fangasi wa kwenye Mdomo na koo
fangasi wa kwenye Mdomo na koo
- Fangasi hawa wa kwenye mdomo watambulikao kama thrush ama oropharyngeal candidiasis wanaweza kuishi kwenye koo na tundu zima la koo kuelekea kwenye tumbo na hawa wanajulikana kama esophageal candidiasis ama candida esophagitis. Fangasi hawa ni maarufu sana kwa watu wanaoishi na HIV ana UKIMWI.
Dalili za fangasi hawa
- Kuwa na madoa meupe kwenye sehemu ya ndani ya shavu, ulimi, sehemu ya juu ya mdomo, na koo.
- Unahisi kama kuna pambai kwenye mdomo
- Kupetea kwa ladha ya unachokila
- Maumivu wakati wa kula ama kumeza
- Kupasuka na kuwa wekundu kwenye kona za mdomo
Walio hatarini kupata fangasi hawa:
Fangasi hawa si kawaida sana kuwapata watu wenye afya madhubuti. Ijapokuwa wapo watu ambao wapo hatarini sana kupata fangasi hawa kama watoto chini ya umri wa mwaka mmoja, na watu wenye matatizo ya kiafya kam wenye:-
- Watu wanaotumia meno bandia
- Watu wenye kisukari
- Watu wenye saratani
- Watu wenye HIV ama UKIMWI
- Watu wanaotumia dawa amazo zinakausha mdomo
- Watu wanaovuta sigara.
- Watu wanaotumia dawa za kupulizia za pumu
Njia ya kupambana na fangasi hawa:
Wengi wanaopata fangasi hawa ni wale ambao mfumo wao wa kinga umeathirika hivyo miili yao haiwezi kupambana vyema na mashambulizi. Hivyo kupambana na fangasi hawa hakikisha unaweka mwili wako katika hali njema ya kiafya. Muone daktari akuelekeze namna ya kuboresha afya yako. Pia piga mswaki kila unapotumia dawa ya kupulizia ya pumu. Wacha kuvuta sigara.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 ai web app 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Maumivu ya kiuno na dalili zake
Posti hii inahusu zaidi maumivu ya kiuno na dalili zake, ni maumivu ambayo utokea kwenye kiuno na kusababisha madhara mbalimbali katika mwili,
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitovuni
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni
Soma Zaidi...Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
Soma Zaidi...Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Nini kinasababisha kizunguzungu?
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu
Soma Zaidi...Madhara ya maumivu kwenye nyonga na kiuno.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa matibabu kwenye nyonga na kiuno hayatafanyika.
Soma Zaidi...