Namna ya kumwosha Mgonjwa vidonda
Posti hii inahusu zaidi njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda, ni njia muhimu ambazo ni lazima kuzipitia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda.
Njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda.
1.Kwanza kabisa unapaswa kumtaarifu Mgonjwa kuhusu huduma unayotaka kumpatia, na pia hakikisha kubwa Mgonjwa amekubaliana na wewe na pia mweke sehemu ambayo utaweza kumwosha bila yeye juwa na wasiwasi.
2.Baada ya kumwandaa mgonjwa unapaswa kuandaa vifaa vyako ambayo ni pamoja na seti yenye vifaa vyote na pia unapaswa kuwa na beseni la maji yenye sabuni, chlorine,na maji mengine ya kawaida kwa ajili ya kuweka vifaa baada ya matumizi na pia unapaswa kuwa na mpira wa kuzuia maji maji kupita wakati wa usafi.
3.Baada ya kuandaa vifaa unaangalia faili la mgonjwa kama kuna dawa yoyote ambayo imeagizwa na daktari pia unapaswa kujiandaa dawa hiyo kama ipo , baada ya hapo unanawa mikono na kuvaa gloves na pia inafunguka seti yenye vifaa unatoa kifaa cha kuweka takataka wakati wa kusafisha.
4.Pamoja na hayo unachukua kufaa cha kuweka uchafu unajiweka karibu na inafunguka kidonda kama kimefungwa na unatoa nadaso ya juu na unaangalia kidonda kama kina usahaa au kama kuna mabadiliko yoyote ya rangi kwa hayapo unaanza kazi kama kuna usaha unatumia hydrogen peroxide na Uso kama hakuna usaha unatumia normal saline.
5. Ukiwa unaosha vidonda unaanza sehemu ya juu na kwenda sehemu ya ndani na unaanza sehemu safi kwenda chafu na ukimaliza unaweka dawa kama ipo na unafunga vizuri kidonda na baadae unamshukuru Mgonjwa kwa ushirikiano na unasaini kwa kuonyesha hali ya kidonda ulivyoikuta.
6. Na baadae inakusanya vifaa vyako unaviosha na kuviweka tayari kwa ajili ya kwenda kuua wadudu ambao wako kwenye vifaa ambavyo utumika. Katika kuosha vidonda tunapaswa kuwa makini ili kuepuka hali ya kupata magonjwa kutoka kwa wagonjwa wa vidonda.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini
Soma Zaidi...Mkojo wa kawaida
Posti hii inahusu zaidi mkojo wa kawaida kwa kila mwanadamu na unavyopaswakuwa, mkojo wa kawaida kwa binadamu huwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa aliyeungua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa aliyeungua
Soma Zaidi...Namna ya kuyatunza macho
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuyatunza macho
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU
Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu.
Soma Zaidi...Namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo, ni njia ya kuwasaidia wagonjwa waliopata madonda ya tumbo
Soma Zaidi...