Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo.
1. Kuchanganyikiwa au kupoteza fahamu
Ni dalili ambayo ujitokeza hasa kama mtu amepatwa na jeraha kwenye ubongo hali hii utofautiana na jeraha kali kwa sababu kupoteza fahamu na kuchanganyikiwa uwa ndani ya masaa ishilini na manne, na baadae mgonjwa uwa kawaida Ila uhisi maumivu katika kichwa kwa hiyo huduma anayopaswa kupewa na dawa ya maumivu na kuendelea kupumzika na hali huwa kama kawaida .
2.Kutokumbuka kilichotokea.
Mgonjwa wa jeraha la kawaida hakumbuki kilichotokea kwa sababu pengine anakuwa amepoteza kabisa fahamu kwa hiyo mara nyingi ukumbuka lile tukio la mwanzoni ambalo utokea kwa hiyo mgonjwa akizinduka mara nyingi uuliza Niko wapi na kwa sababu gani kwa hiyo anapaswa kupewa majibu na kuulizia jinsi anavyojisikia na kwa wakati huu anapaswa kupewa mda wa kupumzika na hapaswi kuulizwa maswali mengi kwa sababu anaweza kugongwa na kichwa.
3.Kichwa kuuma kizunguzungu na uchovu.
Kwa mgonjwa aliyepata jeraha la kawaida uhisi maumivu ya kichwa, kizunguzungu na uchovu hii ni kwa sababu ya mshutuko ambao utokea kwenye ubongo kwa hiyo mgonjwa anapaswa kupewa dawa ya maumivu Ili kupunguza maumivu ya kichwa na pia hapaswi kutembea tembea kwa sababu ya kizunguzungu na Akitaka kwenda sehemu inabidi aende na mtu Ili kuepuka kudondoka na kusababisha matatizo mengine na mgonjwa Upata uchovu kwa sababu pengine wakati wa ajali Kuna sehemu alijikwaruza na hali hii utulia ndani ya masaa ishilini na manne.
4. Kutoona vizuri au kuona maruweruwe.
Mgonjwa wa majeraha ya kawaida mara nyingi huwa haoni vizuri na kwa wakati mwingine uona maruweruwe kwa sababu ya mshutuko kwenye ubongo ambao upelekea nevu za kwenye macho na kutenguka kidogo na baadae hali hii utulia, kwa hiyo mgonjwa wa namna hii anapaswa kutumia hata kusinzia kabisa na hatimaye hali huwa kawaida.
5. Kichefuchefu na kutapika.
Mgonjwa mwenye majeraha ya kawaida uhisi kichefuchefu na kutapika kwa mda hali hii utokea kwa sababu ya mshutuko ambao uingiliana na mfumo wa umengenywaji wa chakula na kwa hiyo hali hii udumu ndani ya masaa ishilini na manne. Kwa hiyo mgonjwa anapaswa kufanyiwa huduma zote za mtu Mwenye Kichefuchefu kama vile kula vyakula vigumu vigumu mfano mkate na chapati na pia kula kidogo kidogo kwa mda mrefu na pia kukaa wima.
6.kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wagonjwa wenye majeraha ya kawaida kwenye ubongo dalili zao pengine zinaweza kuogopesha wahudumu wa mgonjwa lakini kwa kawaida udumu ndani ya masaa ishilini na manne na mda unaniofuata mgonjwa huwa kawaida na kuendelea na matibabu hasa kupunguza maumivu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Kitau cha Fiqh π4 Dua za Mitume na Manabii π5 ai web app π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Ishara za Mpenzi Asiye Mwaminifu
βKuhisi mashaka katika mahusiano ni jambo linaloweza kuleta fadhaa kubwa. Post hii inachunguza ishara mbalimbali za tabia zinazoweza kuashiria kutokuwa mwaminifu, huku ikisisitiza umuhimu wa mawasiliano na ushahidi kabla ya kuhukumu.
Soma Zaidi...Faida za Kunywa Maji Mengi Kila Siku
βMaji ni kiini cha uhai na yanachukua zaidi ya nusu ya uzito wa mwili wa binadamu. Post hii inaangazia umuhimu wa kunywa maji ya kutosha kila siku, jinsi yanavyosaidia utendaji kazi wa viungo vya mwili, na vidokezo vya kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha
Soma Zaidi...Kucha langu LA mguu linang'ooka...nini chaweza kuwa tatizo
Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?
Soma Zaidi...Ni Nini husababisha kinjwaa kutoa harufu mbaya?
Posti hii inaelezea kuhusiana na sababu zinazosababisha kinjwa au mdomo kutoa harufu mbaya?
Soma Zaidi...Yajue magonjwa ya jicho
Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya jicho,ni Magonjwa ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za jicho kwa mfano kwenye retina,kuaribu mishipa ya retina ,macho kuwa makavu na pia mtoto wa jicho, hali hii ya magonjwa ya macho Usababisha madhara mbalimbali kama
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, ni madhara ambayo yanaweza kutokea iwapo maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo hayatatibiwa kwa wakati.
Soma Zaidi...