Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.


image


Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf


11. Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi

Swala ya kupatwa kwa mwezi au jua ni sunnah iliyokokotezwa ambayo huswaliwa katika jamaa. Jua au mwezi unapopatwa Waislamu wanatakiwa waitane na kuswali swala ya Suunah ya kupatwa jua au mwezi kama alivyokuwa akifanya Mtume wa Allah:

 


Aisha (r.a) ameeleza kuwa jua lilitokea kupatwa wakati wa Mtume (s.a.w). Alisimama kuswali na alirefusha kisimamo (kiasi cha kumaliza kusoma Suratul-Baqara). Kisha alirukuu na kurefusha sana rukuu yake. Kisha aliinuka kutoka kwenye rukuu na akarefusha kisimamo lakini kilipungua kidogo kuliko kile cha kwanza. Kisha alirukuu tena na kurefusha rukuu lakini kupungua kidogo kuliko ile rukuu ya kw anza. Kisha alisujudu na kisha akasimama tena lakini kwa kitambo kilichopungua kidogo kuliko kisimamo kilichotangulia. Kisha alirukuu tena kw a kitam bo kilichopungua kidogo kuliko kile cha rukuu iliyotangulia. Kisha aliinuka kutoka kw enye rukuu na kurefusha kisimamo lakini kupungua kidogo kisimamo kilichotangulia. Kisha alirukuu tena na kurefusha rukuu yake lakini kupungua kidogo kuliko ile iliyotangulia. Kisha alis ujudu. Kisha ligeuka (aligeukia watu) na wakati huo jua lilikwisha kuwa jeupe na akawahutubia watu. Alimshukuru (alimhimidi) Allah na akasema: Jua na mwezi ni alama mbili za Allah (s.w). Havipatwi kutokana na kifo cha mtu yeyote, wala kutokana na kuzaliwa kwa mtu yeyote. Enyi Ummah wa Muhammad, hapana yeyote mwenye kupata ghadhabu kuliko Allah anavyomghadhibikia mja wake pindi anapozini. Enyi watu wa Muhammad, naapa kwa Allah kuwa kama mngelikuwa mnajua, mngelicheka kidogo na kulia sana ”. (Muslim)

 


Kutokana na Hadithi hii tunaona kuwa swala ya kupatwa jua na mwezi ina visimamo (au visomo) vinne, rukuu nne na sijda nne. Visimamo na rukuu hutofautiana urefu kama ilivyo oneshwa katika Hadithi.Imamu Shafii na Maimamu wengine wanashikilia kuwa swala ya kupatwa jua na mwezi haina budi kuswaliwa katika muundo huu ulioelezwa katika hadithi hii. Lakini Imamu Abu Daud, anashikilia kuwa swala ya kupatwa kwa jua na mwezi iswaliwe kama swala ya kawaida kwani kutokana na hadithi hiyo Mtume (s.a.w) aliwahi pia kuswali swala hiyo kwa kufuatia muundo wa swala za kawaida.

 

Kwa ujumla wanachuoni wengi wanasisisitiza kuwa pamoja na kwamba swala ya kupatwa kwa jua na mwezi inaweza kuswaliwa kwa kufuata muundo wa kawaida wa swala, ni vizuri zaidi kama swala hiyo itaswaliwa kwa kufuata muundo ulioelezwa katika Hadithi hii wa kuwa na visimamo (visomo) vinne, rukuu nne na sijda nne.

 


Lengo la swala hii ni kumkumbuka Allah(s.w) kwa kuzingatia alama zake. Hivyo ni vyema Imamu baada ya swala awawaidhi Waislamu kuwakumbusha wajibu wao kwa Allah(s.w) na kuwakumbusha marejeo yao ya akhera. Hivyo swala ya kupatwa jua (Swalatul-Kusuf) au swala ya kupatwa mwezi (swalatul-Khusuf) hufuatiwa na khutuba mbili kama ilivyo katika khutuba ya Idd. Katika swala hizi Imamu atasoma kwa sauti.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala. Soma Zaidi...

image Ufafanuzi kuhudu mgogoro wa mwezi ni muda gani mtu aanze kufunga.
Je inapoonekana sehemu moja tufunge duania nzima ama tufunge kwa kuangalia mwandamo katika maenro tunayoishi. Soma Zaidi...

image Fadhila za usiku waalylat al qadir
Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000. Soma Zaidi...

image Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...

image Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali. Soma Zaidi...

image Ni nini maana ya swala
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya haja
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake. Soma Zaidi...

image Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

image Sifa za imamu wa swala ya jamaa
Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii. Soma Zaidi...