Utaratibu kwa wajawazito na wanaonyonshesha wakiwa na virusi vya ukimwi na ukimwi

Je kuna madhara kwa mwenye virusi vya ukimwi kunyonyesha ama kubeba mimba, na nini afyanye kama ameshabeba mimba ama kama ananyonyesha

Utaratibu kwa wajawazito na wanaonyonshesha wakiwa na virusi vya ukimwi na ukimwi



MWANAMKE MWENYE VIRUSI VYA UKIMWI AKIWA MJAMZITO AMA ANAVYOVYESHA.




Watu wengi wamekuwa kijiuliza sana kuhusu hatma ya ujauzito kwa mwenye virusi vya ukimwi. Je ni kiasi gani mtoto aliye tumboni atakuwa salama?. ni tahadhari gani mjamzito mwenye virisi vya ukimwi achukuwe. Na atakapojifunguwa ni muda gani ataendelea kunyonyesha? Katika kipengele hiki tutaangalia kwa ufupi habari hii kama ifuatavyo:-



1.Je inawezekana kushiriki tendo la ndoa na aliyeathirika bila ya kupata HIV/UKIMWI?
Yes inawezekana, na hili ni swali watu wengi wamekuwa wakijiuliza. Itambulike kuwa kushiriki tendo la ndoa na aliyeathirika si lazima kuwa nawe utaathirika, ila kauli hii isieleweke vibaya. Kwani njia ambayo inaongoza leo katika kueneza maambukizi ya HIV ni kushiriki tendo la ndio. Mtu anaweza kushiriki tendo la ndoa na aliyeathirika bila ya kuathirika endapo:-



A.Endapo hakutatokea michubuko wakati wa tendo
B.Endapo muathirika ametumia dawa za ART kwa muda mrefu kwa kufuata masharti hata viral load yake ikawa haionekani (undetected) na akadumu kwa hali hii walau miezi 6
C.Endapo walitumia kinga wakati wa kushiriki tendo.



2.Je HIV ma UKIMWI hupelekea mimba kutoka?
Inategemea, ila kwa ufupi HIV na UKIMWI huhatarisha ujauzito endapo muathirika hatakuwa mwangalifu ama hatafata maelekezo vyema. Wajawazito walioathirika inashauriwa wafike kituo cha afya mapema sananili kupatiwa maelekezo jinsi ya kulea mimba yake kwa usalama bila ya kuathiri afya ya ujauzito wake. Hata hivyo wanatakiwa wafuate maelekezo vyema.



3.Je maisha ya mtoto yapo hatarini endapo mama mjamzito ana HIV na UKIMWI?
Ni kweli kama mama mjamzito hatakuwa makini, anaweza kuweka maisha ya mtoto wake hatarini. Na si maisha ya mtoto tu bali hata maisha yake pia.



4.Je mtoto anapataje HIV na UKIMWI kutoka kwa mama?
A.Wakati wa kujifunguwa kama kuna kosa litafanyika.
B.Wakati wa kumnyonyosha kuanzia miezi sita toka kuzaliwa mtoto
C.Wakati wa kumlea kama mama hatakuwa makni



5.Kwa nyakati za sasa wajawazito wote wanatakiwa kuzalia kwenye kituo cha afya maalumu. Hii ni kwa ajili ya kupunguza maambukizi ya HIV kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Hatahivyo wakunga wa jadi pia wamepatiwa mafunzo maalumu kwa ajili ya dharura. Ila inalazimika kwa mwenye HIV afanye juu chini azalie hospitali kwa usalama zaidi wa mtoto wake.



6.Je kunyonyesha mtoto kunawza kumuambukiza HIV?
Yes inawezekana, hata hivyo mama akiwa makini na maelezo aliyopewa, katu hatoweza kumuambukiza mwanaye. Inashauiwa mtoto kunyonya kwa muda wa miezi 6 tu ama chini ya hapo. Ni kuwa endapo mtoto atakuwa na michubukomdomoni ama tumboni.



7.Mama asimchanganyie mtoto ziwa lake, maziwa ya kopo na chakula. Kama ataamuwakumnyonyesha ndani iwe ni ndani ya miezi 6 tu na asimpe chakula chochote. Na kama ameamuwa kumpa chakula asimnyonyeshe tena. Na kama ameamuwa kumpa maziwa ya makopo ampe hayo tu na asimnyonyeshe. Anaweza kuchanganya chakula na maziwa ya kopo ama ya ng’ombe na si yake na kitu chingine chochote. Mama awe makini sana na jambo hili, asimchanganyie mtoto maziwa yeke na kitu kingine chochote. Hali hii inaweza kusababisha michubuko mdomoni ama tumboni na kusababisha kupata maambukizi.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1875

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito

Soma Zaidi...
Zifahamu sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube, ni sababu ambazo ufanya mirija ya follapian tube kuziba.

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.

Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v

Soma Zaidi...
Je mwanamke anaweza kujijuwa ni mjamzito baada ya muda gani.

Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil

Soma Zaidi...
Je mwanamke anaweza pata mimba ikiwa wakati watendo la ndoa hakukojoa Wala kusikia raha yoyote ya sex wakati watendo landoa

Je wewe ni mwanmake unayepata shida kufika kileleni? (Kukojoa wakati wa tendo lwa ndoa). Post hii itakujibu baadhi ya maswali yako.

Soma Zaidi...
mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt

Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo.

Soma Zaidi...
Tiba mbadala ya fangasi wa uumeni

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala ya fangasi wa uumeni

Soma Zaidi...
Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...
Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha

Soma Zaidi...