Mimba hatari iliyotungia nje ya mji wa mimba, ni zipi dalili zake na ni kivipo mimba inatungia nje?

Mimba ya namna hii kitaalamu hufahamika kama ectopic pregnancy. Je hii ni mimba gani? Hii ni mimba ambayo yai lililorutubishwa linaendelea kukuwa nje ya mji wa mimba (uterus). mimba inaweza kukuwa sehemu yeyote kwenye tumbo ila nje ya mji wa mimba. Kwa asilimia kama 90% mimba hukuwa kwenye mirija ya falopia. Hii ni mimba hatari sana na inahitaji uangalizi wa haraka sana, kwani inaweza kuhatarisha maisha ya mama. Inakadiriwa kuwa mimba za namna hii huchukuwa kati ya asilimia 1 mpaka 2 ya miba zote.
Kwa nini mimba hii ni hatari?
1.Mimba inatkuwa nje ya mji wa mimba hivyo haiwezekani mtoto kupona
2.Inaweza kusababisha kupasuka kwa mirija ama sehemu ilipokuwa.
3.Inaweza kusababisha ulemavu kwa mama endapo itachelewa kuonekana
4.Kwa asilimia 30 mimba hii haina dalili hii ni hatari zaidi.
5.Inaweza kusababisha uvujaji wa damu kwa kiasi ikubwa
6.Inaweza kusababisha mwanamke kuhitajiwa kufanyiwa upasuaji kamma tiba.
Sababu za kutokea mimba hii
Kama nilivyotangulia kukueleza kuwa asilimia 30 ya mimba hizi hazina dalili. Lakini kwa kiasi kikubwa mimba hizi huwa na dalili. Tafiti zinaonyesha kuwa dalili zake hutokea kabla ya wiki ya 10. Sasa hapa nitakutajia baadhi tu ya dalili za mimba hii:-
1.Maumivu ya tumbo upande mmoja wa nyonga.
2.Maumivu ya mabega
3.Kutokwa na damu kwenye uke.
4.Maumivu ya nyonga.
5.Mvurugiko wa tumbo na kutapika
6.Maumivu ya upande mmoja wa mwili.
7.Kizunguzungu na uchovu
8.Maumivu ya mabega, shingo na mkundu.
Sababu za kutokea kwa mimba hii.
1.Kuwa na maambukizi kwenye via vya uzazi yaani PID
2.Uvutaji wa sigara
3.Kama una umri wa miaka 35 na kuendelea
4.Kama unatumia madawa ya kuivisha mayai
5.Kama ulishapata ujauzito huu hapo mwanzo upo uwezekano kuja kupata tena
6.Kama ulifanyiwa upasuaji kwenye mirija ya falopia
7.Kama una tatizo la endometriosis
8.Baadhi ya njia za kuthibiti uzazi mfano, IUD
Nini tena yapasa kujuwa?
1.Ujauzito uliotungia njea haurithiwi yaani kama mama aliwahikupata ujauzito huu hali hii hairithiwi.
2.Kutoka kwa ujauzito sio sababu ya kupata mimba hii
3.Kutoa ujauzito pia hakuna mahusianao na ujauzito huu
4.Mazoezi na michezo pia hihusiani na kutokea kwa ujauzito huu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.
Soma Zaidi...Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.
Soma Zaidi...