Zijuwe nguzo 17 za swala.

Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.

Nguzo za Swala

Utekelezaji wa nguzo za swala ni hatua ya pili katika harakati za kusimamisha Swala. Baada ya kutekeleza kwa ukamilifu sharti za swala, Muislamu huwa tayari kumkabili Mola wake na kuzungumza naye katika swala.Vipi tuzungumze na Mola wetu katika swala, tumeonyeshwa kinadharia na matendo na Mtume Muhammad (s.a.w) ambaye ametuusia: “Swalini kama mlivyoniona mimi nikiswali”. Tunafahamu Mtume (s.a.w) aliswali vipi kwa kurejea Hadith zifuatazo:

 


Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akianza swala kwa takbira na kusoma Qur-an - Alhamdullilaahi Rabil-alamiina (Suratul Fatiha). Alipoinama (kurukuu) hakuwa anaweka kichwa chake juu wala hakuwa anakiinamisha sana bali alikuwa akikiweka katikati ya hali hizo mbili, na alipoinuka kutoka kwenye rukuu hakuwa anakwenda

 

kwenye sijda mpaka asimame kwanza wima na alipoinua kichwa chake kutoka kwenye sijda, hakusujudu mpaka baada ya kukaa wima; na alikuwa akisoma tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, na (katika hiyo tahiyyatu) alikuwa anakaa kwa kuulaza mguu wa kushoto na kuusimamisha wima mguu wa kulia. Alikataza kukaa mkao wa shetani (kunyoosha miguu) na kunyoosha mikono kama mnyama, na alikuwa akifunga (akimaliza) Swala kwa Salaam”. (Muslim)

 


Abu Humid Sayid(r.a) aliwaambia Masw ahaba wa Mtume (s.a.w) alitaka kuwakumbusha jinsi Mtume wa Mwenyezi alivyokuwa akisw ali. Alisema (Abu Humaid) kwamba wakati alipokuwa akisoma takbira Mtume alikuwa akiweka mikono yake mkabala na mabega yake na alipokuw a akirukuu, aliweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kuupinda mgongo wake; wakati alipoinua kichwa (alipoinuka) alijinyoosha (alinyoosha shingo yake) wima mpaka kila kiungo kinarudia nafasi yake; wakati alipokwenda Sijda (aliposujudu) mikono yake ilikuwa kati na kati (haikuwa mbali sana wala haikuwa pamoja), na vidole vyake (ncha za vidole vyake) vya miguu vilielekea (alivielekeza) Ka ’aba, alipokaa baada ya rakaa mbili alikuwa akiukalia mguu wake wa kushoto na kusimamisha mguu wa kulia. Wakati alipokaa katika rakaa ya mwisho aliutanguliza (hakuukalia) mguu w a kushoto na kuusimamisha w a kulia, alikaa kwa makalio. (Bukhari).

 


Abu Hamaid Sayid aliwaambia Maswahaba kumi wa Mtume(s.a.w), kwamba yeye anajua vizuri zaidi jinsi Mtume (s.a.w) alivyokuwa akiswali. Alisema (Abu Hamid) kwamba: Wakati Mtume (s.a.w) aliposimama kuswali, aliinua mikono yake juu mpaka ilipokuwa mkabala na mabega yake. Halafu alisoma takbira na baadaye alisoma Qur-an. Halafu alisoma takbira na kuinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake.Halafu aliinama (alirukuu) akiweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kujiweka mwenyewe sawa sawa (bila ya kuinamisha kichwa wala kukiinua juu). Baadaye aliinua kichwa chake (aliinuka kutoka rukuu) na kusema: “Mwenyezi Mungu anamsikia (humsikia) yule anayemsifu ”. Halafu aliinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake akiwa wima sawa sawa na kusema:“Mwenyezi Mungu ni mkubwa ”. Baadaye alikw enda (chini alikw enda sijda) akiw eka mikono yake mbali na usawa wake na mwili na kupinda vidole vyake vya miguu. Aliinua kichwa chake na aliukunja mguu wake wa kushoto na kuukalia. Alikaa sawasawa (wima) mpaka kila kiungo cha mwili kimerudia mahali pake, na alikwenda tena sijda na kusema:“Mwenyezi Mungu ni mkubwa ”. Aliinuka (alijiinua) kutoka Sijda na kukalia mguu wake wa kushoto. Alikaa sawa sawa mpaka kila kiungo cha mwili kikarudia nafasi yake (mahali pake). Baadaye alisimama juu (wima) na kufanya yote kama alivyofanya

 

katika rakaa ya kwanza. Mw is ho wa rakaa hizi mbili alisimama na kusoma takbira.ya kwanza na aliinua mikono yake hadi ikawa mkabala na mabega yake kama alivyosoma takbira ya kufungulia swala na baadaye alifanya hivyo hivyo katika sehemu ya swala iliyobakia mpaka kufikia Sijda ambamo mlikuwa na (Taslimu). Aliondoa mguu wake wa kushoto (hakuukalia). Alikaa kwa makalio zaidi upande wa kushoto (alikalia mfupa wa kalio la upande wa kushoto) baadaye alitoa Salaam (Taslim). Maswahaba wote `walikubali kuwa Abu Hamid amesema ukweli. (Abu Daud).

 


Hadithi hizi zinatufahamisha kuwa swala ya Mtume(s.a.w) ambaye ametuamrisha tumuigize ina vipengele vilivyogawanyika katika mafungu makubwa mawili. Nguzo za Swala na Sunnah za Swala.

 


Nguzo za Swala

 


Nguzo za swala ni vile vipengele vya swala ambavyo lazima mtu avitekeleze ndio swala yake iweze kukamilika. Nguzo moja tu ikikosekana swala haisihi (haikamiliki). Hivyo ili mwenye kuswali awe na matarajio ya kupata matunda ya Swala hana budi kutekeleza nguzo zake zote kwa ukamilifu. Zifuatazo ni nguzo za Swala:

 


1. Nia - dhamira moyoni.
2. Takbira ya kuhirimia (au Takbira ya kufungulia Swala).
3. Kusoma suratul-Fatiha.
4.Kurukuu.
5.Kujituliza katika rukuu.
6.Kuitidali (kusimama kutoka katika rukuu).
7.Kujituliza katika itidali.
8.Kusujudu.
9.Kujituliza katika sijda.
10.Kukaa kati ya sijda mbili.
11.Kujituliza katika kikao cha kati ya sijda mbili.
12Kusujudu mara ya pili.
13.Kujituliza katika sijda ya pili.
14.Kukaa Tahiyyatu.
15.Kusoma Tahiyyatu.
16.Kumswalia na kumtakia rehema Mtume (s.a.w) na Waislamu.
17.Kutoa Salaam.
18.Kuswali kwa kufuata utaratibu huu (1 - 17).

 


hizi za swala tunaweza kuzigawanya kwenye makundi
(a)Nia.
(b)Nguzo za matamshi (visomo)
(c)Nguzo za vitendo.
(d)Kufuata utaratibu.

 


Katika nguzo 18, nguzo za matamshi ni hizi tano zifuatazo:
(i)Takbira ya kuhirimia swala.
(ii)Ku soma suratul-Fatiha (Al-hamdu).
(iii)Kusoma Tahiyyatu.
(iv)Kumswalia Mtume.
(v)Kutoa Salaam.

 


Nguzo zote zilizobakia, ukiacha nia na kufuata utaratibu ni nguzo za vitendo.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/14/Sunday - 01:26:30 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1180


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu. Soma Zaidi...

Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

Zijuwe sunnha 9 za swala
Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki. Soma Zaidi...

Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkuchunga nyakatibza swala tano. Soma Zaidi...

Al-Arba'uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 1: Nia
huu ni mwanzo wa kitabu hiki cha Matn arbaina Naway Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Mambo yanayoharibu swala yaani yanayobatilisha swala.
Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe. Soma Zaidi...

Faida za kuswali swala za sunnah
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah. Soma Zaidi...

Al-Arba uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 7: Nasaha katika dini
Post hii itakufundisha umuhimu wa nasaha katika dini Soma Zaidi...

Zijuwe nguzo 17 za swala.
Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala. Soma Zaidi...

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...