Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu
Huduma kwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi.
1. Huduma ya kwanza ni kuwapa ushauri na kupima mara kwa mara afya zao Ili kuona wadudu wamafikia hatua gani na kuweza kutoa ushauri na elimu kuhusu namna ya matumizi ya dawa. Kwa sababu kwa wale wanaotumia dawa kila siku na kufuata mashart maendeleo yao ni mazuri mno na idadi ya virus upungua ingawa hawawezi kuisha Bali ufubaa.
2. Kuhakikisha wamekingwa na magonjwa nyemelezi, yaani magonjwa ambayo utokea pale kinga ya mwili inaposhuka , magonjwa hayo ni pamoja na kifua kikuuu ambapo dawa za kifua kikuuu utolewa kwa wagonjwa wetu na pia kuwapatia watoto vyakula mbalimbali Ili kuweza kuhakikisha kuwa wanakuwa na lishe ya kutosha yaani vyakula vya lishe utolewa kwa watoto wenye chini ya miaka mitano Ili kuepuka tatizo la kuwa na utapia mlo.
3. Kuzuia maamikimbi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati Mama akiwa Mjamzito.
Akina Mama wote wanapokwenda clinic au kwenye mahudhulio ni lazima kwanza kabisa kupima ukimwi Ili kuweza kugundua kama Mama ana maambukizi kama anayo ushauri utolewa Ili kuweza kuepuka maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati akiwa Mjamzito, wakati wa kujifungua na wakati mtoto ananyonya kwa kipindi chote Mama anakuwa karibu na wahudumu wa afya Ili kuhakikisha mtoto hasipate maambukizi.
4. Kutoa elimu kwa watu ni kuwaahamasisha kupima virus vya ukimwi.
Kuna vikundi mbalimbali ambavyo vimeandaliwa Ili kuweza kutoa elimu kwa jamii Ili kuhakikisha watu wapime pia na kutumia kinga Ili kuweza kupunguza kuendelea kuwepo kwa ugonjwa wa ukimwi na pia kuwaanzishia dawa wale wote waliopata maambukizi ya ukimwi,kwa kufanya hivyo jamii itaweza kuishi kwa matumaini .
5. Pamoja na kuwepo kwa ugonjwa huu hatari watu wanapaswa kujua kuwa matumizi ya dawa ni muhimu na kwa kufuata mashart kwa sababu Kuna watu wengi wameugua ugonjwa huu lakini bado wanaoishi na wanaendelea vizuri kwa hiyo tusiwakatishe tamaaa wagonjwa tuwajali na tusiwatenge kwa sababu na wenyewe Wana haki ya kuishi kama watu wengine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini
Soma Zaidi...Viwango vitatu vya kuungua.
Posti hii inahusu zaidi viwango vitatu vya kuungua. Ili tuweze kujua mtu ameunguaje Kuna viwango vitatu vya kujua kiasi na namna mtu alivyoungua
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu Ugonjwa wa homa ya utu wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu homa ya uti wa mgongo, kwa kuwa ugonjwa huu mara nyingi uathiri sehemu za kwenye ubongo kuna madhara ambayo yanaweza kutokea endapo Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.
Soma Zaidi...Njia za kupunguza uzito na kitambi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa pamoja na kitambi
Soma Zaidi...Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini
Soma Zaidi...Utaratibu wa lishe kwa vijana
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana
Soma Zaidi...