Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu
1. Huduma ya kwanza ni kuwapa ushauri na kupima mara kwa mara afya zao Ili kuona wadudu wamafikia hatua gani na kuweza kutoa ushauri na elimu kuhusu namna ya matumizi ya dawa. Kwa sababu kwa wale wanaotumia dawa kila siku na kufuata mashart maendeleo yao ni mazuri mno na idadi ya virus upungua ingawa hawawezi kuisha Bali ufubaa.
2. Kuhakikisha wamekingwa na magonjwa nyemelezi, yaani magonjwa ambayo utokea pale kinga ya mwili inaposhuka , magonjwa hayo ni pamoja na kifua kikuuu ambapo dawa za kifua kikuuu utolewa kwa wagonjwa wetu na pia kuwapatia watoto vyakula mbalimbali Ili kuweza kuhakikisha kuwa wanakuwa na lishe ya kutosha yaani vyakula vya lishe utolewa kwa watoto wenye chini ya miaka mitano Ili kuepuka tatizo la kuwa na utapia mlo.
3. Kuzuia maamikimbi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati Mama akiwa Mjamzito.
Akina Mama wote wanapokwenda clinic au kwenye mahudhulio ni lazima kwanza kabisa kupima ukimwi Ili kuweza kugundua kama Mama ana maambukizi kama anayo ushauri utolewa Ili kuweza kuepuka maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati akiwa Mjamzito, wakati wa kujifungua na wakati mtoto ananyonya kwa kipindi chote Mama anakuwa karibu na wahudumu wa afya Ili kuhakikisha mtoto hasipate maambukizi.
4. Kutoa elimu kwa watu ni kuwaahamasisha kupima virus vya ukimwi.
Kuna vikundi mbalimbali ambavyo vimeandaliwa Ili kuweza kutoa elimu kwa jamii Ili kuhakikisha watu wapime pia na kutumia kinga Ili kuweza kupunguza kuendelea kuwepo kwa ugonjwa wa ukimwi na pia kuwaanzishia dawa wale wote waliopata maambukizi ya ukimwi,kwa kufanya hivyo jamii itaweza kuishi kwa matumaini .
5. Pamoja na kuwepo kwa ugonjwa huu hatari watu wanapaswa kujua kuwa matumizi ya dawa ni muhimu na kwa kufuata mashart kwa sababu Kuna watu wengi wameugua ugonjwa huu lakini bado wanaoishi na wanaendelea vizuri kwa hiyo tusiwakatishe tamaaa wagonjwa tuwajali na tusiwatenge kwa sababu na wenyewe Wana haki ya kuishi kama watu wengine.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali ya maumivu ya mwili, Maumivu ya mwili utokea kwa aina mbalimbali kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukujulisha njia za kushusha presha iliyopanda.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujilinda na magonjwa ya meno
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa protini
Soma Zaidi...Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara
Soma Zaidi...