image

Fadhila za usiku waalylat al qadir

Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000.

Umuhimu wa usiku wa Lailatul Qadr

Umuhimu wa Usiku wa Lailatul Qadr umebainishwa wazi katika Qur-an kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

 

Katika (usiku) huu hubainishwa kila jambo la hikima. Ndiyo hukumu itokayo kwetu; kwa hakika sisi ni w aletao (Mitume ili w awaongoe watu). (44:4-5).
Katika Suratul-Qadr tunasoma

 

“Hakika tumeiteremsha (Qur-an) katika Lailatul-Qadr (Usiku wenye heshima kubwa). Na ni jambo gani litakalo kujulisha ni nini huo usiku wa Lailatul-Qadr? Huo usiku (wa Lailatul-Qadr) ni bora kuliko miezi elfu. Huteremka Malaika na Roho (Jibril) katika usiku huo kwa idhini ya Mola w ao kw a kila jambo. Ni amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajir. ” (9 7:1 -5).

 


Tunajifunza katika aya hizi kuwa Allah (s.w) ameutukuza Usiku mmoja katika mwezi wa Ramadhani ili iwe kumbukumbu kwa Waumini wa umati huu wa Mtume Muhammad (s.a.w), ya kuletewa mwongozo pekee wa maisha yao kutoka kwa Mola wao. Mwongozo ambao huwa ni ponyo na rehma kwa Waumini na ambao hauwazidishii makafiri ila khasara:

 

 

 

Na tumeteremsha katika Qur-an (hayo mafundisho yake) ambayo ni ponyo (poza la nyoyo) na rehema kwa wanaoamini. Wala hayawazidishii (mafundisho haya) madhalimu ila khasara ” (1 7:82).

 


Tunafahamishwa katika aya zilizomo katika Surat Qadr kuwa Allah (s.w) ameutukuza usiku huu zaidi ya miezi elfu moja au miaka 83 na miezi 4. Ina maana kuwa muumini akifanya amali njema katika usiku huu, thamani yake katika malipo na katika uwezo wa kumfikisha mja kwenye lengo la maisha yake itakuwa ni kubwa zaidi ya thamani ya amali hiyo iliyofanywa kwa miezi elfu moja. Umuhimu wa lailatul-Qadr pia unabainika katika Hadith ifuatayo:

 


Ames imulia Abu Hurairah (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani akiwa na Imani na akiwa na tegemeo la kupata malipo kutoka kwa Allah (s.w), basi dhambi zake zote zilizopita zitasamehewa. Na mwenye kusimama kwa swala katika usiku wa Qadr akiwa na imani na mategemeo ya kupata malipo kutoka kwa Allah, basi dhambi zake zote zilizotangulia zitasamehewa.” (Bukhari).

 


Ili kupata malipo na baraka ya usiku huu wa Lailatul-Qadr, Mtume (s.a.w) ametuhimiza sana kuupania huo usiku kwa kuzidisha ibada za usiku kwa kuswali, kusoma Qur-an, kumkumbuka Allah (s.w) kwa wingi na kuomba maghfira.

 


Aysha (r.a) ameeleza: Niliuliza: “Ewe Mtume wa Allah! Nifahamishe niseme nini nitakapoudiriki usiku uliobarikiwa ?” Akasema (Mtume s.a.w) sema; “Ee, Allah! Wewe ni Msamehevu Unayependa kusamehe, Basi (Nakuomba) Unisamehe”. (Ahmad, Ibn Majah, Tirmidh).

 


Usiku wa Lailatul-Qadr ni usiku uliofichwa na Allah (s.w). Yaani haijulikani siku maalum ya mwezi wa Ramadhani ambamo usiku huu hutokea. Kwa jitihada zetu tunaona hekima ya kufichwa usiku huu ni ili Waislamu wasiwe wavivu wa kufanya ibada katika mausiku yote ya mwezi wa Ramadhani na badala yake wakautegea usiku huo mmoja tu. Hata hivyo, kutokana na Hadith sahihi tunajifunza kuwa usiku huu hutegemewa zaidi kutokea katika kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani. Mtume (s.a.w) aliutafuta usiku huo katika kumi la mwisho kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:

 

Abu Sayed al-Khudr(r.a) am eeleza kuw a Mtum e (s.a.w) alikaa itiqaf katika siku kumi za kwanza za Ramadhani. Kisha akakaa tena itiqaf katika kumi la katikati la Ramadhani. Kisha aliinua kichwa chake akasema: “Hakika nilikaa Itiqaf katika siku kumi za mwanzo, niliutafuta usiku huu (wa Qadr). Kisha nilijiwa na kufahamishwa kuwa usiku huu hupatikana katika siku kumi za mw isho. Yule atakayekaa Itiqaf na mimi, basi na akae katika kumi la mwisho, kwa sababu nilionyeshwa kutokea kwake katika siku hizo lakini nilifanywa kusahau (siku gani hasa), japo niliuona mimi mwenyewe nikiwa (kwenye ndoto) nikiwa ninasujudu kwenye maji na matope. Basi utafuteni usiku huu katika siku kumi za mwisho na hasa mausiku ya witr ...” (Bukhari na Muslim).

 


Hadith hii inatufahamisha kuwa mtume (s.a.w) alibainishiwa u siku huo kuwa katika kumi la mwisho la Ramadhani na akakokoteza watu wakae Itiqaf katika kumi hilo.Pia kutokana na Hadith hii mausiku yenye mategemeo zaidi katika hili kumi la mwisho ni zile za witr - usiku wa 21, 23, 25, 27, na 29. Katika Hadith iliyosimuliwa na Zirri bin Hubaish (r.a) na kupokelewa na Muslim, usiku wa 27 umetiliwa mkazo zaidi. Lakini hasa alichosisitiza Mtume (s.a.w) sio kutegemea usiku mmoja tu kama vile usiku wa 27, bali kujizatiti kwa kuzidisha ibada za usiku kwa kuswali, kusoma Qur-an, kumkumbuka Allah kwa wingi, kuomba maghfira na dua mbali mbali kwa mausiku yote ya kumi la mwisho la Ramadhani.Hivi ndivyo alivyofanya Mtume (s.a.w) kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:

 


Aysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akijizatiti sana kufanya ibada katika mausiku ya kumi ya mwisho, kuliko ilivyokuwa kawaida yake katika wakati mwingine. (Muslim).

 


Aysha (r.a) ameeleza kuwa wakati usiku wa kumi la mwisho ulipoingia, Mtume (s.a.w) alikuwa akijifunga kibwebwe akikesha katika Ibada na akiamsha familia yake kwa swala. (Bukhari na Muslim).

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1131


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala. Soma Zaidi...

umuhimu wa swala katika uislamu
Soma Zaidi...

Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu
Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi
Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu. Soma Zaidi...

Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala. Soma Zaidi...

Swala ya jamaa na mnamna ya kuswali swala ya jamaa, nyumbni, msikitini na kwa wanawake
Soma Zaidi...

Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...

Waislamu wanaolazimika kufunga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni zipi funga za suna, na faida na fadhila zake pamoja na wakati wake wa kufunga
Soma Zaidi...

Ujuwe utaratibu mzima wa funga na kutekeleza ibada ya Swaumu
Soma Zaidi...

Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea
Soma Zaidi...

Shahada nguzo ya kwanza ya uislamu, sifa zake na umuhimu wake.
Soma Zaidi...