Namna ya kujikinga na kifua kikuu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu

Namna ya kujikinga na kifua kikuu.

1.Kwanza kabisa tunajua kua kifua kikuu kinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu tunapaswa kutumia njia ili kuepuka kusambaza ugonjwa huu ambao ni hatari kwenye jamii. Tuanaweza kujikinga kama ifuatavyo.

 

2.Tunapaswa kuwakinga kwanza watoto wakiwa wadogo kwa kuwapatia chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hii chanjo utolewa kwa watoto pindi wanapozaliwa na utolewa kwenye mkono wa jua wa mtoto na tunapaswa kuhakikisha kuwa kovu limetokea kama halijatokea chanjo urudiwa, kwa hiyo njia ya kwanza ni kwa kutumia chanjo kwa watoto.

 

3.Kufunika mdomo wakati wa kupiga chafya.

Wakati wa kupiga chafya tunapaswa kufunika mdomo kwa leso safi ili kuepuka mate kusambaa kwenye sehemu mbalimbali wakati wa kupiga chafya na kunawa mikono pindi unapogusa mate au majimaji yoyote kutoka kwenye pua au mdomo.

 

4.Kuvaa Maski au barakoa unapohisi kama kuna mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu au mtu mwenye Maambukizi ya kifua kikuu anapaswa kuvaa Maski ili kuepuka hali ya kuwaambukiza wengine na kufanya ugonjwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5.Kuepuka kutupa vitambaa au vitu vyote vilivyohusiana na kupanga makamasi vinapaswa kutupwa kwenye sehemu ya takataka ili kuepukana na kusambaa kwa ugonjwa wa kifua kikuu.

 

6.Pia tukumbuke kuwa mgonjwa wa kifua kikuu kama hajaanza dawa ndipo anaweza kusambaza ugonjwa ila kama akianza dawa na akazitumia kwa mda wa wiki mbili hawezi kuambukiza kwa hiyo tuachane na tabia za kuwanyanyapaa na kuwatenga wagonjwa wa kifua kikuu , maana ugonjwa huu unatibika na una dawa na wengi wamepona

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 2871

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Namna ya kumsaidia mgonjwa aliye na Maambukizi kwenye milija na ovari

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa waliopata maambukizi kwenye milija na ovari, ni wagonjwa waliopata maambukizi kwenye milija na ovari.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza

Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Soma Zaidi...
Zijue kazi za ovari

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa ovari kwenye mwili wa mwanamke. ovari ni sehemu ambapo mayai ya mwanamke hutunza, kwa hiyo kila mwanamke huwa na ovari ambayo husaidia kutunza mayai.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu wa madini (anemia ya upungufu wa madini)

upungufu wa damu wa madini ya chuma ni aina ya kawaida ya upungufu wa damu hali ambayo damu haina chembe nyekundu za damu zenye afya. Seli nyekundu za damu hubeba oksijeni kwa tishu za mwili. Bila chuma cha kutosha, mwili wako hauwezi kutoa dutu ya k

Soma Zaidi...
Visababishi vya magonjwa.

Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula na madhara yake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya mwili.

Posti hii inahusu zaidi sababu ya kuwepo kwa maumivu ya mwili kwa sababu tunaweza kuhisi maumivu kwenye sehemu za mwili kwa sababu mbalimbali kama tutakavyoona hapo chini

Soma Zaidi...