Namna ya kujikinga na kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu

Namna ya kujikinga na kifua kikuu.

1.Kwanza kabisa tunajua kua kifua kikuu kinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu tunapaswa kutumia njia ili kuepuka kusambaza ugonjwa huu ambao ni hatari kwenye jamii. Tuanaweza kujikinga kama ifuatavyo.

 

2.Tunapaswa kuwakinga kwanza watoto wakiwa wadogo kwa kuwapatia chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hii chanjo utolewa kwa watoto pindi wanapozaliwa na utolewa kwenye mkono wa jua wa mtoto na tunapaswa kuhakikisha kuwa kovu limetokea kama halijatokea chanjo urudiwa, kwa hiyo njia ya kwanza ni kwa kutumia chanjo kwa watoto.

 

3.Kufunika mdomo wakati wa kupiga chafya.

Wakati wa kupiga chafya tunapaswa kufunika mdomo kwa leso safi ili kuepuka mate kusambaa kwenye sehemu mbalimbali wakati wa kupiga chafya na kunawa mikono pindi unapogusa mate au majimaji yoyote kutoka kwenye pua au mdomo.

 

4.Kuvaa Maski au barakoa unapohisi kama kuna mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu au mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu anapaswa kuvaa Maski ili kuepuka hali ya kuwaambukiza wengine na kufanya ugonjwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5.Kuepuka kutupa vitambaa au vitu vyote vilivyohusiana na kupanga makamasi vinapaswa kutupwa kwenye sehemu ya takataka ili kuepukana na kusambaa kwa ugonjwa wa kifua kikuu.

 

6.Pia tukumbuke kuwa mgonjwa wa kifua kikuu kama hajaanza dawa ndipo anaweza kusambaza ugonjwa ila kama akianza dawa na akazitumia kwa mda wa wiki mbili hawezi kuambukiza kwa hiyo tuachane na tabia za kuwanyanyapaa na kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu , maana ugonjwa huu unatibika na una dawa na wengi wamepona

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2022/02/16/Wednesday - 09:44:45 am     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 1823

Post zifazofanana:-

Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuzuia Malaria kwa wajawazito. Soma Zaidi...

Dalili na Ishara za mawe kwenye figo
Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako. Soma Zaidi...

Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto. Soma Zaidi...

Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi. Soma Zaidi...

Zijue sababu za kupoteza fahamu.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

mambo ambayo utaulizwa mama mjamzito ukifika kituo cha afya unatakiwa utoe majibu sahihi.
Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa kipindupindu.
Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha'Kuhara'na'Upungufu wa maji mwilini. Soma Zaidi...

Mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe
Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana. Soma Zaidi...

Faida za Uzazi wa mpango
Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA. Soma Zaidi...

Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri
Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa. Soma Zaidi...

Zifahamu sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube, ni sababu ambazo ufanya mirija ya follapian tube kuziba. Soma Zaidi...

Huduma ya Kwanza kwa aliyeng'atwa na nyuki
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyuko Soma Zaidi...