image

Walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi watu walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu, pamoja na kuwepo Kwa sababu zinazopekekea kupata tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ila Kuna watu wenye hali Fulani wako kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu kama

Walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu.

​​​​​​1. Watu wenye matatizo kwenye mfumo wa ubongo au Kwa kitaalamu central nervous system, au Kwa lugha ya kawaida wale ambao wanaanguka kifafa Kwa ujumla.

Kama tulivyoona kwenye Saba za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ni pamoja na kitendo Cha kuhama bakteria kutoka sehemu mbalimbali za mwili na kuingia kwenye mfumo wa hewa na kushambulia mapafu, Kwa hiyo Kwa wanaokuwa na kifafa pengine uanguka chini na kuzilai Kwa hiyo mate kutoka mdomoni yanaweza kuingia sehemu ya mfumo wa hewa na kusababisha bakteria ambao wapo mdomoni na kuingia kwenye mfumo wa hewa na kushambulia mapafu.

Kwa hiyo inawezekana kwenye jamii zetu wagonjwa Hawa tunaishi nao ni ndugu zetu,jamaa na marafiki Kwa hiyo ili kuepuka na tatizo hili ikitokea mgonjwa Kaanguka kifafa ni vizuri kabisa kumlaza vizuri ili kuepuka tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni vizuri kumlaza upange ili mate yadondoke chini au kumlaza Chali na kichwa kuangalia pembenu ili kuepuka mate yasiingie Kwenye mfumo wa hewa.

 

 

2. Pia na wale wenye kikohozi kikali Cha mara Kwa mara na wale wenye matatizo kwenye kumeza.

Kwa upande wa kikohozi Cha Mara Kwa mara wanaweza kukohoa na kusababisha makohozi kuchanganyikana na mate ya mdomoni na baadae kurudi kwenye mfumo wa hewa hasa pale mgonjwa akiwa anakohoa na akapaliwa tena,Kwa hiyo ni vizuri kabisa kutibu kikohozi Kwa watu wenye matatizo hayo .

Kwa upande wa watu wenye matatizo kwenye kumeza na wenyewe wapo hatarini kupata usaha kwenye mapafu Kwa sababu wakiwa wanameza Kwa shida pengine ni Kwa sababu ya maumbile wanaweza kusababisha baadhi ya vyakula kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuingia pamoja na bakteria na kusababisha madhara kwenye mfumo wa.

 

 

 

3. Watumiaji wa madawa ya kulevya na wavutaji wa sigara.

Hawa nao wapo kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu Kwa upande wa wavutaji wa sigara Kuna wakati mwingine wanapovuta ule Moshi ukiingia kwenye  mfumo wa hewa uweza kushambulia mapafu na kusababisha makovu kwenye mapafu hatimaye kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,Kwa hiyo wavutaji wa sigara wanapaswa kuwa makini sana Kwa kupunguza kiwango Cha sigara au ikiwezekana kuacha kabisa Kwa sababu hata kwenye viwanda vya kutengeneza sigara wanakwambia kwamba , sigara ni hatari Kwa afya yako.

 

Vile vile na watumiaji wa madawa ya kulevya nao wanapata madhara Yale yale kama wavutaji wa sigara iwe ni njia ya kuvuta au kujidunga Kwa sindano wote wanapatwa na matatizo hayo hayo,Kwa hiyo elimu ni Bora Kwa wavutaji wa madaw ya kulevya kuhusu madhara kwenye mapafu ili waweze kubadili mfumo wa maisha na kuweza kuachana na hizo bangi.

 

 

4. Watumiaji wa pombe kupita kiasi

Hawa nao wapo hatarini kupata usaha kwenye mapafu,Kwa sababu kwenye pombe Kuna kemikali mbali mbali ambazo mtumiaji anapokuwa anatumia zikifanikiwa kuingia kwenye mapafu usababisha mapafu kushambuliwa na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,na pia zike pombe zinazopikwa kienyeji ni mbaya Zaidi Kwa sababu kemikali yake ni kubwa Zaidi, mbaya Zaidi ni pale mtumiaji anapotumia Kwa kiwango kikubwa na Cha kupitiliza na hatimaye kupoteza fahamu na kuanza kutapika hali ambayo usababisha baadhi ya matapishi kutoka kwenye mmengenyo wa chakula na kuingia kwenye mfumo wa hewa na kusababisha mapavu kushambulia na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

Kwa hiyo wanywaji wa pombe wanapaswa kuwa makini katika matumizi ya pombe na kuwa na kiasi ,wanywe pombe za starehe sio kuzidisha na hatimaye kujiletea matatizo ya ki afya 

 

 

5. Walio na maambukizi kwenye koromeo au Kwa kitaalamu oesophagus.

Kuna wakati mwingine maambukizi kwenye sehemu ya kiromeo usababisha kuwepo na wadudu, wanaweza kuwa bakteria , virus au wadudu wowote wale, kwa hiyo tunapaswa kufahamu kwamba kwenye sehemu ya koromeo wadudu wanaweza kuhama na kwenda kwenye mfumo wa hewa na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

6. Pia na wale wenye Kansa ya mapafu wapo tayari kupata usaha kwenye mapafu.

Kwa Sababu ya kuzalishwa Kwa seli ambazo usababisha kuwepo Kwa kitu kingine kwenye seli za kawaida usababisha kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,Kwa hiyo katika kutoa huduma Kwa wagonjwa wa Kansa ya mapafu ni wazi kwamba kunakuwepo na uwezekano wa kupata usaha kwenye mapafu.

 

 

7. Wale wanaotumia mionzi kwenye matibabu ya Kansa ya mapafu au sehemu yoyote ile inayohusika na mfumo wa upumuaji.

Kwa kawaida katika matumizi ya mionzi kwenye matibabu ya Kansa yoyote ile ya mfumo wa hewa Kuna uwezekano kabisa wa kuharibu mfumo wa hewa ambao uambatana na kuwepo Kwa kemikali inayohusika na kuuua seli ambazo hazihitajiki Kwa kitaalamu huitwa abnormal sell,Kwa hiyo na hali hii usababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

8. Vile vile na watu wenye upungufu wa Kinga mwilini.

Tunafamu kwamba Kinga mwilini ikishapungua Kuna uwezekano kabisa wa kuwepo Kwa magonjwa nyemelezi Kwa hiyo na hii inawezekana kabisa kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu Kwa sababu ya kuwepo Kwa Kinga ndogo kwenye mwili.

 

 

 

9.kuwepo Kwa magonjwa kwenye mfumo wa upumuaji ambayo utumia mda mrefu.

Pengine Kuna tatizo la kuwepo Kwa magonjwa kwenye mfumo wa upumuaji ambayo utumia mda mrefu  na bila matibabu Kwa kitaalamu huitwa prolonged infections of respiratory system,kwa mfano nimonia ya mda mrefu na ambayo haina matibabu nayo inawezekana kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,na vile vile pumu ya mda mrefu hasa hasa kama hakuna matibabu na yenyewe usababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,Kwa hiyo ni vizuri kabisa kutibu magonjwa yote yanayohusika na mfumo wa upumuaji Kwa wakati Kwa sababu bakteria au virusi na maambukizi mengine yote yanaweza kuhama kutoka kwenye sehemu yoyote ile ya mfumo wa hewa na kushambulia mapafu na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

 

10. Upasuaji kwenye mapafu.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na upasuaji kwenye mapafu ili kutoa pafu moja kama limeshambuliwa sana na magonjwa,Kwa kawaida upasuaji wa namna hii uhitaji umakuni wa hali ya juu Kwa wakati mwingine Kuna complications  baada ya upasuaji ambazo usababisha kuwepo Kwa maambukizi kwenye sehemu ya mapafu ambapo upasuaji umefanyika, Kwa hiyo inawezekana pia kwenye pafu ambalo limefanyiwa upasuaji likapatwa ma tatizo kama Hilo la maambukizi na kusababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu Kwa hiyo ni vizuri kabisa baada ya kumaliza upasuaji ni kutumia antibiotics ambazo zina uwezo wa kuzuia maambukizi kwenye mapafu.

 

 

11. Familia kuwa na historian ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

Kuna wakati mwingine na ni Kwa mara chache Kuna familia nyingine unakuta Kuna tatizo hili la kuwepo Kwa wagonjwa wa usaha kwenye mapafu , inawezekana isiwe Kwa familia yote ila akatokea mgonjwa mmoja mmoja mwenye tatizo hili,Kwa hiyo ikitokea kwenye familia ni kuwepo Kwa umakini na matibabu yanapaswa kutokatika kwenye familia hiyo yenye kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,na pia kuhakikisha kuwaleta wagonjwa hospital ili waweze kupata matibabu na vile vile kuepuka inyanyasaji Kwa wagonjwa wa tatizo hilo.

 

 

12. Kwa hiyo hapo juu sio sababu za moja Kwa moja ila ni viashilia au watu walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu.

 

 

 

 

 

 

 

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 375


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Sababu za mtu kuwa na mfadhaiko au wasiwasi
Post hii inahusu sababu za mtu kuwa na mfadhaiko na wasiwasi, mfadhaiko ni nguvu fulani anayoisikia ndani mwake kwa sababu ya tukio la kushutushwa linalomfanya afikilie sana, Soma Zaidi...

VIDONDA VYA TUMBO SUGU
VIDONDA VYA TUMBO SUGU Matibabu ya vidonda vya tumbo mara nyingi hufanikiwa, na kusababisha uponyaji wa vidonda. Soma Zaidi...

Je daktari hizo dalili zamwanzo za HIV hazioneshi kama mwili kupungua
Dalili za HIV zina utofauti na dalili za UKIMWI. Kwani HIV huwezakuonyesha dalili wiki ya pili hadi ya sita baada ya kuathirika kisha zinapotea, lakini dalili za UKIMWI huwezakutokea baada ya miaka 5 hadi 10. Soma Zaidi...

Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo.
Posti hii inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo, tunajua kubwa mama kama ana ugonjwa huu anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Ugonjwa huu. Soma Zaidi...

Dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanaume
Posti hii inakwenda kukuletea dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanaume Soma Zaidi...

Dalili za Ugonjwa wa pombe wakati Mtoto akiwa tumboni
Ugonjwa wa ulevi wakati Mtoto akiwa tumboni (fetasi) ni hali ya mtoto inayotokana na unywaji pombe wakati wa ujauzito wa mama. Ugonjwa wa pombe wa fetasi husababisha uharibifu wa ubongo na matatizo ya ukuaji. Soma Zaidi...

Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia Soma Zaidi...

Msaada kwa wenye Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwahudumia wenye Maambukizi kwenye mifupa, ni njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuwasaidia wenye Maambukizi kwenye mifupa. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili Soma Zaidi...

Ijuwe saratani ya kibofu cha nyongo
Makala hii inakwenda kukufahamishavkuhusu saratani yavkibifu cha mkojo. Soma Zaidi...

Aina za kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari Soma Zaidi...

Je wiki 1 dalili zinaonyesha za maambukizi ya ukimwi na wiki 3 vipimo vinaweza kuonyesha Kama umeasilika
Muda ambao maambukizi ya virusi vya ukimwi kuonyesha dalili unaweza kutofautiana kutika mtu hadi mwingine. Soma Zaidi...