picha

Namna ya kujikinga na kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu

Namna ya kujikinga na kifua kikuu.

1.Kwanza kabisa tunajua kua kifua kikuu kinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu tunapaswa kutumia njia ili kuepuka kusambaza ugonjwa huu ambao ni hatari kwenye jamii. Tuanaweza kujikinga kama ifuatavyo.

 

2.Tunapaswa kuwakinga kwanza watoto wakiwa wadogo kwa kuwapatia chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hii chanjo utolewa kwa watoto pindi wanapozaliwa na utolewa kwenye mkono wa jua wa mtoto na tunapaswa kuhakikisha kuwa kovu limetokea kama halijatokea chanjo urudiwa, kwa hiyo njia ya kwanza ni kwa kutumia chanjo kwa watoto.

 

3.Kufunika mdomo wakati wa kupiga chafya.

Wakati wa kupiga chafya tunapaswa kufunika mdomo kwa leso safi ili kuepuka mate kusambaa kwenye sehemu mbalimbali wakati wa kupiga chafya na kunawa mikono pindi unapogusa mate au majimaji yoyote kutoka kwenye pua au mdomo.

 

4.Kuvaa Maski au barakoa unapohisi kama kuna mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu au mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu anapaswa kuvaa Maski ili kuepuka hali ya kuwaambukiza wengine na kufanya ugonjwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5.Kuepuka kutupa vitambaa au vitu vyote vilivyohusiana na kupanga makamasi vinapaswa kutupwa kwenye sehemu ya takataka ili kuepukana na kusambaa kwa ugonjwa wa kifua kikuu.

 

6.Pia tukumbuke kuwa mgonjwa wa kifua kikuu kama hajaanza dawa ndipo anaweza kusambaza ugonjwa ila kama akianza dawa na akazitumia kwa mda wa wiki mbili hawezi kuambukiza kwa hiyo tuachane na tabia za kuwanyanyapaa na kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu , maana ugonjwa huu unatibika na una dawa na wengi wamepona

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4110

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Madhara ya kunywa pombe kiafya

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kunywa pombe kiafya, ni madhara ambayo utokea kwa watu wanaokumywa pombe kwa kupita kiasi kwa hiyo wanapaswa kupunguza kunywa pombe baada ya kujua madhara yake.

Soma Zaidi...
fahamu vitamini A na kazi zake

Je na wewe i katika wale ambaowanahitaji kujuwa kuhusu Vitamini A, kazi zake na vyakula vya vitamini A. post hii inakwenda kukujuza zaidi pamoja na historia ya vitamini A.

Soma Zaidi...
Sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini

Soma Zaidi...
Mbinu za kuondoa sumu mwilini.

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuondoa sumu mwilini, ni njia mbalimbali ambazo uweza kutumika ili kuondoa sumu mwilini.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU

Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu.

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda

Soma Zaidi...