picha

Namna ya kujikinga na kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu

Namna ya kujikinga na kifua kikuu.

1.Kwanza kabisa tunajua kua kifua kikuu kinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu tunapaswa kutumia njia ili kuepuka kusambaza ugonjwa huu ambao ni hatari kwenye jamii. Tuanaweza kujikinga kama ifuatavyo.

 

2.Tunapaswa kuwakinga kwanza watoto wakiwa wadogo kwa kuwapatia chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hii chanjo utolewa kwa watoto pindi wanapozaliwa na utolewa kwenye mkono wa jua wa mtoto na tunapaswa kuhakikisha kuwa kovu limetokea kama halijatokea chanjo urudiwa, kwa hiyo njia ya kwanza ni kwa kutumia chanjo kwa watoto.

 

3.Kufunika mdomo wakati wa kupiga chafya.

Wakati wa kupiga chafya tunapaswa kufunika mdomo kwa leso safi ili kuepuka mate kusambaa kwenye sehemu mbalimbali wakati wa kupiga chafya na kunawa mikono pindi unapogusa mate au majimaji yoyote kutoka kwenye pua au mdomo.

 

4.Kuvaa Maski au barakoa unapohisi kama kuna mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu au mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu anapaswa kuvaa Maski ili kuepuka hali ya kuwaambukiza wengine na kufanya ugonjwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5.Kuepuka kutupa vitambaa au vitu vyote vilivyohusiana na kupanga makamasi vinapaswa kutupwa kwenye sehemu ya takataka ili kuepukana na kusambaa kwa ugonjwa wa kifua kikuu.

 

6.Pia tukumbuke kuwa mgonjwa wa kifua kikuu kama hajaanza dawa ndipo anaweza kusambaza ugonjwa ila kama akianza dawa na akazitumia kwa mda wa wiki mbili hawezi kuambukiza kwa hiyo tuachane na tabia za kuwanyanyapaa na kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu , maana ugonjwa huu unatibika na una dawa na wengi wamepona

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3927

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu kazi za ini.

Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...
Vipi kuhusu kibofu kukaza sana na unapokula unahisi kama tumbo kujaa zaidi je hii nidall yamimba?

Dalili za mimba zinaweza kuwa tata sana kuzijua mpaka upate vipimo. Kwa mfano unaweza kupatwa na maumivu yakibofu. Je unadhani nayo ni dalili ya mimba?

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR

Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kizunguzungu

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kizungu Zungu ni tatizo ambalo utokea kwa watu mbalimbali na kwa sababu tofauti tofauti na pengine mtu akipata kizungu sehemu mbaya anaweza kusababisha majeraha au pengine kupata ulemavu

Soma Zaidi...