Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kujifungua hatua kwa hatua
DALILI ZA KUJIFUNGUWA HATUA KWA HATUWA:
Ni ndoto za wanawake wengi siku moja abebe ujauzito, azae mtoto kisha aitwe mama. Haswa hata wanaume hupendelea hivyo. Ila mwanamke anapofikia kujifunguwa hapa ndipo kizaazaa huonekana. Sasa makala hii itakwenda kukueleza dalili za kujifunguwa.
Daliili za kukaribia kujifunguwa kwa siku kadhaa1.Maumivu ya nyonga kuongezeka2.Uchovu kuongezeka3.Kutoa damu yenye utelezi4.Viungo kuachia5.Njia ya kuzalia kutanuka zaidi.6.Maumivu ya tumbo kuongezeka.7.Maumivu ya tumbi na kutungwa.8.Kuharisha9.Maumivu ya mgongo kuongezeka
Dalili za kujifunguwa kwa masaa machache:1.Mikazo ya tumbo inayotokea katika muda maalumu2.Kutokwa na damu yenye utelezi3.Kutokwa na utelezi kwa wingi4.Njia kuachia zaidi5.Mtoto kushuka karibu na njia ya kutokea.
Uchungu wa kujifunguwa:Uchungu wa kujifunguwa hauwezi kuelezeka kwa maandishi machache haya. Hata hivyo kuna machache naweza kukueleza ijapokuwa huwenda usiwe uhalisia. Kujifunguwa kunapitia hatuwa kuu tatu ambazo ni kama ifuatavyo:-
1.Katika hatuwa ya kwanzacevix (mlango wa mimba) hulegea na kufumguka kwa sentimita 10. hata hivyo kulegea kwa cevix kunaweza kuanza siku chache nyma, kidogo kidogo. Majimaji yanayotoka ukeni huongezeka baada ya kupasuka kwa utando uliomzunguka mtoto. Katika hatuwa hii mikazo ya tumbo la kujifunguwa yanaweza kuwa makali sana ndani ya sekunde 30 mpaka 60 kisha yanakata kwa dakika kama 4 ama 5 kisha huanza tena kama hivi.
Katika hatuwa hii maumivu yanaweza kuwa makali sana kiasi cha kuwa kama vile hayakati. Hapa mtoto anaanza kusogea kwenye njia ya kuzalia. Wakati huu atakuwa ana sukumana na njia ya haja kubwa na hapa mwanamke anaweza kujisikia kuenda haja kubwa. Baadhi ya wanawake walio mara ya kwanza kupata ujauzito wanaweza kwenda chooni na hatimaye anazalia chooni. Kumbuka mikazo ya tumbo haupoi hata kwa dawa za kukata maumivu.
2.Hatua hii ya piliHatuwa hii huanzia toka pale mlango wa kuzalia unapofunguka hadi mwisho (sentimita 10) mpaka mtoto atakapozaliwa. Mikazo ya tumbo katika hatuwa hii inazidi na kuwa katika mpangilio maalumu kwa kuachana. Kila mkazo unapokuwa mkubwa hapa mwanamke atajihisi kusukuma mtoto. Hapa mwanamke atahisi moto kwenye uke wake wakati mtoto anashuka ama atahisi kutanuka kwa uke wake hasa pale kichwa cha mtoto kinapoanza kutoka.
Kipindi hiki mama mamzito atakuwa anapewa maelekezo kuhuku kusukuma mtoto ili kuwezehsa kuzaa kwa haraka. Kuna mengi ambayo daktari ama anayezalisha atatakiwa kuyafanya hapa ili kuwezesha kujifunguwa kwa salama. Mtoto ataanza kutokeza kichwa kisha shingo ikifuatiwa na mabega na baadaye mwili kumalizia. Katika hatuwa hii wahudumu wa afya huwa makini zaidi maana ndio hatuwa yenye hatari sana. Hatuwa hii kwa wanawake ambao ndio ujauzito wao wa kwanza inaweza kuchukuwa lisaa limoja mpaka masaa mawili (1 - 2)
3.Hatuwa ya tatuHatuwa hii huanza pale mwanamke atakapojifunguwa. Hatua hii huhu huhusisha kutowa placent, ama kondo la uzazi. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka dakika 30. upotevu wa damu hapa utaendelea kuwepo ijaokuwa si mkubwa. Mikazo ya tumbo la uzazi itasaidia kupunguza upotevu wa damu. Kitukibaya zaidi katika hatuwa hii ni endapo damu itatoka kwa wingi.
Hali hii inaweza kupelekea tatizo lijulikanalo kama postpartum haemorrhage na kupelekea upungufu wa damu na uchovu. Hivyo wakunga na wahudumu wataendelea kuwa makini sana katika hatuwa hii. Katika hatuwa hii ndipo mtoto atatenganishwa na placenter.
NINI UFANYE UKIWA KATIKA UCHUNGU WA KUJIFUNGUA KATIKA1.Kunywa maji ama juisi kwa wingi ama chai2.Unaweza pia kula kitu kitamu cha kufyonza kama utaruhusiwa. Hii ni kwa ajili ya kukuongezea nguvu3.Badilisha mikao kuaa, kulala, ubavuubavu, chalichali, kusimama na kukaa na kadhalika)4.Kama utaweza kuoga maji ya moto fanya hivyo kabla ya kuingia leba5.Mwambie msimamizi wako kama ataruhusiwa kuingia akufanyie maseji mgongoni ana akusuguesugue6.Jitahidi kurilax kati ya mikazo ya tumbo usisukume mtoto mpaka uambiwe kufanya hivyo7.Unaweza kuomba dawa za maumivu kama utaruhusiwa.8.Usione aibu hata kidogo ukiwa katika leba. Hao unaowaonea aibu wameshaona kila kitu kwako na kwa watu wengine. Kama unataka kulia lia sana, tambuwa kuwa kila kitakachokutokea hapo ni siri na katu hakuna atakayehadithia, hata hivyo kila kitu ni kawaida sana katika leba.9.Fuata maelekezo kama utakavyoambiwa na wahudumu wako. Kosa lolote utakalofanya kumbuka linaweza kuhatarisha maisha yako na ya mtoto wako.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dalili za mimba kutoka, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mimba zote ambazo utaka kutoka kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Idadi ya siku hatari za kupata mimba hutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja namwinhine. Kinda ambao idadivyavsikuvzao za hatari ni nyingi kuliko wengine.
Soma Zaidi...Kupata Ukimwi ama HIV hufungamana na mambo mengi. Si kila anayefanya ngono zembe nabmuathiria naye lazima aathirike. Hiivsibkweli, ila tangu kuwa hali hii ni hatari kwani kupata maambukizi ni rahisi sana.
Soma Zaidi...Nitakujiza dawa ya chango na maumivu ya tumbo lahedhi, dalili zake na njia za kukabiliana na maumivu ya tumbo la chango.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba katika mwezi was kwanza
Soma Zaidi...