picha

Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu

Huduma kwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi.

1. Huduma ya kwanza ni kuwapa ushauri na kupima mara kwa mara afya zao Ili kuona wadudu wamafikia hatua gani na kuweza kutoa ushauri na elimu kuhusu namna ya matumizi ya dawa. Kwa sababu kwa wale wanaotumia dawa kila siku na kufuata mashart maendeleo yao ni mazuri mno na idadi ya virus upungua ingawa hawawezi kuisha Bali ufubaa.

 

2. Kuhakikisha wamekingwa na magonjwa nyemelezi, yaani magonjwa ambayo utokea pale kinga ya mwili inaposhuka , magonjwa hayo ni pamoja na kifua kikuuu ambapo dawa za kifua kikuuu utolewa kwa wagonjwa wetu na pia kuwapatia watoto vyakula mbalimbali Ili kuweza kuhakikisha kuwa wanakuwa na lishe ya kutosha yaani vyakula vya lishe utolewa kwa watoto wenye chini ya miaka mitano Ili kuepuka tatizo la kuwa na utapia mlo.

 

3. Kuzuia maamikimbi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati Mama akiwa Mjamzito.

Akina Mama wote wanapokwenda clinic au kwenye mahudhulio ni lazima kwanza kabisa kupima ukimwi Ili kuweza kugundua kama Mama ana maambukizi kama anayo ushauri utolewa Ili kuweza kuepuka maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati akiwa Mjamzito, wakati wa kujifungua na wakati mtoto ananyonya kwa kipindi chote Mama anakuwa karibu na wahudumu wa afya Ili kuhakikisha mtoto hasipate maambukizi.

 

4. Kutoa elimu kwa watu ni kuwaahamasisha kupima virus vya ukimwi.

Kuna vikundi mbalimbali ambavyo vimeandaliwa Ili kuweza kutoa elimu kwa jamii Ili kuhakikisha watu wapime pia na kutumia kinga Ili kuweza kupunguza kuendelea kuwepo kwa ugonjwa wa ukimwi na pia kuwaanzishia dawa wale wote waliopata maambukizi ya ukimwi,kwa kufanya hivyo jamii itaweza kuishi kwa matumaini .

 

5. Pamoja na kuwepo kwa ugonjwa huu hatari watu wanapaswa kujua kuwa matumizi ya dawa ni muhimu na kwa kufuata mashart kwa sababu Kuna watu wengi wameugua ugonjwa huu lakini bado wanaoishi na wanaendelea vizuri kwa hiyo tusiwakatishe tamaaa wagonjwa tuwajali na tusiwatenge kwa sababu na wenyewe Wana haki ya kuishi kama watu wengine.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1385

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Mambo yanayoweza kudhoofisha kinga ya mwili

Kinga ya mwili inapodhoofu mwili unakuwa hatarini kupata maradhi. Je unayajuwa mambo yanayodhoofisha kinga ysbmeili?

Soma Zaidi...
Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa

Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na minyoo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Post hii inahusu zaidi tiba na huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Soma Zaidi...
Namna ya kuchoma chanjo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.

Soma Zaidi...
Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...