Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda

NJIA ZA KUKABILIANA NA PRESHA YA KUPANDA (HYPERTENSION)

1.Fanya mazoezi ya mwili na viungo walau kila siku kwa dakika kama 30 mpaka 60. si lazima uwe unakimbia ama mazoezi magumu ya kutoa jasho, hapana unaweza hata kuamua kutembea kwa miguu kwa mwendo mrefu kwa lisaa limoja na ikawa ni mazoezi tosha.

2.Kula vyakula vilivyo bora kwa afya, ambavyo vinasaidia kupunguza ama kuzuia presha. Kitaalamu mlo huu huitwa DASH yaani Diet Aproaches to Stop Hypertension. Vyakula hivi ni kama:

A.Matunda

B.Mboga za majani

C.Nafaka nzima

D.Samaki, karanga na korosho

E.Wacha kula vyakula vyenye mafuta mengi

3.Punguza ulaji wa chumvi sana. Kuzidi kwa ulaji wa vyakula vyenye chumvi nyingi kunaweza kusababisha presha ya kupanda. Kitaalamu ni kuwa ukila chumvi sana mwili unahitaji kupata maji mengi na hali hii itapelekea presha.

4.Punguza uzito uliozidi mwilini. Rafiki mkubwa wa presha ni kuzidi kwa uzito. Na tambuwa kuwa uzito wa mwili unatakiwa uendane na urefu wa mtu na si umri ama unene alio nao. hivyo tambua. Ili kuhakikisha kama uzito wako upo sawa unaeza kujipimia kiuno chako. Kikawaida wanaume wnatakiwa viuno vyao visizidi nchi 40 na wanawake viuno vyao visizidi nchi 35.

5.Punguza matumizi ya sigara ama wacha kabisa. Ndani ya sigara kuna kemikali za nicotine na nyinginezo. Nicotine ni rafiki sana na presha ya kupanda.

6.Punguza unywaji wa pombe ama wacha kabisa. Unywaji wa pombe sio hatari tu wa afya ya moyo lakini pia unaweza kuleta shida nyingine za kiafya kama saratani. Hakikisha kama ni mnywaji unapunguza unywaji ama unawacha kabisa itakuwa ni bora kwako.

7.Hakikisha huna misongo ya mawazo. Misongo ya mawazo inaweza kuwa ni adui mkubwa wa afya ya ubongo. Ni vyema kusamehe wanaokukosea na kuomba msamaha unapo kosea hali zote hizi mbili zitakusaidia kupunguza misongo ya mawazo. Jichanganye na watu na pemba kuwa mbali na fujo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1701

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dalili za unyanyasaji wa kimwili

Unyanyasaji wa kimwili. Unyanyasaji wa watoto kimwili hutokea wakati mtoto amejeruhiwa kimwili kimakusudi. Unyanyasaji wa kijinsia. Unyanyasaji wa watoto kingono ni shughuli yoyote ya kingono na mtoto, kama vile kumpapasa, kushikana mdomo na sehemu

Soma Zaidi...
Vyakula vya fati na mafuta

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya fati na mafuta

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fati na mafuta na kazi zake mwilini

Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii

Soma Zaidi...
Nini husababisha kizunguzungu?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo mbalimbali ambayo husababisha kizunguzungu.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoathiri Uponyaji was jeraha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kuadhiri Uponyaji wa jeraha.jeraha huleta maumivu makali sana, vilevile Uvimbe, kutoa usaha. Pia jeraha hutofautiana katika kupona kwa mtu mzima na Mtoto.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kazi za ini.

Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Uvimbe kwenye utandu laini uliopo tumboni (peritonitis)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Uvimbe au mashambulizi ya bacteria kwenye utando laini uliopo tumboni ambao kitaalamu hujulikana Kama peritonitis.

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...