Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.
Njia za kuwalisha wagonjwa ambao hawawezi kujilisha mwenyewe.
1 Kwanza kabisa wagonjwa wengi wanashindwa kujilisha wenyewe kwa sababu mbalimbali labda hali zao haziwahusu kwa sababu ya aina ya ugonjwa kwa hiyo tunapaswa kuwalisha kwa sababu chakula na dawa vinaendana kwa hiyo Mgonjwa hasipokula hawezi kupona mapema kwa hiyo hata mgonjwa kama mgonjwa hawezi kujilisha anapaswa kulishwa kwa kufuata njia zifuatazo.
2. Mweke Mgonjwa kwenye hali ambayo ataweza kukaa vizuri na kula chakula na kama hajiwezi mwekee kitu cha kumfanya aweze kukaa vizuri na msafishe kinywa kabla ya kumpatia chakula kwa sababu kinywa kikiwa kisafi uongeza hamu ya kula.
3. Mwekee kitambaa kwenye kifua ili kuweza kumkinga na vyakula ambavyo vinaweza kudondokea nguo na pia leta sahani ya chakula karibu na mgonjwa na kumbuka kunawa mikono kabla ya kumlisha Mgonjwa na baada ya kumlisha Mgonjwa.
4. Kaa karibu na mgonjwa na pia ni vizuri kuwa na msaidizi wakati wa kumlisha Mgonjwa na chukua chakula cha mgonjwa na kiweke kwenye kijiko kuanzia kwenye mdomo wa kijiko na mlishe kidogo kidogo na wakati wa kumlisha subiri kwanza atafute ameze na ndipo umwekee chakula kingine .
5.Na pale Mgonjwa unapomlisha mruhusu kupumzika kidogo akimaliza kumeza na mlishe tena na akiwa amepumzika ongea naye taratibu na pia endelea kumlisha mpaka atakaposhiba na kama anahisi kichefuchefu mpumzishe kumlisha mpaka apo baadae atakapo tulia.
6. Mpatie maji ya kunywa au juise akimaliza kula mpe kidogo na kwa utaratibu mpaka atakapomaliza kiasi ulichompimia na akimaliza msafishe mdomoni ili kutoa mabaki yaliyobaki na pia mpanguse chakula ambacho kilianguka kwenye nguo.
7.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuchukua wajibu wa kuwalisha wagonjwa kwa sababu wagonjwa walio mahututi wengi ufariki mapema kwa kukosa chakula sio kwamba chakula hakipo hapana ila njia na elimu kuhusu kuwalisha wagonjwa hawana kwa hiyo natumaini tutaweza kuwatisha wagonjwa wetu baada ya kujua haya
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.
Soma Zaidi...Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kushuka
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi, ni faida ambazo upatikana kwa watu wanaodhani wameambukizwa na virus vya ukimwi na kuweza kujikinga.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi rangi isiyo ya kawaida kwenye mkojo, kawaida mkojo huwa na rangi ya kahawia Ila ukiona rangi zifuatazo Kuna shida kwenye mkojo.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wazee
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa watu waliopata ajali. Ajali ni tukio lisilotarajiwa ambalo kinaweza kumkuta mtu yeyote, tunapotoa huduma ya kwanza tnazingatia rangi ambazo huwakilisha jinsi watu walivyoumia.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria kwa kitaalamu huitwa vibrio cholera.
Soma Zaidi...