Siku za kupata ujauzito

Siku za kupata ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata ujauzito

Download Post hii hapa

SIKU YA KUPATA UJAUZITO

 

Swala la kupata ujauzito limekuwa likikabiliwa na imani nyingia ambazo sio sahihi. Watu wengi wamekuwa wakipoteza muda na fedha kujaribu kutatua maswali yao. Leo nitakusaidia kutatua swali hili Je..! ni zipi dalili za mimba changa. Swali hili ni la msingi kwani kuna watu wengi wamekuwa wakichanganya dalili za ujauzito na shida nyingine za kiafya. Hapa nitajaribu kukufahamisha utofauti wa dalili hizi na nyingine ili upate kufahamu vyema.

 

Imani potofu kuhusu dalili za ujauzito:-1.Mimba inaingia siku yeyote ile. Hii sio sahihi kabisa mimba inasiku maalumu ambazo huweza kutungwa. Kitaalamu siku hizi zinafahamika kama fertile window2.Siku yya 14 ndio siku ambayo mimba hingia. Hii pia sio sahihi, kwani wanawake sio wote wanaingia siku 28, kuna wengine ni kati ya 21 mpaka 353.Unaweza kupima mimba kwa ktumia sukari, chumvi, mafuta, sabuni, delto. Hizi zote sio sahihi kabisa.

 

Ni siku gani mimba huingia.Mimba huweza kuingia siku ambayo yai litakutana na mbegu ya kiume kwenye mirija ya falopia kwenye tumbo la uzazi la mama. Yai la mwanamke kuzalishwa kwenye ovari. Mwanamke ana ovari mbili, moja upande wa kulia na nyingine kushoto. Hizi mbili hupeana zamu ya kutoa mayai. Yaani kama mwezi huu limetoa hili na nyingine itatoa mwezi ujao.

 

Tafiti zinaonyesha kuwa yai huweza kuanza kukomaa kuanzia siku ya 10 toka kupata hedhi mpaka siku ya 14. hii ni kwa wanawake wengi. Ila si wote. Kikawaida yai hutolewa (ovulation) kwa makadiria ya siku 12 mpaka 16 kabla ya kupata hedhi nyingine. Yaani unaweza kuhesabu kabla ya kuingia hedhi siku 12 nyuma, kisha toa siku 4 mnyuma ndani ya siku nne zizi ndizo yai hutolewa. siku hizi ndizo moja wapo yai hutolewa. Kwa mfano:--

 

1.Mwanamke mwenye mzunguko wa siku 21, sasa tunatoa siku 12 nyuma kabla ya kuingia hedhi (21 - 12 = 9) kisha toa nne nyuma (9-4=5) basi mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 5 na 9 katika siku zake.

 

2.Mwanamke mwenye mzunguruko wa siku 32: tunaanza kutoa siku 12 nyuma kabla ya kupata hedhi yake (32-12=20) tonatoa siku nne tena nyuma (20-4=16) kwa hiyo mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 16 mpaka 20.

 

4.Mwanamke mwenye siku 28: 28-12 = 16 kisha toa siku 4 nyuma 16 - 4 = 12. hivyo siiku ambazo yai hukomaa kwa mwenye siku 28 ni kati ya 12 mpaka 16.

 

Sasa baada ya kuzijua siku hizi ambazo yai hukomaa, inabidi ufahamu kuwa yai la mwanamke huweza kuishi kati ya masaa 12 mpaka 24 toka kukomaa (ovulation). kwa upande mwingine mbegu za kiume huisho kati ya siku 3 mpaka 5. hivyo ujauzito unaweza kutungwa kwa mbegu ambayo ilikuwepo toka siku tatu zilizopita.

 

NI IPI HASA SIKU AMBAYO NITAFUTE UJAUZITO?Kama ulipojifunza hapo juu kuwa zipo siku maalaumu ambazo yai hukomaa. Katika siku hizo mojawapo yai huletwa kwenye mirija ya falopia. Baada ya kukokotoa siku zako hapo juu sasa itakubidi kuongeza siku moja ama mbili nyuma. Hii ni kwa sababu makadirio ya siku hutofautiana. Na si lazima kkutafuta toto katika siku zote hizi. Unaweza kuruka kwa siku moja moja.

 

Jitahidi kufanya tendo la ndoa hasa katika siku hizo nne ulizozipata baada ya kukokotoa. Katika siku hizo jitahidi kufanya tendo siku ambayo itakuwa na sifa zifuatazo:-

 

1.Majimaji ya mwanamke ukeni yatakuwa ni mengi kuliko siku zilizopita. Mwanamke mwenyewe anaweza kujichunguza hali hii na kuigundua ila taabu. Anaweza kutumia kidole ama kitambaa safi kuchunguza uwepo wa majimaji haya katika ukeni kwake. Kumbuka hali hii isiambatane na shida nyingine za afya kama PID. Wakati mwingine inaweza kuwa ngumu kuchunguza hasa kwa wale wanaotumia uzazi wa mpango hasa hasa kwa kutumia vidonge vya homoni.

 

2.Joto la mwanamke litakuwa ni kubwa kuliko siku nyingine. Joto hili sio homa, na lisiambatane na sababu nyingine kama maumivu ya kichwa, ama kutokana na kulala sana, ama misongo ya mawazo. Kikawaida siku ambayo yai hutolewa joto la mwanamke linakuwa kubwa hivyo akishiriki siku hii ujauzito ni rahisi kuingia.

 

3.Siku ambayo mwanamke atakuwa na hamu sana ya kushiriki tendo. Wakato ambapo yai hutolewa kuna homoni huzalishwa kwa wingi. Homoni hizi zinaweza kusababisha mwanamke kutamani sana kushiriki tendo zaidi ya siku nyingine.

 

Pindi mwanamke atakapojigundua kuwa siku hii ameipata basi ni vyema kushiriki tendo ndani ya siku hii ama siku itakayofata haraka iwezekanavyo, maana yai la mwanamke linaweza kufa ndani ya muda mchach masaa 12 mpaka 24

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3121

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.
Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.

Soma Zaidi...
   Fahamu kuhusiana na kubalehe kwa msichana na mvulana.
Fahamu kuhusiana na kubalehe kwa msichana na mvulana.

Kubalehe ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana.

Soma Zaidi...
Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Soma Zaidi...
Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa
Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa

Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa

Soma Zaidi...
DALILI ZA TEZI DUME
DALILI ZA TEZI DUME

Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk

Soma Zaidi...
Njia huanza kufunguka mda gani kabla ya kujifungua
Njia huanza kufunguka mda gani kabla ya kujifungua

Mtoto huweza kuzaliwa ndani ya miezi 6 na unaweza kupona. Na huyu mdoe mtoto njiti. Na anaweza kuzliwa kwa njia ya kawaida. Hakuna ushahidi unaiinyesha kuwa njiti hukabiliwanamatatizo ya kitalima kwenye ukubwa wako.

Soma Zaidi...
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?

Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?

Soma Zaidi...
Zifahamu sifa za mtoto mchanga.
Zifahamu sifa za mtoto mchanga.

Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy

Soma Zaidi...
Namna za kujilinda na  fangasi  ukeni
Namna za kujilinda na fangasi ukeni

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.

Soma Zaidi...