picha

Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,

Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo.

1. Kuchanganyikiwa au kupoteza fahamu

Ni dalili ambayo ujitokeza hasa kama mtu amepatwa na jeraha kwenye ubongo hali hii utofautiana na jeraha kali kwa sababu kupoteza fahamu na kuchanganyikiwa uwa ndani ya masaa ishilini na manne, na baadae mgonjwa uwa kawaida Ila uhisi maumivu katika kichwa kwa hiyo huduma anayopaswa kupewa na dawa ya maumivu na kuendelea kupumzika na hali huwa kama kawaida .

 

2.Kutokumbuka kilichotokea.

Mgonjwa wa jeraha la kawaida hakumbuki kilichotokea kwa sababu pengine anakuwa amepoteza kabisa fahamu kwa hiyo mara nyingi ukumbuka lile tukio la mwanzoni ambalo utokea kwa hiyo mgonjwa akizinduka mara nyingi uuliza Niko wapi na kwa sababu gani kwa hiyo anapaswa kupewa majibu na kuulizia jinsi anavyojisikia na kwa wakati huu anapaswa kupewa mda wa kupumzika na hapaswi kuulizwa maswali mengi kwa sababu anaweza kugongwa na kichwa.

 

3.Kichwa kuuma kizunguzungu na uchovu.

Kwa mgonjwa aliyepata jeraha la kawaida uhisi maumivu ya kichwa, kizunguzungu na uchovu hii ni kwa sababu ya mshutuko ambao utokea kwenye ubongo kwa hiyo mgonjwa anapaswa kupewa dawa ya maumivu Ili kupunguza maumivu ya kichwa na pia hapaswi kutembea tembea kwa sababu ya kizunguzungu na Akitaka  kwenda sehemu inabidi aende na mtu Ili kuepuka kudondoka na kusababisha matatizo mengine na mgonjwa Upata uchovu kwa sababu pengine wakati wa ajali Kuna sehemu alijikwaruza na hali hii utulia ndani ya masaa ishilini na manne.

 

4. Kutoona vizuri au kuona maruweruwe.

Mgonjwa wa majeraha ya kawaida mara nyingi huwa haoni vizuri na kwa wakati mwingine uona maruweruwe kwa sababu ya mshutuko kwenye ubongo ambao upelekea nevu za kwenye macho na kutenguka kidogo na baadae hali hii utulia, kwa hiyo mgonjwa wa namna hii anapaswa kutumia hata kusinzia kabisa na hatimaye hali huwa kawaida.

 

5. Kichefuchefu na kutapika.

Mgonjwa mwenye majeraha ya kawaida uhisi kichefuchefu na kutapika kwa mda hali hii utokea kwa sababu ya mshutuko ambao uingiliana na mfumo wa umengenywaji wa chakula na kwa hiyo hali hii udumu ndani ya masaa ishilini na manne. Kwa hiyo mgonjwa anapaswa kufanyiwa huduma zote za mtu Mwenye Kichefuchefu kama vile kula vyakula vigumu vigumu mfano mkate na chapati na pia kula kidogo kidogo kwa mda mrefu na pia kukaa wima.

 

6.kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wagonjwa wenye majeraha ya kawaida kwenye ubongo dalili zao pengine zinaweza kuogopesha wahudumu wa mgonjwa lakini kwa kawaida udumu ndani ya masaa ishilini na manne na mda unaniofuata mgonjwa huwa kawaida na kuendelea na matibabu hasa kupunguza maumivu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2996

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 ai web app     πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Ni Nini husababisha kinjwaa kutoa harufu mbaya?

Posti hii inaelezea kuhusiana na sababu zinazosababisha kinjwa au mdomo kutoa harufu mbaya?

Soma Zaidi...
MJUE MBU, NA YAJUWE MARADHI MAKUU MATANO (5) HATARI YANAYOAMBUKIZWA NA MBU, malaria kukamata namba moja kwenye maradhi hayo)

Mbu ni katika wadudu ambao husababisja vifo vya maelfu kila mwaka, na mamilioni ya watu wanaathirika na maradhi yaletwayo na mbu.

Soma Zaidi...
Athari za mabadiliko ya misimu (Seasonal Affective Disorder).

Seasonal Affective Disorder (SAD)β€”aina ya sonona inayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa na misimu. Makala haya yanachambua dalili zake, sababu za kisayansi, na jinsi ya kukabiliana nayo ili ubaki na furaha na utulivu mwaka mzima.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa hepatitis C

Hepatitis C ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoshambulia ini na kusababisha kuvimba. Watu wengi walioambukizwa na virusi vya Hepatitis C (HCV) hawana dalili. Kwa kweli, watu wengi hawajui kuwa wana maambukizi ya Hepatitis C hadi uharibifu wa ini

Soma Zaidi...
Sababu za Maumivu ya shingo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu.

Soma Zaidi...
Nini sababu ya kuchubuka midomo na kuwa myeupe

Kama una tatizo la midomo kuchubuka na kuwa myeupe ama kuwa na vidonda. Post hii inakwenda kuangalia swala hili.

Soma Zaidi...