Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu

Umuhimu na Hekima ya Sheria ya Mirathi ya Kiislamu

1. Mrithi na Mrithishaji mkuu ni Allah (s.w).

Rejea Qur’an (7:128), (57:10)



2. Sheria ya Kiislamu kuhusu mirathi imezingatia nguzo kubwa ya jamii ambayo ni familia.


3. Mirathi katika Uislamu inahusika tu kwa ndugu na jamaa wa karibu wa marehemu kinasaba wenye sifa za kurithi.


4. Kila mwenye sifa za kurithi, ana fungu lake lililokadiriwa kwa madhumuni ya ustawi wa jamii na kujenga mapenzi ya familia.


5. Uislamu umezingatia uhusiano wa karibu na wa mbali wa kinasaba na marehemu ili kila mmoja apate haki na fungu lake analostahili.


6. Mgawo wa mirathi katika Uislamu unazingatia uwiano wa nafasi na majukumu ya kila mwenye fungu ndani ya jamii.


7. Sheria ya Uislamu juu ya kurithi, inazuia kila aina ya upendeleo, dhuluma, unyanyasaji, n.k miongoni mwa warithi.




Hekima ya Mtoto wa Kiume Kupata Mara Mbili ya Mtoto wa Kike

1. Mtoto wa kiume ndiye mwenye majukumu makubwa ya kulea na kuhudumia familia na jamii kwa ujumla.


2. Mtoto wa kiume pia anajukumu la kuwa walii kwa dada zake pindi inapoidhinishwa kwa nafasi hiyo katika kuwaozesha.


3. Mtoto wa kike ikitokea ameachwa (ametalikiwa), kaka yake ndiye muwajibikaji wa kumtunza mpaka atakapoondoka katika himaya yake.

4. Mtoto wa kike pamoja na kuwa na majukumu machache kulinganisha na wa kiume, bado anafursa ya kupata fungu la mahari yake pia.


5. Mtoto wa kike pamoja na kuwa na fursa ya kumiliki mali na rasilimali, bado hana wajibu wowote wa kutuzimia kuhudumia familia ila kwa dharura.




Udhaifu wa Sheria za Kitwaghuti za Kurithi

- Katika jamii za kijahili, wanawake hawana haki na nafasi ya kurithi chochote.

- Katika zama za Jahiliyah, kabla ya kuja Mtume (s.a.w), sio tu wanawake walikuwa hawarithi, bali wao wenyewe walikuwa wanarithiwa kama mali pia.


- Sheria za kitwaghuti juu ya mirathi zimejengeka katika misingi ya upendeleo, dhuluma, unyanyasaji, n.k.


- Sheria za kitwaghuti hazizingatii sifa na vigezo vya warithi kwa marehemu kinasaba ambapo wasiostahiki wanaweza kupewa na wanaostahiki wakakosa.


- Hakuna mafungu maalum ya kurithi katika sheria ya kitwaghuti, bali kwa vigezo vya kijinsia.


- Sheria za kitwaghuti hazizingatii majukumu ya warithi.

Mfano mwanamke hupewa fungu kubwa kuliko mwanaume kwa kigezo kuwa eti hana uwezo wa kuchuma.


- Sheria za kitwaghuti huzingatia, hali ya maisha, uwezo kati ya warithi badala ya ukaribu wa nasaba na vigezo.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1359

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu

Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.

Soma Zaidi...
Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...
Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu.

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
Njia haramu za uchumi.

Njia hizi ni haramu katika kukuza uchumi wako.

Soma Zaidi...
Hijja na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina za Najisi na twahara katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu

Soma Zaidi...