Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kutoa elimu kwa watu ili kuweza kuwajulisha watu kuwepo kwa ugonjwa huu, namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine jinsi unavyoweza kutibiwa na mbinu au njia za kuzuia Ugonjwa huu ili usiendelee kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
2. Pia kama kuna Dalili za kuwepo kwa Ugonjwa huu kwenye jamii, jamii inapaswa kuepukana na mikusanyiko isiyo ya lazima ili kuepuka madhara makubwa ambayo yanaweza kutokea kama mtu mmoja ana Ugonjwa huu kwenye mkusanyiko anaweza kusambaza kwa wengine na kusababisha kuendelea kuwepo kwa Maambukizi.
3. Kuwaelimisha watu kuacha tabia za kugusana moja kwa moja ambazo zinaweza kusababisha kuenea kwa Ugonjwa huu kwa mfano kubusiana, na pia kwa wale wenye tatizo hili hawapaswi kutema tena mate ovyo wawe na sehemu maalum kwa ajili ya kuweka mate siyo kuyasambaza hali ambayo Usababisha kuendelea kuenea kwa ugonjwa na kuweza kuongeza namba ya waathirika wa Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
4. Pia madawa ya kutibu Ugonjwa huu yanapaswa kuwepo na pia kila aina ya kipimo inapaswa kuwepo ili kuweza kutambua visababishi mbalimbali,na pia kwa upande wa watoto wadogo wanapaswa kutolewa chanjo mapema ili kuweza kuwa na kinga ya kupambana na ugonjwa huu endapo utatokea .
5. Kwa wale wenye imani tofauti au potofu kuhusu Ugonjwa huu ni lazima waache ili kuweza kuwapeleka wagonjwa hospitalini na kupata matibabu mapema ili kuokoa maisha kwa sababu Ugonjwa huu bila matibabu yoyote hali inaweza kuwa mbaya na hatimaye kuwapoteza wapendwa wetu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.
Soma Zaidi...Fangasi na Aina zao Fangasi wa kwenye kucha Fangasi wa Mapunye Fangasi aina ya candida Fangasi wa Mdomoni na kooni Fangasi wa kwenye uke Fangasi wanaoshambulia mfumo wa damu na ogran kama moyo, figo n.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia ugonjwa wa madonda ya koo,ni njia ambazo usaidia katika kujikinga na ugonjwa wa madonda ya koo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Soma Zaidi...