SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)
Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.
SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA
Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka. Yaani karibia robo ya mimba zinazopatikana hutoka. Kitendo hiki cha kutoka kitaalamu huitwa misscarriage. Hiki ni kitendo cha kupotea kwa ujauzito kabla ya wiki ya 20.
Sababu za kutoka kwa mimba:
- Sababu za kurithi (genetics): hutokea mwanamke akarithi hizi sabau kutoka kwenye familia yake. Sababu hizi huenda zikapelekea matatizo ambayo baadaye huchangia mimba kutoka. Matatizo haya ni kama
- Mtoto kutokuendelea kukuwa tumboni
- Kiini tete (embriyo) kutokutengenezwa
- Placenta kuwa kubwa zaidi tofauti na kawaida.
- Afya ya mama; hutokea mwanamke mjamzito afya yake ikawa ni sababu ya ujauzito wake kutoka. Mwanamke akiwa na maradhi yafuatayo ujauzito wake unaweza kuwa hatarini:
- Kisukari
- Maradhi ya moyo
- Presha ya kupanda (hypertension)
- Maradhi ya figo
- Maambukizi; mwanamke mjamzito anweza kuweka ujauzito wake hatarini kama atakuwa na maambukizi ama mashambulizi ya maradhi kama:
- Chlamydia
- Gonoria
- Syphilis
- Malaria
- Ukimwi
- Udhaifu wa cervix; cervics ni mlango wa nyumba ya mimba.
- PCOS (Polycystic Ovary Syndrome). hii hupelekea ovary kuwa kubwa tofauti na kawaida. Ovary ndio sehemu ambayo mayai ya mwanamke hutengenezwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za mimba changa
Zijuwe dalili 17 za mimba na mimba changa, kuanzia siku ya kwanza mpaka mwezi mmoja
Soma Zaidi...Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Ndug mi naitaj ushauri mimi nishaingia kwenye tendo dakika 7 tu nakua nishafika kilelen naomba ushauri ndugu
Kama unadhani una tatizo la kuwahi kufika kileleni basi post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Dalili za Ujauzito mchanga Siku Saba Baada ya Ovulation
Unaweza kujiuliza ikiwa inawezekana kupata dalili za ujauzito mchanga kama siku 7 baada ya kudondoshwa kwa yai (DPO yaani Days Past Ovulation).
Soma Zaidi...Magonjwa ya kwenye ovari na Dalili zake.
Post hii inahusu zaidi Magonjwa yanayoshambulia sana ovari na Dalili zake, haya ni magonjwa ambayo yanashambulia sana ovari ni kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Soma Zaidi...