picha

Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Njia za kuwalisha wagonjwa ambao hawawezi kujilisha mwenyewe.

1 Kwanza kabisa wagonjwa wengi wanashindwa kujilisha wenyewe kwa sababu mbalimbali labda hali zao haziwahusu kwa sababu ya aina ya ugonjwa kwa hiyo tunapaswa kuwalisha kwa sababu chakula na dawa vinaendana kwa hiyo Mgonjwa hasipokula hawezi kupona mapema kwa hiyo hata mgonjwa kama mgonjwa hawezi kujilisha anapaswa kulishwa kwa kufuata njia zifuatazo.

 

2. Mweke Mgonjwa kwenye hali ambayo ataweza kukaa vizuri na kula chakula na kama hajiwezi mwekee kitu cha kumfanya aweze kukaa vizuri na msafishe kinywa kabla ya kumpatia chakula kwa sababu kinywa kikiwa kisafi uongeza hamu ya kula.

 

3. Mwekee kitambaa kwenye kifua ili kuweza kumkinga na vyakula ambavyo vinaweza kudondokea nguo na pia leta sahani ya chakula karibu na mgonjwa na kumbuka kunawa mikono kabla ya kumlisha Mgonjwa na baada ya kumlisha Mgonjwa.

 

4. Kaa karibu na mgonjwa na pia ni vizuri kuwa na msaidizi wakati wa kumlisha Mgonjwa  na chukua chakula cha mgonjwa na kiweke kwenye kijiko kuanzia kwenye mdomo wa kijiko na mlishe kidogo kidogo na wakati wa kumlisha subiri kwanza atafute ameze na ndipo umwekee chakula kingine .

 

5.Na pale Mgonjwa unapomlisha mruhusu kupumzika kidogo akimaliza kumeza na mlishe tena na akiwa amepumzika ongea naye taratibu na pia endelea kumlisha mpaka atakaposhiba na kama anahisi kichefuchefu mpumzishe kumlisha mpaka apo baadae atakapo tulia.

 

6. Mpatie maji ya kunywa au juise akimaliza kula mpe kidogo na kwa utaratibu mpaka atakapomaliza kiasi ulichompimia na akimaliza msafishe mdomoni ili kutoa mabaki yaliyobaki na pia mpanguse chakula ambacho kilianguka kwenye nguo.

 

7.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuchukua wajibu wa kuwalisha wagonjwa kwa sababu wagonjwa walio mahututi wengi ufariki mapema kwa kukosa chakula sio kwamba chakula hakipo hapana ila njia na elimu kuhusu kuwalisha wagonjwa hawana kwa hiyo natumaini tutaweza kuwatisha wagonjwa wetu baada ya kujua haya

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1688

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi

Soma Zaidi...
Kazi ya chanjo ya kifua kikuu

Posti hii inahusu kazi ya chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu huitwa BCG. Ni chanjo ambayo uzuia kifua kikuu na ukoma.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupumzika kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupumzika kiafya, kwa kawaida mwili na viungo vingine vya mwili uweza kufanya kazi zaidi pale mtu akiwa amepumzika.

Soma Zaidi...
Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa, Mgonjwa akiwa anaumwa na pia anakula chakula ni lazima asafishwe kinywa Ili kuweza kuepuka madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kinywani.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu protini na kazi zake mwilini

Tunahitaji kuwa na protini mwilini. Kuna baadhi ya makundi ya watu wanahitaji protini zaidi. Je unawajuwa hao ni kina nana?, na je unauwa kazi za protini mwilini na athari za upungufu wake? endelea na makala hii.

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.

Soma Zaidi...