image

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

11. Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi

Swala ya kupatwa kwa mwezi au jua ni sunnah iliyokokotezwa ambayo huswaliwa katika jamaa. Jua au mwezi unapopatwa Waislamu wanatakiwa waitane na kuswali swala ya Suunah ya kupatwa jua au mwezi kama alivyokuwa akifanya Mtume wa Allah:

 


Aisha (r.a) ameeleza kuwa jua lilitokea kupatwa wakati wa Mtume (s.a.w). Alisimama kuswali na alirefusha kisimamo (kiasi cha kumaliza kusoma Suratul-Baqara). Kisha alirukuu na kurefusha sana rukuu yake. Kisha aliinuka kutoka kwenye rukuu na akarefusha kisimamo lakini kilipungua kidogo kuliko kile cha kwanza. Kisha alirukuu tena na kurefusha rukuu lakini kupungua kidogo kuliko ile rukuu ya kw anza. Kisha alisujudu na kisha akasimama tena lakini kwa kitambo kilichopungua kidogo kuliko kisimamo kilichotangulia. Kisha alirukuu tena kw a kitam bo kilichopungua kidogo kuliko kile cha rukuu iliyotangulia. Kisha aliinuka kutoka kw enye rukuu na kurefusha kisimamo lakini kupungua kidogo kisimamo kilichotangulia. Kisha alirukuu tena na kurefusha rukuu yake lakini kupungua kidogo kuliko ile iliyotangulia. Kisha alis ujudu. Kisha ligeuka (aligeukia watu) na wakati huo jua lilikwisha kuwa jeupe na akawahutubia watu. Alimshukuru (alimhimidi) Allah na akasema: Jua na mwezi ni alama mbili za Allah (s.w). Havipatwi kutokana na kifo cha mtu yeyote, wala kutokana na kuzaliwa kwa mtu yeyote. Enyi Ummah wa Muhammad, hapana yeyote mwenye kupata ghadhabu kuliko Allah anavyomghadhibikia mja wake pindi anapozini. Enyi watu wa Muhammad, naapa kwa Allah kuwa kama mngelikuwa mnajua, mngelicheka kidogo na kulia sana ”. (Muslim)

 


Kutokana na Hadithi hii tunaona kuwa swala ya kupatwa jua na mwezi ina visimamo (au visomo) vinne, rukuu nne na sijda nne. Visimamo na rukuu hutofautiana urefu kama ilivyo oneshwa katika Hadithi.Imamu Shafii na Maimamu wengine wanashikilia kuwa swala ya kupatwa jua na mwezi haina budi kuswaliwa katika muundo huu ulioelezwa katika hadithi hii. Lakini Imamu Abu Daud, anashikilia kuwa swala ya kupatwa kwa jua na mwezi iswaliwe kama swala ya kawaida kwani kutokana na hadithi hiyo Mtume (s.a.w) aliwahi pia kuswali swala hiyo kwa kufuatia muundo wa swala za kawaida.

 

Kwa ujumla wanachuoni wengi wanasisisitiza kuwa pamoja na kwamba swala ya kupatwa kwa jua na mwezi inaweza kuswaliwa kwa kufuata muundo wa kawaida wa swala, ni vizuri zaidi kama swala hiyo itaswaliwa kwa kufuata muundo ulioelezwa katika Hadithi hii wa kuwa na visimamo (visomo) vinne, rukuu nne na sijda nne.

 


Lengo la swala hii ni kumkumbuka Allah(s.w) kwa kuzingatia alama zake. Hivyo ni vyema Imamu baada ya swala awawaidhi Waislamu kuwakumbusha wajibu wao kwa Allah(s.w) na kuwakumbusha marejeo yao ya akhera. Hivyo swala ya kupatwa jua (Swalatul-Kusuf) au swala ya kupatwa mwezi (swalatul-Khusuf) hufuatiwa na khutuba mbili kama ilivyo katika khutuba ya Idd. Katika swala hizi Imamu atasoma kwa sauti.

 



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/15/Monday - 11:14:50 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 641


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir Soma Zaidi...

Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Msisitizo juu ya kutoa zaka na sadaka
Soma Zaidi...

Umuhimu wa funga ya ramadhan
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafungu ya mirathi katika uislamu
Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1. Soma Zaidi...

Nini maana ya twahara katika uislamu
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo Soma Zaidi...

Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu? Soma Zaidi...

.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu
3. Soma Zaidi...

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya
Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Soma Zaidi...