Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kutoa elimu kwa watu ili kuweza kuwajulisha watu kuwepo kwa ugonjwa huu, namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine jinsi unavyoweza kutibiwa na mbinu au njia za kuzuia Ugonjwa huu ili usiendelee kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
2. Pia kama kuna Dalili za kuwepo kwa Ugonjwa huu kwenye jamii, jamii inapaswa kuepukana na mikusanyiko isiyo ya lazima ili kuepuka madhara makubwa ambayo yanaweza kutokea kama mtu mmoja ana Ugonjwa huu kwenye mkusanyiko anaweza kusambaza kwa wengine na kusababisha kuendelea kuwepo kwa Maambukizi.
3. Kuwaelimisha watu kuacha tabia za kugusana moja kwa moja ambazo zinaweza kusababisha kuenea kwa Ugonjwa huu kwa mfano kubusiana, na pia kwa wale wenye tatizo hili hawapaswi kutema tena mate ovyo wawe na sehemu maalum kwa ajili ya kuweka mate siyo kuyasambaza hali ambayo Usababisha kuendelea kuenea kwa ugonjwa na kuweza kuongeza namba ya waathirika wa Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
4. Pia madawa ya kutibu Ugonjwa huu yanapaswa kuwepo na pia kila aina ya kipimo inapaswa kuwepo ili kuweza kutambua visababishi mbalimbali,na pia kwa upande wa watoto wadogo wanapaswa kutolewa chanjo mapema ili kuweza kuwa na kinga ya kupambana na ugonjwa huu endapo utatokea .
5. Kwa wale wenye imani tofauti au potofu kuhusu Ugonjwa huu ni lazima waache ili kuweza kuwapeleka wagonjwa hospitalini na kupata matibabu mapema ili kuokoa maisha kwa sababu Ugonjwa huu bila matibabu yoyote hali inaweza kuwa mbaya na hatimaye kuwapoteza wapendwa wetu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya makende kushindwa t, hiki ni tatizo na huleta madhara
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kichaa cha mbwa ni virusi hatari vinavyoenezwa kwa watu kutoka kwa mate ya wanyama walioambukizwa. Virusi vya kichaa cha mbwa kawaida hupitishwa kwa kuuma.
Soma Zaidi...SABABU ZA KUTOKEA KWA VIDONDA VYA TUMBO Sababu za kawaida za vidonda vya tumbo ni maambukizo na bakteria Helicobacter pylori (H.
Soma Zaidi...AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha dalili na mabo ya hatari kwenye ugonjwa wa saratani ya mdomon.Saratani ya mdomo inarejelea Kansa inayotokea katika sehemu zozote zinazounda mdomo. Saratani ya mdomo inaweza kutokea kwa: Midomo, Fizi, Lugha, Nd
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Naomba kuuliza swaliJe mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika.
Soma Zaidi...