Siku ambazo haziruhusiwi kufunga

Ni haramu kufunga katika masiku haya. Na endapo utafunga basi funga haitakuwa na malipo.

Siku Zilizoharamishwa Kufunga Sunnah

(i)Siku kuu za Iddil-Fitri na Iddil-Hajj

 


Imeharamishwa kufunga katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Abu Sayyid al-Khudri (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema: Hakuna funga katika siku mbili - siku ya (Iddil) Fitr na siku ya (Idd ya) kuchinja.” (Bukhari na Muslim).

 


(ii)Siku za Tashriq
Siku za Tashriq ni mwezi 11 hadi 13 Dhul-Hijjah. Ni haram kufunga
katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Ibn Al-Hazali(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Siku za Tashriqu ni siku za kula na kunywa na kumkumbuka Allah (s.w) (kwa Takbira). (Muslim).

 


(iii)Siku ya Shaka
Siku ya Shaka ni siku moja kabla ya Ramadhani. Yaani mwezi 30 Shaabani ambapo inawezekana ikawa ni siku ya kufunga. Mtume (s.a.w) amekataza kufunga sunnah katika siku hii ya mashaka ila kwa yule mwenye ada ya kufunga. Kwa mfano mtu mwenye ada ya kufunga Jumatatu ameruhusiwa kufunga endapo siku hiyo itaangukia Jumatatu. Hadith ifuatayo inabainisha makatazo haya:

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume wa Allah amesema: “Usifunge siku moja au mbili kabla ya Ramadhani ila kwa mtu yule mwenye ada ya kufunga funga fulani (k.m. funga ya Alhamisi), yeye anaruhusiwa kufunga ” (Muslim).

 


Inatakiwa siku moja au mbili kabla ya Ramadhani tusifunge ili tuweze kuukabili tukiwa na nguvu mpya na ili tutofautishe funga ya Ramadhani na funga za Sunnah.

 


(iv) Siku ya Ijumaa
Mtume (s.a.w) amekataza funga ya Sunnah katika siku ya Ijumaa tu, lakini kama mtu ana tabia ya kufunga sunnah, ikatokea siku ya Ijumaa ni miongoni mwa siku anazofunga, basi hapana ubaya. Tunajifunza haya katika Hadith zifuatazo:

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Na asifunge siku ya Ijumaa yeyote miongoni mwenu; ila tu akiwa ameanza kufunga kabla yake au ameendelea kufunga baada yake”. (Muslim).

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Usiuchopoe usiku kabla ya Ijumaa ukafanya usiku pekee kwa kusimama kwa swala na usiichague siku ya Ijumaa pekee kati ya siku za wiki kuwa ndio siku ya kufunga, ila kama mmoja wenu ana tabia ya kufunga sunnah na ikatokea siku ya Ijumaa imeangukia katika tarehe anayopaswa kufunga. ” (Muslim).

 

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/18/Thursday - 07:55:48 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 14406

Post zifazofanana:-

Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii. Soma Zaidi...

Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu. Soma Zaidi...

Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki. Soma Zaidi...

Hili ndio lengo la kufunga.
Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga. Soma Zaidi...

Mambo ambayo hayafunguzi funga
Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya. Soma Zaidi...

Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu
Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga. Soma Zaidi...

Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku. Soma Zaidi...

Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu. Soma Zaidi...

Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah
Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao Soma Zaidi...

Watu wanaolazimika kufunga mwezi wa Ramadhani
Hapa utajifunza watu ambao wanalazimika kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu
Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii. Soma Zaidi...