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.
Soma Zaidi...Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.
Soma Zaidi...