Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.
Njia za kuwalisha wagonjwa ambao hawawezi kujilisha mwenyewe.
1 Kwanza kabisa wagonjwa wengi wanashindwa kujilisha wenyewe kwa sababu mbalimbali labda hali zao haziwahusu kwa sababu ya aina ya ugonjwa kwa hiyo tunapaswa kuwalisha kwa sababu chakula na dawa vinaendana kwa hiyo Mgonjwa hasipokula hawezi kupona mapema kwa hiyo hata mgonjwa kama mgonjwa hawezi kujilisha anapaswa kulishwa kwa kufuata njia zifuatazo.
2. Mweke Mgonjwa kwenye hali ambayo ataweza kukaa vizuri na kula chakula na kama hajiwezi mwekee kitu cha kumfanya aweze kukaa vizuri na msafishe kinywa kabla ya kumpatia chakula kwa sababu kinywa kikiwa kisafi uongeza hamu ya kula.
3. Mwekee kitambaa kwenye kifua ili kuweza kumkinga na vyakula ambavyo vinaweza kudondokea nguo na pia leta sahani ya chakula karibu na mgonjwa na kumbuka kunawa mikono kabla ya kumlisha Mgonjwa na baada ya kumlisha Mgonjwa.
4. Kaa karibu na mgonjwa na pia ni vizuri kuwa na msaidizi wakati wa kumlisha Mgonjwa na chukua chakula cha mgonjwa na kiweke kwenye kijiko kuanzia kwenye mdomo wa kijiko na mlishe kidogo kidogo na wakati wa kumlisha subiri kwanza atafute ameze na ndipo umwekee chakula kingine .
5.Na pale Mgonjwa unapomlisha mruhusu kupumzika kidogo akimaliza kumeza na mlishe tena na akiwa amepumzika ongea naye taratibu na pia endelea kumlisha mpaka atakaposhiba na kama anahisi kichefuchefu mpumzishe kumlisha mpaka apo baadae atakapo tulia.
6. Mpatie maji ya kunywa au juise akimaliza kula mpe kidogo na kwa utaratibu mpaka atakapomaliza kiasi ulichompimia na akimaliza msafishe mdomoni ili kutoa mabaki yaliyobaki na pia mpanguse chakula ambacho kilianguka kwenye nguo.
7.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuchukua wajibu wa kuwalisha wagonjwa kwa sababu wagonjwa walio mahututi wengi ufariki mapema kwa kukosa chakula sio kwamba chakula hakipo hapana ila njia na elimu kuhusu kuwalisha wagonjwa hawana kwa hiyo natumaini tutaweza kuwatisha wagonjwa wetu baada ya kujua haya
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Posti hii inahusu zaidi dalili za kuwepo kwa kizungu Zungu,ni Dalili ambazo Uweza kujionyesha kwa mtu ambaye ameshawahi kupatwa na tatizo la kizungu Zungu au hajawahi kupata dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Kunywa soda ama dawa kwenyechupa zakioo ambayo ina ufa ama mipasuko ni hatari. Ni kwa sababu huwezijuwa huwenda kipande kikaingia mdomoni na umangimeza. Sasa nini ufanye endapo umeshakula?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Poshi hii inahusu madhara ya ulevi.Utegemezi wa pombe kwa kawaida humaanisha kuwa mtu anatumia kiasi kikubwa cha pombe na kuna masuala kuhusu kupoteza udhibiti.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa figo. Ni ugonjwa unaotokana pale figo linaposhindwa kufanya kazi, tuone mbinu za kufanya Ili kuepuka na tatizo hilo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Uvimbe au mashambulizi ya bacteria kwenye utando laini uliopo tumboni ambao kitaalamu hujulikana Kama peritonitis.
Soma Zaidi...