image

Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.

Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.

Namna ya kumwosha Mgonjwa.

1.Kwanza kabisa tunajua kuwa kama mgonjwa hajiwezi na hawezi kuamka mara nyingi usahaulika kwa upande wa usafi, nimeshuhudia mara nyingi wagonjwa wa hivi ukiwaosha hali zao zinabadilika na anapata nafuu na mgonjwa hasipooga kwa mwezi mzima anaweza hasipone haraka kwa hiyo tunapaswa kuwasafisha wagonjwa kama ifuatavyo.

 

2. Kwanza kabisa unaondoa mashuka ya juu ya mgonjwa na hakikisha hakuna Watu ambao hawahusiki na labda msaidizi tu na siku zote tumia maji ya moto na pia ondoa mito na bakiza kidogo ambayo inaweza kumfanya aweze ku kukaa vizuri.

 

3.Anza kutoa mashuka ya upande mmoja wakati mgonjwa umemlaza upande na mashuka  hayo umeyasogeza kwa upande ambao ameulalia na chukua maji na sabuni weka kwenye Dodoki na anza kusafisha upande mmoja na pia hakikisha chini kuna mpira ili kuepuka kulowanisha kitanda na suhuza sehemu hiyo kwa kitambaa   ambacho kimekamuliwa vizuri na hakikisha upande unatakata.

 

4.Mgeuze vizuri mgonjwa kwa upande wa pili na Isha upande huo vizuri kwa kuweka maji na sabuni kwenye Dodoki na sugua vizuri na baadae suuza kwa kitambaa kisafi kilichokamuliwa na ukimaliza upande wa pili, nenda kwenye sehemu za siri weka maji kwenye kutimbaa pangusa vizuri pia suuza nenda kwenye miguu na fanya hivyo hivyo ila kama mgonjwa anaweza kujifanyia usafi kwenye sehemu za siri mwache afanye mwenyewe.

 

5.Baada ya hapo mpake mafuta na ondoa mashuka machafu yaliyokuwepo wakati unamsafisha mvalishe nguo na pia mtandikie vizuri na mgonjwa akifanyiwa hivyo mara kwa mara kama alikuwa mahututi na hali yake itakuwa nzuri kabisa na wakati mgonjwa unamsafisha maji lazima yabadilishwe kutoka sehemu moja kwenda nyingine





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 832


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo Soma Zaidi...

Kuboresha afya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayosaidia kuboresha afya Soma Zaidi...

Msaada kwa wenye tonsils
Posti hii inahusu zaidi msaada kwa wenye tonsils, kwa wale wenye tonsils wanapaswa kufanya yafuatayo ili kuweza kupambana na ugonjwa huu. Soma Zaidi...

tamaa
33. Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari Soma Zaidi...

Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa
Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa. Soma Zaidi...

Faida za damu kwenye mwili
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa damu mwilini, Damu ni tisu pekee yenye majimaji ambayo hufanya kazi mbalimbali katika mwili wa binadamu. Soma Zaidi...

Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha Soma Zaidi...

Aina za vidonda
Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti. Soma Zaidi...

Mkojo wa kawaida
Posti hii inahusu zaidi mkojo wa kawaida kwa kila mwanadamu na unavyopaswakuwa, mkojo wa kawaida kwa binadamu huwa na sifa zifuatazo. Soma Zaidi...

Aina mbalimbali za maumivu ya mwili.
Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali ya maumivu ya mwili, Maumivu ya mwili utokea kwa aina mbalimbali kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka Soma Zaidi...