Je manii ni twahara au najisi?

Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis

Wanazuoni wamehitilafiana juu ya suala hili kwa kauli mbili:

 

Kauli ya kwanza:

 

Inasema kwamba manii ni najsi. Kauli hii ameisema Abu Haniyfah na Maalik, nayo ni riwaya iliyopokelewa toka kwa Ahmad. Wamelitolea dalili hilo kwa Hadiyth ya 'Aaishah alipoulizwa kuhusu manii yaliyoingia kwenye nguo akasema:  "Nilikuwa nikiyaosha kwenye nguo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kisha anatoka moja kwa moja kwenda kuswali huku athari ya doa la maji  ikiwa katika nguo yake". [Imepasishwa na Al-Bukhaariy (230) na Muslim (289)].

Na kuosha hakuwi ila kwa kitu najsi.

 

 

Kauli ya pili:

 

Wenye kauli hii wamesema kuwa manii ni twahara. Kati ya waliolisema hilo ni Ash-Shaafi'i na Daawuud. Hii ni riwaya Swahiyh zaidi kati ya riwaya mbili zilizopokelewa toka kwa Ahmad. Wamelitolea dalili hilo kwa Hadiyth ya 'Aaishah kuhusu manii, aliposema: "Nilikuwa nikiyakwangua kuyatoa kweye nguo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)”. [Hadiyth Swahiyh: Muslim (288)].

 

Na kwa Hadiyth yake nyingine kwamba mgeni alishukia kwa 'Aaishah na akawa anaiosha nguo yake. 'Aaishah  akamwambia: "Ilikuwa inakutosha tu ikiwa utayaona, uoshe mahala pake, na ikiwa hukuyaona, unyunyizie maji kuzungukia hapo. Na bila shaka umeniona nikiyakwangua kwa umakini kwenye nguo ya Nabiy wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na yeye akaiswalia". [Hadiyth Swahiyh: Muslim (288)].

 

Na kutosheka kuyakwangua, kunaonyesha kuwa manii ni twahara.

 

Wenye kusema kuwa manii ni najsi, wamejibu kuwa kukwangua  hakuonyeshi kuwa manii ni twahara, bali kunaonyesha namna ya kuyatwaharisha kama vinavyotwaharishwa viatu kwa kuvipangusa katika mchanga.

 

Hili linajibiwa  kwa kusema kuwa 'Aaishah  alipoyakwangua manii mara moja na kuyaosha mara nyingine, hilo halihukumii kuwa ni najsi, kwani nguo inaoshwa kwa kuingia makamasi, mate au uchafu. Na hivi ndivyo walivyosema baadhi ya Maswahaba kama vile Sa'ad bin Abiy Waqqaasw, Ibn 'Abbaas na wengineo. Wamesema:

"Manii ni kama makamasi na mate, jisafishe uyaondoshe japokuwa kwa kijiti." [Majmuu Al-Fataawaa (21/605)].

 

Na kwa hili, inadhihiri kuwa kitendo cha 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa), kinaingia katika mlango wa kujichagulia namna ya kusafisha. [Sharhu Muslim].

 

Hukmu ya kuwa manii ni twahara inapata nguvu tunapojua kwamba Maswahaba walikuwa wakiota wakati wa enzi ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na manii hayo yalikuwa yakiingia katika miili na nguo za baadhi yao. Na lau kama yangelikuwa ni najsi, basi ingelikuwa ni lazima kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) awaamrishe wayasafishe kama alivyowaamrisha wastanji. Na kwa kuwa hakuna yeyote aliyelinukuu hili, inajulikana kwa yakini kuwa kuyaondosha hakukuwa ni jambo la lazima.  Allaah Ndiye Ajuaye zaidi. [Majmuu Al-Fataawaa (21/604)].

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1562

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Madhara ya riba kwenye jamii

Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?

Soma Zaidi...
Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake

Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Zoezi la nne mada ya fiqh.

Maswali mbalimbali kuhusu fiqh.

Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii

Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?

Soma Zaidi...