Haki za mwanamke katika Uislamu
Katika kuhakikisha kuwa mwanamke anapata haki zake Uislam umesisitiza mambo ya msingi yafuatayo:
Kwanza, Uislamu umeweka wazi kuwa uongozi aliopewa mwanamume juu ya familia yake asije akautumia vibaya na akawageuza watu wa familia yake kuwa "Watumwa" naye akawa "Bwana". Bali anatarajiwa kuiongoza familia na kufikia lengo tarajiwa.
Pili, Uislamu umesisitiza kuwa wanawake wapewe fursa zote zitakazo wawezesha kuendeleza vipawa vyao katika kiwango cha juu ili kuinua na kuiendeleza jamii, ila tu mipaka ya Uislamu ichungwe.
Tatu, Uislamu unasisitiza kumuendeleza mwanamke kiwango cha hali ya juu na kumbakisha katika hadhi ya mwanamke. Kuwa mwanamume au kumtayarisha kwa majukumu ya wanaume si katika haki zake wala Si jambo litakalo mletea maendeleo yeye binafsi na jamii nzima kwa ujumla.
Kwa kuzingatia vipengele hivi vya msingi Uislamu unampa mwanamke haki katika nyanja zote za kijamii kama ifuatavyo:
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi
Soma Zaidi...Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.
Soma Zaidi...