picha

Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni

Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.

Njia za kuwalisha wagonjwa ambao hawawezi kujilisha mwenyewe.

1 Kwanza kabisa wagonjwa wengi wanashindwa kujilisha wenyewe kwa sababu mbalimbali labda hali zao haziwahusu kwa sababu ya aina ya ugonjwa kwa hiyo tunapaswa kuwalisha kwa sababu chakula na dawa vinaendana kwa hiyo Mgonjwa hasipokula hawezi kupona mapema kwa hiyo hata mgonjwa kama mgonjwa hawezi kujilisha anapaswa kulishwa kwa kufuata njia zifuatazo.

 

2. Mweke Mgonjwa kwenye hali ambayo ataweza kukaa vizuri na kula chakula na kama hajiwezi mwekee kitu cha kumfanya aweze kukaa vizuri na msafishe kinywa kabla ya kumpatia chakula kwa sababu kinywa kikiwa kisafi uongeza hamu ya kula.

 

3. Mwekee kitambaa kwenye kifua ili kuweza kumkinga na vyakula ambavyo vinaweza kudondokea nguo na pia leta sahani ya chakula karibu na mgonjwa na kumbuka kunawa mikono kabla ya kumlisha Mgonjwa na baada ya kumlisha Mgonjwa.

 

4. Kaa karibu na mgonjwa na pia ni vizuri kuwa na msaidizi wakati wa kumlisha Mgonjwa  na chukua chakula cha mgonjwa na kiweke kwenye kijiko kuanzia kwenye mdomo wa kijiko na mlishe kidogo kidogo na wakati wa kumlisha subiri kwanza atafute ameze na ndipo umwekee chakula kingine .

 

5.Na pale Mgonjwa unapomlisha mruhusu kupumzika kidogo akimaliza kumeza na mlishe tena na akiwa amepumzika ongea naye taratibu na pia endelea kumlisha mpaka atakaposhiba na kama anahisi kichefuchefu mpumzishe kumlisha mpaka apo baadae atakapo tulia.

 

6. Mpatie maji ya kunywa au juise akimaliza kula mpe kidogo na kwa utaratibu mpaka atakapomaliza kiasi ulichompimia na akimaliza msafishe mdomoni ili kutoa mabaki yaliyobaki na pia mpanguse chakula ambacho kilianguka kwenye nguo.

 

7.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuchukua wajibu wa kuwalisha wagonjwa kwa sababu wagonjwa walio mahututi wengi ufariki mapema kwa kukosa chakula sio kwamba chakula hakipo hapana ila njia na elimu kuhusu kuwalisha wagonjwa hawana kwa hiyo natumaini tutaweza kuwatisha wagonjwa wetu baada ya kujua haya

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1900

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Soma Zaidi...
Namna ya kumwosha Mgonjwa vidonda

Posti hii inahusu zaidi njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda, ni njia muhimu ambazo ni lazima kuzipitia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda.

Soma Zaidi...
Imani potofu juu ya chanjo.

Post hii inahusu zaidi Imani potofu juu ya chanjo kwa watoto na akina Mama, ni baadhi ya Imani waliyonayo watu juu ya chanjo.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Soma Zaidi...
Zijue sababu za kupoteza fahamu.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Soma Zaidi...