picha

fangasi wa kwenye Mdomo na koo

fangasi wa kwenye Mdomo na koo

fangasi wa kwenye Mdomo na koo

  1. Fangasi hawa wa kwenye mdomo watambulikao kama thrush ama oropharyngeal candidiasis wanaweza kuishi kwenye koo na tundu zima la koo kuelekea kwenye tumbo na hawa wanajulikana kama esophageal candidiasis ama candida esophagitis. Fangasi hawa ni maarufu sana kwa watu wanaoishi na HIV ana UKIMWI.

 

Dalili za fangasi hawa

  • Kuwa na madoa meupe kwenye sehemu ya ndani ya shavu, ulimi, sehemu ya juu ya mdomo, na koo.
  • Unahisi kama kuna pambai kwenye mdomo
  • Kupetea kwa ladha ya unachokila
  • Maumivu wakati wa kula ama kumeza
  • Kupasuka na kuwa wekundu kwenye kona za mdomo

 

Walio hatarini kupata fangasi hawa:

Fangasi hawa si kawaida sana kuwapata watu wenye afya madhubuti. Ijapokuwa wapo watu ambao wapo hatarini sana kupata fangasi hawa kama watoto chini ya umri wa mwaka mmoja, na watu wenye matatizo ya kiafya kam wenye:-

  • Watu wanaotumia meno bandia
  • Watu wenye kisukari
  • Watu wenye saratani
  • Watu wenye HIV ama UKIMWI
  • Watu wanaotumia dawa amazo zinakausha mdomo
  • Watu wanaovuta sigara.
  • Watu wanaotumia dawa za kupulizia za pumu

 

Njia ya kupambana na fangasi hawa:

Wengi wanaopata fangasi hawa ni wale ambao mfumo wao wa kinga umeathirika hivyo miili yao haiwezi kupambana vyema na mashambulizi. Hivyo kupambana na fangasi hawa hakikisha unaweka mwili wako katika hali njema ya kiafya. Muone daktari akuelekeze namna ya kuboresha afya yako. Pia piga mswaki kila unapotumia dawa ya kupulizia ya pumu. Wacha kuvuta sigara.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 8213

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za kifua kikuu (tuberculosis)

Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kiafya yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Kwa binadamu sababu ya kawaida ni Mycobacterium tuberculosis.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya njia ya mkojo kwa wanawake

​Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) ni moja kati ya changamoto kubwa za kiafya zinazowasumbua wanawake wengi kote ulimwenguni. Makala haya yanajadili kwa kina vyanzo vya maambukizi haya, dalili zake, sababu zinazowafanya wanawake kuwa katika hatari zaidi, mbinu za kujikinga, na ufafanuzi wa ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu zilizopo kwenye jamii.

Soma Zaidi...
YAJUE MARADHI YA KISUKARI

Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Dalili za Mapenzi ya Kweli

Mapenzi ya kweli ni zaidi ya hisia za kupagawa; ni uamuzi wa kudumu na kujitolea. Posti hii inachunguza alama kuu zinazotofautisha mapenzi ya dhati na mazoea, ikisisitiza umuhimu wa heshima, uaminifu, na ukuaji wa pamoja katika mahusiano.

Soma Zaidi...
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake

Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kumfurahisha Mwenza Wako

Mahusiano yenye furaha hayajitokezi kwa bahati; yanajengwa kupitia juhudi za makusudi. Posti hii inatoa mwongozo wa mbinu rahisi lakini zenye nguvu za kumfanya mwenza wako ajihisi anathaminiwa, anapendwa, na anafurahia maisha ya pamoja nawe.

Soma Zaidi...